Clouds fm inaniboa kwa wingi wa matangazo

Clouds fm inaniboa kwa wingi wa matangazo

Salaam wanajf,

Jamani natambua umuhimu na jukumu la kutoa habari na burudani hasa kituo bora kabisa cha Clouds, ila tu nadhani jamaa wana matangazo mengi sana yani yakianza ni dk 10 bampa to bampa matangazo. Sijakataa uwepo ma matangazo maana ndo yanayowalipa ila tu nadhani yanapozidi namna hii inaboa.
Nilishaachaga kuwasikiliza, labda michezo saa tatu usiku, ila jamaa wamezidi matangazo, kama huamini fungua hiyo redio sasa hivi kama hujakutana na tangazo, cha kushangaza tangazo likishatangazwa nao wanaanza kulielezea upya kama masaa kadhaa
 
Redio saivi haisikiliziki, yani asilimia karibu 90% ya content ni matangazo tena yanajirudia hadi kinyaa, watangazaji wakiwasha mic kila mmoja anasoma tena tangazo lake wakimaliza wanaongea mazungumzo nonsense tupu afu wanarudia kupiga matangazo na mapambio. Yani hata hao watangazaji nadhani hawajitambui udhalilishaji wanaofanyiwa wao wanasema wingi wa matangazo ndo kipimo cha success kumbe wasikilizaji wanapukutika kila uchao.
Ninyi mnaowasikiliza mna shida kubwa
 
Inakula kwa wenye matangazo watu hawasikilizi matangazo huwa wanahamisha station tu mpaka matangazo yaishe
 
Nilishaachaga kuwasikiliza, labda michezo saa tatu usiku, ila jamaa wamezidi matangazo, kama huamini fungua hiyo redio sasa hivi kama hujakutana na tangazo, cha kushangaza tangazo likishatangazwa nao wanaanza kulielezea upya kama masaa kadhaa
Kweli mkuu umeonae, yani kila bidha ya tangazo wanaielezea ooh nilivyotumia bla bla
 
Back
Top Bottom