Cleopa D. Msuya: Nimemkubali

Kwa jinsi nilivyomsikiliza jana, anafaa kabisa kurudia nafasi ya uwaziri mkuu, lau kama ingekuwa i nawezekana!
Wakuu, nilimsikia mtangazaji akimtaja pia kwa cheo cha Makamu wa Rais...je alikamata nafasi hiyo kwa muda gani?
Mimi personally nimefanya nae kazi ni mchapa kazi mzuri saaaaaaaana.

Napenda kutoa ANGALIZO yeye alikuwa Waziri mkuu na makamo wa Pili wa Rais kwani makamo wa kwanza wa rais alikuwa ni Rais wa Zanzibar.

Tatizo lake kubwa Msuya na ambalo kwa wakti ule lilikuwa ni MKABILA sana. Kwake yeye namnani, chedi ni kitu cha kwanza.

Nawaasa WaTZ especially waTanganyika muwe makini na watu hao kwani atawazamisha sana.

Mimi nilikuwa wizara ya mipango yeye akiwa PM alilazimisha kila kizuri kipelekwe upareni.

Msalimieni sana mzee wangu huyu. Alizoea kuniita Mwarabu na nilimpokea mtoto wake wakti nikiwa Japan
 
Mnyonge mnyongeni lakini hakh ake mpeni.

hakuna mtu mahiri na mwenye uwezo mkubwa miongoni mwa mawaziri wakuu wooote huko Tanzania zaidi ya ahali yangu SALIM Ahmed SALIM.
Hata JK Nyerere alilijua hilo

Mkuu huyo si tayari ameshatajwa huko juu. Au unamrudia rudia kwa kuwa ni mwarabu mwenzio.
 
CD Msuya didn't abide by rule of the game when he was a player, he's now 'seeing' others not abiding by the rule of the same game while playing.
Badala ya kukaa dak 45 ITV angepeleka ushauri wake huo kwenye vikao vya chama chake tawala. Anajua hatosikilizwa!
Hivyo tuliyosikia jana kayasema ili tumwone yy si kati ya waharibifu. Kwani ni lini Tanzania tuliwahi ku export kingi kuliko tunach import?
Who knows how rich is Msuya anyway? Mwenye kujua naomba anijuze.
Its unfair ndugu yangu.
Sisi tulioishi long enough wakati ule gari rasmi za serikali zilikuwa Renault Roho,Peugoet 404 na baadaye 504.
Hapakuwa na makuu.
Chenji serikalini ilikuwepo, tena kwa sana kwa hela ya kigeni.Shilingi yetu ilikuwa very strong and at par na Shilingi ya kenya na Uganda.
Kwa wale wanao kumbuka Paundi moja ya kiingereza ilikuwa sawasawa na Shilingi ishirini(leo Tshs 2500-2600)
Mishahara ilikuwa inalipwa kwa hela ya kodi zetu na fedha nyingi tu kubaki na kuwekwa akiba(Reserves).
Generally viongozi wengi katika awamu ya Mwalimu walikuwa waaminifu sana,of course kama kuna exceptions basi ziweke jamvini ukweli na uongo udhihirike.
 
niliiona kwa vipande lkn mzee anaonekana yuko vizuri sana na hazina ya ufahamu na hekima kama akina JK wakipenda kumtumia! Natamani pia ningeona mahojiano kama hayo yakifanywa na mawaziri wakuu wastaafu John Samwel Malecela na Edo Lowassa,lakini kwa kifupi Mzee CD Msuya yuko vizuri sana.

Mkuuu kumbe nawe ulimuona jana mzee aliongea mambo mengi sana yalinikumbusha ile Mwl.Nyerere 1995 Mei Mosi Kule mbeya na huyu mzee nae kayarudia baadhi ya mambo mwali aliseme eg Viongozi wetu wana penda sana kusingizia Wolrd Bank na IMF huku wakishindwa kutafuta mbinu za ukusanyaji wa mapato i mean kodi viwanda ndio hakuna na ndio hayo mwalimu pia aliyasema Mei Mosi 95 na Basili mramba alikuwepo kwa ile Mei Mosi ila vichwa vya hawa viongozi tulio nao ni Corrupted kabisa hawataki kusikia wala kukubali ukweli mpaka Mzee Msuya jana akasema Management ya Serikali yetu inamatatizo which meana kwangu ni rusha na Political Interest ndio zawatawala viongozi wengi esp Nchini mwetu mbali na nchi zingine za kiafrika hapa kwet tume kubuhuu na kweli twa tayarisha kitu kina itwa TIME BOOM likilipuka humu hatuta onana kabisa viongozi ndio watakao hatarisha AMANI ya nchi hii coz ya uchu wa madaraka
 
Tatizo ni kwamba tofauti na ilivyo kuwa kwa Nyerere hawa viongozi wetu wastaafu wengi wana ushawishi kidogo mno kama wanao kabisa. Sidhani hata kama wanafuatwa kwa ushauri na kama wanafuatwa kutoa ushauri sina ushahidi wa ushauri wao kufanyiwa kazi. Wazee wetu hawa wamekua vyombo vya public relations kwa kualikwa tu kwenye hafla mbali mbali.

