Clouds FM acheni Utoto

Ndo matatizo yenu... nifanye declaration ya nini? Muulize Sugu... na microphone yake, na jukwaa lake la kisiasa, pamoja na kutoa album mzima ya kuwatukana Clouds, amefanikiwa kiasi gani katika kuwashusha? For three consecutive years imekuwa the only superbrands radio station in TZ huku ikijitokeza kuwa among the top 20 best in africa... unafikiri hizo dua za kuku huwa zinafaulu??

By the way, mtu amesema mwenyewe kwamba nyimbo zake zisipigwe nyie mnalalamika kwa kigezo eti ni nyimbo ya Mwana-FA. So, what's the difference? Huyo FA mwenyewe na Jide haziendi... what if hata FA mwenyewe hataki sauti ya Jide isikike kwenye nyimbo zake? Yaani mnataka kusema yale matusi ya Jide mmeyasahau au mlikuwa na chuki zenu dhidi ya Clouds since then manake nafahamu hii sio post ya kwanza na wala haitakuwa ya mwisho lakini suaa la nyimbo za wasanii kutopigwa kwenye radio ni suala ambalo lipo kwenye vituo karibu vyote!! Why always Clouds? Acheni kuchanganya siasa na burudani...
 
Acha zako hizo mkuu unafikiri kuna chenye mwanzo kisicho na mwisho?mwisho wake ni pale sisi watazamaji ambao ndio wadau tukaposema basi.
Kila kitu kina mwisho lakini mwisho wa Clouds hauwezi kuwa sababu ya Jide au haters au wasio na hoja za msingi!
 
Kutopiga nyimbo za wasanii ndo "kusambaza upendo"
Sasa wenye nyimbo zao wameshakuambia usipige na usijihusishe kwa lolote kuhusu wao includingi kifo, so we unatarajia bado upige tu kisa unasambaza upendo? Hilo kanisa linaloaminika kusambaza upendo tena wakisukumwa na masuala ya kiroho bado kila siku linapiga watu ban ukiwazingua, itakuja kuwa Clouds???!!
 

Unachanganya mada mkuu,jikite kwenye utoto unaofanywa na clouds hizo beef achana nazo.....wasanii wanajua kama kituo hiki hakipigi kazi zetu basi vituo hivi vinapiga kazi zetu,gazeti hili kama haliandiki kazi zetu basi magazeti haya yataandika kazi zetu,kama wameamua kutopiga wasipige kabisa mambo ya ku-mute na kuskrachi ni utoto.
 
Reactions: Kig
Kwa hiyo tayari mmeshamuendea kwa sangoma kuweka gundu kwenye biashara yake?
Mmmmmmmm! mna mambo nyie, dah! Uchawi Uchawi Uchawi hadi kwa biashara za watu! Na nyie mtakuja kurogwa mgeuzwe vocha halafu watu wawakwangue, wawaingize halafu wawatupe.
 
Reactions: Kig
Kwani JIDE kashafariki? yeye alisema akifa Clouds isipige nyimbo zake, sasa Hajafa!! na hakusema kuwa nyimbo alizoshirikishwa nazo zisipigwe au ziwe muted akiwa hai au akiwa amefariki! huu ni ushamba tu wa Ruge mutaaba na clouds fm,

Kwanza, nilitegemea hiyo media itafute usuluishi na JD!
 
Reactions: Kig
Acha zako hizo mkuu unafikiri kuna chenye mwanzo kisicho na mwisho?mwisho wake ni pale sisi watazamaji ambao ndio wadau tukaposema basi.

Watazamaji gani unaowaongelea? Jisemee wewe husikilizi acha ngonjera za kuwasemea wote. Nenda kawe ukasikilize vichekesho vya mkude.
 

Pamoja na hayo yote mnayojivunia acheni mambo ya kipuuzi kama hayo yaliyoelezwa na mleta mada. Si busara, si hekima kutumia taasisi kama yenu kuendeleza bifu na mtu binafsi. Ugomvi uwe kati yenu uso kwa uso sio kuhusisha wasikilizaji wa radio yenu. Kazi mojawapo ya vyombo vya habari ni kuelimisha na kuburudisha jamii (wasikilizaji). sasa mambo kama hayo yalielezwa hapa yanasaidia nini. Hakuna elimu, hakuna burudani kama baadhi ya sehemu ya wimbo mna mute. Onyeshen professionalism kwenye media zenu. After all unapokosolewa na msikilizaji wa radio yako ujue kuna tatizo. Ni vema ukalifanyia kazi lile unalokosolewa badala ya kuja na picha za vyeti vya tuzo, au ushahidi kuwa radio ipo top 20 africa, au story za kuwa radio inawasikilizaji milion ngapi. Heri kuongeza wasilikilizaji kuliko kupoteza msikilizaji hata kama ni mmoja.
 
Wakae kuyazungumza ili iweje? Yote kukufurahisha wewe? Hahaha wabongo hamuishi vituko. Jide keshakula yamini kuwa hata akifa wasikanyage, na wakionekana msibani kwake wapigwe mawe sasa unaanzia wapi kujikomba kwa mtu wa namna hiyo? Acha utoto wewe.

eti wabango haya mmarekani mweusi umesahau kutupiamo na kiingilishi cha ki usa sasa nalud ktk mada hata kagame wanapojaribu kutafuta suluhisho la kule kivu congo drc la kikundi chake cha m23 huwa anachukia anatetea maslah nahis hata wewe utakuwa unamaslah na huo ugomvi kwa nn hupend wapatane? kwangu mm ntafurah sna kama wakiyamaliza huwa sipendi bifu natambua dunia sio yetu ni njia tu kama wewe hupend watu waish kwa amani na upendo wengine hatuko hivyo.
 
