Clouds FM kufungiwa?

watakua hawajawaonea,wamezidi kuingilia hasa mambo ya siasa,tena kwa kuegemea chama fulani,kwani ni nani asiyewafahamu kazi yao kusifia tu viongoz wa ccm,kwa nini wasitafute mada za msingi za kuongelea mpaka wazungumzie watu binafsi,au wanahongwa ili kufanya hivyo.nadhani TCRA ikemee tabia hizi kwa sababu ni kero kubwa kwa jamii.

mkuu punguza jazba, inachofanya clouds ni sawa na magazeti ya uhuru, tanzania daima nk,
na humu jf wengi mnatatizwa na kipindi kimoja tu ambacho ni jahazi
kama unasikiliza asubuhi wana power break fast, humo nikukosoa serikali kwa kwenda mbele.
Kuna leo tena, karibu 80% ya wanawake hapa dar wanasikiliza.
Kisha kuna xxl, vijana karibu wote town hii ndio kipindi yao,
sasa kuna jahazi, hapa ndipo jf wanapochefuka simple kwasababu ya mtu mmoja tu, kibonde.
Kisha vipindi vinavyofuata ni miziki na michezo.
Jf kama great thinker sioni mantiki ya kila siku kupost mambo ya clouds na kuyapa kipaumbele utadhani issue ya maana, hii ni radio ya burudani siasa ni by the way.
Hakuna ubaya wowote kwa wao kuegemea ccm kama ilivyo sahihi kwa tanzania daima kuegemea chadema,
naomba niwe mkweli napenda kusikiliza clauds kama kituo cha burudani na nina hakika wengi wetu humu ndani niwasikilizaji wazuri wa clouds thats why chochote kitakacho jiri clouds utakikuta humu jf.
Na kama unajidanganya kuwa haipendwi jaribu kufanya jautafiti kadogo, pita uswahilini, panda madaladala utapata majibu
 
haifai kuwa redio ya kusikiliza bali inatakiwa iwe kijarida cha kitchen part tu................akina kibonde wanaharibu sana redio na mimi niliishaacha kusikiliza tangu niliipoona kuwa wamenunuliwa na mafisadi na ccm wakati wa uchaguzi............wamefulia........
CLOUDS HAWANA VIPINDI VYA KUELEIMISHA NA WALA HAWANA UWEZO WA KUELIMISHA....REDIO YAO IFUNGIWE KWANI HAPO BAADAE WANAWEZA KUWA WACHOCHEZI HASA MTU KM KIBONDE...........NOT WANTED IN MEDIA AENDE AKAGANGE NJAA CCM


Clouds FM ikifungiwa itakuwa imeonewa kwani ni miongoni mwa redio bora, na imekuwa ikikemea mambo maovu yanayotokea katika jamii. Tatizo ni kwamba watu wanaosemwa na kuwekwa mambo yao hadharani ndio wanaichukia redio hiyo na wanaijengea zengwe ili ifungiwe.
 
Wafungiwe wasifungiwe nothing will change kila siku clouds clouds we have better things to think off
 
haifai kuwa redio ya kusikiliza bali inatakiwa iwe kijarida cha kitchen part tu................akina kibonde wanaharibu sana redio na mimi niliishaacha kusikiliza tangu niliipoona kuwa wamenunuliwa na mafisadi na ccm wakati wa uchaguzi............wamefulia........
CLOUDS HAWANA VIPINDI VYA KUELEIMISHA NA WALA HAWANA UWEZO WA KUELIMISHA....REDIO YAO IFUNGIWE KWANI HAPO BAADAE WANAWEZA KUWA WACHOCHEZI HASA MTU KM KIBONDE...........NOT WANTED IN MEDIA AENDE AKAGANGE NJAA CCM
Usiusemee moyo............ WENGINE BILA CLOUDS FM SIKU HAIENDI..........

Pamoja na kuipenda kwetu........ mwanahalisi ilishawahi kufungiwa........... Kwa hiyo kwa Clouds FM sitashangaa kwa vile WAPO WANAOFANANA NA WEWE KWENYE MAAMUZI YA AINA HIYO
 
Mmmh

Jamani sio kwamba tunachanganya mambo kutokana na kitendo cha clous kufunga vipindi vyao?

Mi nijuacyo clous kila mwezi 12 huwa wanakuwa na kitu cha kuwatoa hewani, na wanarudi after new year, sijui lakini kama inauhusiano wowote na haka ka te-te-teeeesi
 
Ni ajabu kuona namna baadhi ya Watanzania wasivyoelewa maana ya umuhimu wa vyombo vya habari. CLOUDS FM inaweza kuwa na matatizo yake ( na awali ya yote ni nani asiye na matatizo yake) lakin i kwa sasa ni redio ambayo inaongoza kwa kuwa na 'wateja' (wasikilizaji) wengi, ingawa utafiti wa kina bado haujafanyika.

Baadhi yetu sisi wana-JF tunavyozidi kuichukia na kuanzisha mjadala wa kuijadili ndivyo tunavyozidi kuipa ,chati' redio hii. Hata tv yao nayo ni kiboko. Hii ni redio ambayo siyo ya mafisadi ni ya watanzania wenzatu waliojaa ubunifu na kuthubutu kuanzisha kitu cha maana. Isipokuwa sisi baadhi ya watanzania tulivyo na wivu ndio maana sishangai kuona kuwa baadhi ywetu tumeanza kuichukia clouds ambayo hata ukichukia namna gani haisaidii.
 
Niliwachukia sana tena sana hasa wakati wafanyakazi wanataka kugoma(kejeli zilikuwa nyingi-Kibonde) na wakati wa uchaguzi lakini watu wa sports extra nilikuwa siachi kuwasikiliza hasa IBRAHIM MASOUD MAESTRO NA SHAFII DAUDA,Tangu juzi ni miziki tu huenda wamefungiwa kweli.
 
na kwa sababu wewe sio miongoni mwa great thinkers tunaomba uondoke humu
 
clouds na gazeti la uhuru ni wamoja. wanatoa hoja upepo na za kipumbavu. siyo lazima iwepo. lakini kubwa ni watangazaji wake wanafiki.
 
Guys hawa jamaa ni Entertainment media house, what they do is Entertainment so tuwaache waburudishe, ukionwa unakwazwa waweza badilisha redio station tu ziko nyingi Redio Tumain, Wapo, Praise Power, Redio uhuru, Morning Star, TBC 1 nk

Bahati mbaya kabisa mambo haya huwa hayaendi kirahisi hivyo!
CLOUDS wanajulikana kwa lugha isiyo staha, maneno ya vijembe na kuhubiri chuki, binafsi nilishafuta kabisa hizo frequency nyumbani kwangu, kwani zinachafua mazingira! Sasa kama waTanzania wenyewe wamewasilisha malalamiko TCRA, na TCRA ina miiko yake ambayo kama wakibainika wameivunja, TCRA tutawashangaa kama hawataifunga hiyo station inayoendeshwa na wajingajinga! Yeyote anayeshabikia media yenye content za kihuni kama CLOUDS itaniwia vigumu kumuelewa!
 
Ni ajabu kuona namna baadhi ya Watanzania wasivyoelewa maana ya umuhimu wa vyombo vya habari. CLOUDS FM inaweza kuwa na matatizo yake ( na awali ya yote ni nani asiye na matatizo yake) lakin i kwa sasa ni redio ambayo inaongoza kwa kuwa na 'wateja' (wasikilizaji) wengi, ingawa utafiti wa kina bado haujafanyika.

Baadhi yetu sisi wana-JF tunavyozidi kuichukia na kuanzisha mjadala wa kuijadili ndivyo tunavyozidi kuipa ,chati' redio hii. Hata tv yao nayo ni kiboko. Hii ni redio ambayo siyo ya mafisadi ni ya watanzania wenzatu waliojaa ubunifu na kuthubutu kuanzisha kitu cha maana. Isipokuwa sisi baadhi ya watanzania tulivyo na wivu ndio maana sishangai kuona kuwa baadhi ywetu tumeanza kuichukia clouds ambayo hata ukichukia namna gani haisaidii.

Mambo vp Gadna?
 
Back
Top Bottom