Mimi ninge washauri hawa wazee pamoja na kujitokeza kwa mahojiano kama hivi waandike vitabu vingi kuhusu maisha yao na utumishi wao.
tatizo kubwa sidhani kama ni hao viongozi wastaafu perse. Nadhani wamechoka kudharauliwa na viongozi waliopo madarakani. kama ulivyoonyesha, viongozi wetu wa sasa wamekuwa wajuaji kiasi kwamba hawapati shida kuomba ushauri kutoka kwa vichwa hivi vilivyotangulia, hii ni mbaya sana hasa ukizingatia kuwa nchi inakabiliwa na matatizo mengi sana na kuna watu wenye uzoefu wa kutosha wa jinsi ya kukabiliana na matatizo hayo.
Wakati mwingine, baadhi yao wanafikia hatua ya kuchoka na kuamua kutoa ushauri publicly, lajkini tumekuwa tukishuhudia jinsi wanavyoshuhsuliwa hadharani pia.
wazo la wao kuandika vitabu ni zuri kwa sababu itawapatia fursa ya kutoa maoni yao kwa uopana wake, lakini tatizo ni kwua watanzania wengi hawana (au hatuna) tabia ya kusoma - hasa vitabu. naohifia kuwa ushauri wao utaishia hewani hata ukiwekwa kwenye vitabu ingawa ni wazo zuri sana
 
Msuya kiongozi mzuri na wengine wote. Sioni kwa nini anaingizwa Kikwete humu; kwanza Msuya hata afanye nini hamfikii Kikwete, kwa sababu kikwete Ni RAIS, na akimaliza anakuwa RAIS MSTAAFU.

Kumkashifu kikwete ni kuwakashifu waliompigia kura.

Tusiende huko kwa sasa. tubaki na CD MSUYA, Amekubaliwa.

Mie pia nimemkubali; kapeleka umeme mwanga, Bunda kuna nini?
Ndugu yetui, matatizo mengi ndo yaanzia hapo - URAIS.
Hivi ni nani kakwambia kwua kwa kuwa Kikwete ni rais basi ana akili kuliko watanzania wote? Au, nini kinamfanya Kikwete awe anaimiliki nchi hii kama kitu binafsi eti kwa sababu tu ni rais? Kumbuka kuwa cheo ni dhamana na Urais wa Kikwete ni kazi kama zilivyo kazi nyingine na mbaya zaidi waajiri wake ni sisi watanzania. Imekuwa ni ajali tu kuwa katiba inampa madaraka lakini inavyotakiwa rais hapaswi kuwa na mamlaka zaidi ya mamlakam waliyonayo wananchi dhidi yake.
Kuona kuwa Msuya hamfikii Kikqwete kwa sababu Kikwete atakuwa rais mstaafu, ni ufinyu wa mawazo wa nini kichanoongelewa hapa
 
ni vizuri tumuweka mtu ktk mizani kutokana na uzalendo wake wa vitendo kwa nchi na wananchi kwa ujumla,sio eti kwa sababu leo hii mtu anaweza kujieleza vzr ,kama suala la kuongea vzr mbona majuzi hapa tumeona lowasa alivyokuwa bungeni alishangiliwa mpaka kwa kupiga meza na hata baadhi yetu humu tulidiriki kusema anatufaa 2015,naona kuna wanaosema kama ingewekana mzee msuya angepata cheo cha uwaziri mkuu tena ingekuwa swaafi,kwa nini tumpime kwa anayoyasema leo na siyo yale aliyoyatenda wakati akiwa madarakani
 
Niliona mahojiano, mzee alijibu vizuri na kwa umakini sana. Madai haya mengine eti alipeleka umeme Mwanga,kwani siyo Tanzania? Ama hawakustahili kupata umeme? Tuache hizo watanzania wenzangu!
 
niliiona kwa vipande lkn mzee anaonekana yuko vizuri sana na hazina ya ufahamu na hekima kama akina JK wakipenda kumtumia! Natamani pia ningeona mahojiano kama hayo yakifanywa na mawaziri wakuu wastaafu John Samwel Malecela na Edo Lowassa,lakini kwa kifupi Mzee CD Msuya yuko vizuri sana.

Tatizo la viongozi wetu ni kuzidisha siasa na kudharau wataalamu ndio maana mambo hayaendi. Kilimo kwanza hakina maana kama hakiwalengi watu wa kawaida ambao ndio wengi. Mbilioni ya miradi ya umwagiliaji yanishia kwenye semina za viongozi badala ya kuweka infrustructure laaana kabisa!
 
Niliona mahojiano, mzee alijibu vizuri na kwa umakini sana. Madai haya mengine eti alipeleka umeme Mwanga,kwani siyo Tanzania? Ama hawakustahili kupata umeme? Tuache hizo watanzania wenzangu!
Mwalimu aliyekuwa Rais kwa zaidi ya miaka 20 nchi hii aliiacha wilaya yake ya Musoma(V) haina maji, barabara ya lami wala umeme.
 