Hapo hakuna cha utoto wala nini sema mnakuza mambo! Wao walikuwa wanafanya album review ya Mwana-FA unfortunately moja ya wimbo ambao ulipigwa ni huo wa Alikufa Kwa Ngoma ambao Jide ameingiza sauti yake! Sasa huwezi kusema wimbo mzima usipigwe kwa sababu ya chorus aliyoingiza Jay Dee ambayo kila chorus haifiki hata sekunde 30... yaani uache wimbo wote kisa itaonekana unafanyika utoto!? Come on dude, hata wewe mwenyewe am certain huwa unasikiliza wimbo na ukifika sehemu ianyozingua, una-forward au una-mute! That's one, aidha, kwamba ku-scratch ni utoto kwa sababu tu sehemu iliyokuwa scratched inamuhusu Jide ni hoja isiyo na maana yoyote coz' mara kibao tu, nyimbo mbali mbali, huwa scratched or muted kwa sababu mbalimbali kama vile labda kipande husika kina lugha isiyofaa kwa jamii n.k! So, for Clouds, moja ya sababu ndo hiyo... mtu asiyetaka kazi zake zisikike, unapiga ukucha tu... huwezi kuacha wimbo mzima kwa ajili ya mtu mmoja!! Hapa hatutaki mambo ya nyama ya kitimoto haramau lakini mchuzi wake sawa tu!!!
 
Wakae kuyazungumza ili iweje? Yote kukufurahisha wewe? Hahaha wabongo hamuishi vituko. Jide keshakula yamini kuwa hata akifa wasikanyage, na wakionekana msibani kwake wapigwe mawe sasa unaanzia wapi kujikomba kwa mtu wa namna hiyo? Acha utoto wewe.

kwanza jina tu linasadifu kilichopo akilini mwako sasa sijui nani mtoto anaeshabikia ugonvi mi nahis ww utoto umekujaa sio bure ukiulizwa eti alisema kwani wangapi waliongea na wakalekebishwa yakaisha hakuna mkamilifu kila mmoja angekuwa anakomalia kauli za mwenzie tungeisha hapa duniani hata ww kuna watu umewakwaza lakini wanakuchulia po tu.
 
Unawaonea bure jama, huwezi kumzuia mtoto ili aache utoto, kwani pale kuna mtu mzima? It's a Radio Station full of big fat babies!!!!


After-all hujalazimishwa kuisikiliza. There are hundreds of radio stations out there, far more better than the "Big babies' station"




Sent from my iPhone using JamiiForums app
 
Reactions: Kig

kuanzia pale, umeona redio ilivyoyumba? hando alibaki, lkn mimi nilimuona mjinga sana
 
Hivi wewe na wenzako mlifuatilia lile bifu au mnaongea tu? NI mara ngapi Ruge alinukuliwa akimuomba Jide wakutane nae ili wayamalize? Jide alijibu nini? Sio huyo huyo Jide ndie alijibu hana muda wa kukutana nao na hapo akatangaza kwamba Clouds wasipige nyimbo zake na hata akifa habari za kifo chake wasitangaze na Kusaga pamoja na Ruge wasikanyage kwenye msiba wake wake??!! Sasa pamoja na yote hayo, bado mnawalaumu Clouds, kwa lipi? Au kwavile hiyo nyimbo siyo ya Jide kwahiyo wangepiga tu? Hivi mtu aliyefikia hadi kutangaza kwamba siku akifa Kusaga na Ruge wakithubutu kukanyaga msiba wake, ataona taabu gani kutaka wale alioshirikiana nyimbo zao wafute sehemu alizoimba yeye kwa sababu tu Clouds waliiavchia hewani sehemu husika?
 

Wakikaa na hilo gumegume kusululishana nitawadharau sana. Yaani kampuni ikamnyenyekee mwanamke aliyewapiga marufuku kutangaza kazi zake? Labda yeye ndo akawaombe msamaha kwa jinsi alivyowadhalilisha kwenye mitandao. Yaani wakosewe wao na msamaha waombe wao??? Hivi una kichaa? Nitawadharau sana endapo wakinyafa upuuzi kama huo ili kukufurahisha wewe.
 
kuanzia pale, umeona redio ilivyoyumba? hando alibaki, lkn mimi nilimuona mjinga sana
Umetumia vigezo gani kusema kwamba radio imeyumba? EFM waliingia na mwara wa kuchukua cream presenters kwenye kila idara... imechukua wangapi ambao ni cream kutoka Clouds? Sasa huyo Hando unayemuona mjinga, unamlinganisha na nani aliyetoka kwa kuona Clouds inayumba?

Hebu weka indicators zako hapa kuonesha kwamba Clouds imeyumba manake wengine tunafahamu kwamba, baada ya hapo ndio kwanza wakafungua station Abu Dhab na hivyo kuwa the first media house in East Africa kufanya hivyo! Hivi una habari kuna kitu kinaitwa Clouds International? Huko kuyumba unakosema wewe ni kupi? Manake moja ya mambo yanayokera Clouds ni matangazo... linatoka hili, linakuja lile halafu unasema Radio inayumba? You can't be serious!!!
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…