Hivi siyo yeye alishirikiana na mpare mwenzake wakatoa tenda mbovu kule mtera mpaka lile bwawa likatengenezwa bila kutolewa tope hadi sasa tunalia kina cha maji oh sijui nini.... Huyu jamaa ni very selfish na hamumjui tu....
 
kwa hiyo kwa mtazamo wako umeme ni kwa ajili ya wanaoishi kwenye maeneo tambarare tuu eeh? wa milimani hawastahili si ndio!!!

Chimbuko la ufisadi ni ubinafsi uliokithiri, na katika historia ya nchi hii mtu aliyeshika madaraka ya juu kabisa na kuonesha ubinafsi wa wazi ndio huyu mnayemuona leo ni shujaa. Suala sio kupeleka umeme milimani, suala ni kuonyesha upendeleo wa wazi kwa watu wa huko upareni. Ubinafsi ulianza kwa kupendelea jimbo na baadaye umezaa ufisadi wa kupendelea familia. Hawa mafisadi tunaowajadili kila kukicha wanachofanya ni kuchukua mali ya umma na kuitumbua na familia zao. Yeye kama waziri mkuu alichofanya kikubwa cha maana ni kuelekeza nguvu kubwa kupeleka umeme jimboni kwake huko milimani, na baada ya kusemwa sana ndio akaibuka na hiyo kauli ya kila mtu atabeba msalaba wake.
 
Tatizo watanzania ni wepesi sana wa kusahau. Huyu jamaa alivyokuwa kiongozi alipeleka umeme huko milimani kwao ambako kwa hali ya kawaida hakufikiki kabisa kwa gharama kubwa za serikali!!!!!!!!!!!!????????????

Kwani huko milimani kwao si kuna watanzania wanaishi pia au wao hawastahili kupelekewa umeme, inamaana ulitaka hizo gharama kubwa za serikali zitumike kwenye mashangingi(V8) na posho za wabunge wa viti maalum au sio!!!


Kama wewe ni mpare unakila sababu ya kumsifia huyu jamaa, maana wapare walimchagua kuwa mbunge wa maisha wa jimbo la mwanga mpaka alivyoamua kustaafu mwenyewe. Vinginevyo kwa makabila mengine na kwa taifa kwa ujumla, jamaa hana la maana lolote zaidi ya ubinafsi na ukabila uliokithiri enzi za uongozi wake. Kile kirusi cha ubinafsi alichokuwa nacho na upendeleo wa wazi kwa watu wa kabila lake ndio kimezaa sasa na kuleta ufisadi uliokithiri ndani ya nchi hii.
 
Alikuwa anaogopaogopa kukosoa moja kwa moja, sijajua kwanini!
Wanajifanya wanabusara hadi mambo yanaharibika 1kwa1!
Mtangazaji nae alikuwa mbwiga tu anashindwa kumuuliza maswali vizuri, sijui kasoma wapi yule!? Ya msingi ya kuuliza yalikuwamengi sio kumwacha msuya akieleze kirahisi vile!

Hivi Tanzania hatuna wanahabari mahiri kama kina Tim Sebastian wa Hardtalk ya BBC?
 
Kama wewe ni mpare unakila sababu ya kumsifia huyu jamaa, maana wapare walimchagua kuwa mbunge wa maisha wa jimbo la mwanga mpaka alivyoamua kustaafu mwenyewe. Vinginevyo kwa makabila mengine na kwa taifa kwa ujumla, jamaa hana la maana lolote zaidi ya ubinafsi na ukabila uliokithiri enzi za uongozi wake. Kile kirusi cha ubinafsi alichokuwa nacho na upendeleo wa wazi kwa watu wa kabila lake ndio kimezaa sasa na kuleta ufisadi uliokithiri ndani ya nchi hii.

Bwana ndugu, mimi sidhani kama ulifanya kazi chini ya CD Msuya kudraw hii conclusion ambayo naona ni mawazo binafsi.
Na je mtu akipeleka umeme kwao kuna dhambi gani, alimradi kulikuwa hakuna umeme-huko hakuna waTanzania wanaotaka umeme kama wananchi wa sehemu nyingine kama Kisarawe ,Kishapu au Kiteto?
Tuache kutetea sera za kimaskini.
Mtu kwao.
Nasema hivi kwa vile mimi si Mpare lakini sioni kosa la kupeleka umeme unaozalishwa Nyumba ya Mungu na unapita juu kwa juu barabarani.
 
Ili eneo lipate umeme kigezo mojawapo ni wakazi wa hapo kuwa na nyumba bora. Sasa ww unaelalamika,huko kijijini kwenu kukoje? Kama siyo wengi wetu tukisha fika mjini,hatutaki kurudi vijijini. Watu wa Mwanga wameweza! Tusiwaonee wivu.
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom