Cleopa D. Msuya: Nimemkubali

Cleopa D. Msuya: Nimemkubali

Kwa jinsi nilivyomsikiliza jana, anafaa kabisa kurudia nafasi ya uwaziri mkuu, lau kama ingekuwa i nawezekana!
Wakuu, nilimsikia mtangazaji akimtaja pia kwa cheo cha Makamu wa Rais...je alikamata nafasi hiyo kwa muda gani?

No PJ, hafai hata kidogo. Kujibu maswali siyo tija. Tija ni uzalendo na kufanya mambo yanayookoa maisha ya watanzania hasa wakati huu mgumu tulio nao. Hawa wazee wetu mnaowapa sifa kuwa wanajua kujibu maswali wanafanya nini mda wote huo mpaka nchi ididimie kiuchumi hivi. Wameshindwa hata kupaza sauti pale mambo yanapoenda mrama. Msuya ni muoga kama pinda. Angalia jana wakati anajieleza alishindwa kusema ukweli kuwa serikali imeshindwa akabaki kujingatangata. Musya, Malecela, Sumaye & Lowasa ni mizigo ya moto.Bora hata Warioba na SAS kidogo wanaichallenge serikali mambo yanapoenda mrama.
 
Kwa jinsi nilivyomsikiliza jana, anafaa kabisa kurudia nafasi ya uwaziri mkuu, lau kama ingekuwa i nawezekana!
Wakuu, nilimsikia mtangazaji akimtaja pia kwa cheo cha Makamu wa Rais...je alikamata nafasi hiyo kwa muda gani?
Cheo cha Makamu wa Rais kilikuwepo kwa muda mrefu sana wakati wa Awamu ya Kwanza.
Mwishoni mwa utawala wa Mwalimu ndio cheo cha Uwaziri Mkuu kikarudishwa tena baada ya kufutwa wakti tu tumepata uhuru.
 
Tusiingize mambo ya fitna ya kuwachonganisha watu bali tujadili mada -Mzee CDM- unamkubali? Mimi huyu mzee namkubali sana na nimekuwa na msimamo huu tangu awali wakati akiwa waziri mkuu. Hata zile fitna za kupindisha maana na lengo la kauli yake ya kila mtu kubeba mzigo wake haziwezi kufuta ukweli kuwa huyu mzee ni material tangu wakati huo hadi hii leo.
 
Wazee hawa wanaonekana ktokubaliana na mambo mengi yanavyoendeshwa ndani ya CCM na serikali wanayoita ni yao. Hakuna jitihada za wazi au hata za kificho wanazofanya kuibadili hali hii kwa manufaa ya NCHI yetu na WATANZANIA. Ukiwaambia watoke CCM wajiunge na upinzani ndio hawakuelewi kabisaa! Wanabaki tu kulialia kwenye vimahojiano kama hivi basi. Nadhani wana makandokando mengi yanayowazuia kuwa jasiri.
 
Katika kipindi cha 45 minutes cha ITV leo jioni , mtoa mada alikuwa CD Msuya, Waziri Mkuu na Makamu wa Kwanza wa Rais, enzi ya Mwalimu.
Kwa hakika amenikosha sana.
Bado ana data na current za kiuchumi-inaelekea nafuatilia sana current events
Hana papara wala jazba kujibu maswali, na alikuwa composed.
Lakini zaidi ya yote ameiasa nchi mambo makuu yafuatayp
  • kuwawezesha wakulima kutukia mbegu bora, utaalam bora wakilimo, na mechanization
  • ameishauri serikali kupunguza matumizi(kuachana na mashangingi)
  • kuongeza uzalishaji mali-katika kilimo n.k. ili kuongeza pato la taifa nahatimaye kupunguza kuporiomoka kwa shilingi yetu
Kwa jinsi alivyokuwa akijieleza kwa ufasaha, tofauti kubwa imeonekana , ukilinganisha na "Mawaziri vijana" wetu waliopo sasa.
Walioona tupeni maoni, good or bad.

Mkuu nami nilikuwa nawaza kuweka hii taarifa, Nimemkubali, mzee ana busara zake na enzi hizo walikuwa hawabahatishi. Naona hata sasa ana uwezo wa kuongoza nchi. Kwa yale aliyo yaongea, yangeweza kuwasaidia majambazi wanao ongoza kwa sasa na kuinua taifa. BIG-UP Mzee Msuya.
 
Kwa jinsi nilivyomsikiliza jana, anafaa kabisa kurudia nafasi ya uwaziri mkuu, lau kama ingekuwa i nawezekana!
Wakuu, nilimsikia mtangazaji akimtaja pia kwa cheo cha Makamu wa Rais...je alikamata nafasi hiyo kwa muda gani?
Tulipokuwa na Rais Mzanzibar Ali Hassan Mwinyi, Makamu wake toka bara ukianzia na JS Warioba, JS Malecela na akamalizia na CD Msuya wali-combine UMAKAMU na UWAZIRI MKUU. Na wote walipata nafasi hizo kwa UKRISTO wao kwanza!
 
Hapa nafikiri mtoa mada alikuwa anataka tujadili hoja, Hoja iliyowekwa bayana na C.D.M,Na si mapungufu ya Mtu, hayo kila mtu anayo, Hoja hapa ni namna ya kuinua uchumi wa nchi kwa sasa, Mazingira ya kazi ya wakati wa CDM ni tofauti sana na sasa, Mfumo wa uchumi umebadilika nchini, Fursa zimeongezeka na bado uchumi umedorora.Suala la kubana matumizi JK na serikali haitaki kusikia, ulipwaji wa posho umepewa kipaumbele kuliko uboreshaji wa Huduma za jamii zikiwemo shule na Zahanati, Na Mahospitali.
Katika karne hii ya sasa wakati nchi kama Rwanda mwanafunzi wa shule ya msingi anatumia Laptop,Tanzania wanafunzi wanakaa chini bila Vitabu wala Walimu, halafu tunataka kuingia katika ushindani wa Afrika mashariki? Na Viongozi wetu hawa tulionao tena wana spidi kweli ya uundaji wa shirikisho! Nawauliza watanzania wenzangu je TUKO TAYARI?
 
Kwa jinsi nilivyomsikiliza jana, anafaa kabisa kurudia nafasi ya uwaziri mkuu, lau kama ingekuwa i nawezekana!
Wakuu, nilimsikia mtangazaji akimtaja pia kwa cheo cha Makamu wa Rais...je alikamata nafasi hiyo kwa muda gani?

Mkuu PJ.

Enzi za Mwl hadi Mzee ruksa wadhifa wa Makamu wawili wa Rais ulikuwepo.Rais akitoka upande wa Tanzania bara Makamu wa kwanza alikuwa Rais wa Zanzibar,Makamu wa pili wa Rais alikuwa Waziri mkuu.Rais wa JMT akitokea Zanzibar makamu wa kwanza wa Rais alikuwa ni Waziri mkuu na Makamu wa pili wa Rais alikuwa Rais wa Zanzibar.Mkuu hili jambo wazanzibar hadileo wanalilalamikia sana ,wanadhani Rais wa Zanzibar kuondolewa wadhifa wa makamu wa Rais kadharauliwa sana.

 
Hata kama aliharibu wakati wa uongozi wake lakini bado ananafasi ya kuwa mshauri mzuri wa viongozi wetu wa sasa kama akitumiwa vizuri.
 
Inawezekana ameongea vizuri ila binafsi sijaona hayo mahojiano ila kiukweli huyu jamaa ukiangalia kwa umakini yeye ni kati ya vyanzo vikuu vya mmomonyoko wa maadili ya kiuongozi na ufisadi. Tatizo watanzania ni wepesi sana wa kusahau. Huyu jamaa alivyokuwa kiongozi alipeleka umeme huko milimani kwao ambako kwa hali ya kawaida hakufikiki kabisa kwa gharama kubwa za serikali, huu ulikuwa ubinafsi mkubwa na chimbuko la ufisadi tunaouona sasa.

Sielewi kwanini mnamsifia kwa anayoyaongea badala ya kuweka data alivyokuwa na cheo kikubwa kabisa serikalini alifanya nini ? Hata huyu JK mnamponda leo baada ya miaka 10 mtasifia kweli na kumuona ni kiongozi mwenye busara na jasiri. Watanzania tusiwe wepesi wa kusahau.

kwa hiyo kwa mtazamo wako umeme ni kwa ajili ya wanaoishi kwenye maeneo tambarare tuu eeh? wa milimani hawastahili si ndio!!!
 
Kuongea kaongea vizuri, lakini mi naona ndo wale wale tu. Kwani hata Sumaye pamoja na ufisadi wote aliokuwa akituhumiwa kipindi cha uongozi wake lakini ukimsikiliza anvyoongea leo unaweza ukasema huyu ndo aina ya viongozi tunaowataka, lakini wakati yupo madarakani hakuyafanya hayo anayoyasema sasa na badala yake alikuwa Mchumiatumbo.

Usikute huyu CD Msuya ndo ameanza na "Ntoke vipi". Huwezi jua 2015 bado kitambo kidogo na nafasi kama bado iko "Open" vile. Tusubiri tu!
 
Good about Msuya was not a Party Politician; he was a stateman a country politician who wanted the better for his Nation and not talk with no ideas as Party Politicians do.

Yeah he did have his short-cummings such as hating Moringe Sokoine and was not that much Socialist but he did work hard...
Yeah he still has some appealing Data's on how our Economy is doing our current leaders should go to him and get some brains from him...
 
Alikuwa anaogopaogopa kukosoa moja kwa moja, sijajua kwanini!
Wanajifanya wanabusara hadi mambo yanaharibika 1kwa1!
Mtangazaji nae alikuwa mbwiga tu anashindwa kumuuliza maswali vizuri, sijui kasoma wapi yule!? Ya msingi ya kuuliza yalikuwamengi sio kumwacha msuya akieleze kirahisi vile!

Yule dogo mara nyingi yeye ndo huwa ANAONGOZWA na wale anaowahoji badala ya yeye kuwaongoza. Nimesikiliza vipindi vyake vingi sana tangu Wassira, Lukuvi, Nahodha..........hadi hiyo jana kwa Msuya; dogo ana mapungufu yafuatayo:

1. Anaongozwa na hao anaowahoji
2. Anawaogopa anaowahoji kwa vyeo vyao hivyo huwa hawaulizi maswali chokonozi
3. Huwa anapenda kuwauliza "light and general questions" ambayo majibu yake tumeyazoea; mfano tumejenga barabara, mahospitali, shule za kata, mgao wa umeme utakuwa historia, n.k.
4. Wakati mwingine huwa inaonekana bayana kuwa yale maswali yote alishawapatia kabla hivyo hata kabla hajafikia swali husika utakuta waziri anatoa majibu ambayo unaona wazi kuwa ameyakariri kabla hajaingia studio.

Kwa mawazo yangu yule dogo hafai kwa kile kipindi aidha awekwe mtu ambaye ata-fit ama kipindi kibadilishwe jina.
 

Mkuu PJ.

Enzi za Mwl hadi Mzee ruksa wadhifa wa Makamu wawili wa Rais ulikuwepo.Rais akitoka upande wa Tanzania bara Makamu wa kwanza alikuwa Rais wa Zanzibar,Makamu wa pili wa Rais alikuwa Waziri mkuu.Rais wa JMT akitokea Zanzibar makamu wa kwanza wa Rais alikuwa ni Waziri mkuu na Makamu wa pili wa Rais alikuwa Rais wa Zanzibar.Mkuu hili jambo wazanzibar hadileo wanalilalamikia sana ,wanadhani Rais wa Zanzibar kuondolewa wadhifa wa makamu wa Rais kadharauliwa sana.

Wazanzibar wanaitaka NCHI yao. Haya mengine ni visingizio vya hapa na pale. Tuwape Nchi yao. Itatusaidia sana. Bunge letu la Muungano litapungua kwa zaidi ya Wabunge 60.
 
Yule dogo mara nyingi yeye ndo huwa ANAONGOZWA na wale anaowahoji badala ya yeye kuwaongoza. Nimesikiliza vipindi vyake vingi sana tangu Wassira, Lukuvi, Nahodha..........hadi hiyo jana kwa Msuya; dogo ana mapungufu yafuatayo:

1. Anaongozwa na hao anaowahoji
2. Anawaogopa anaowahoji kwa vyeo vyao hivyo huwa hawaulizi maswali chokonozi
3. Huwa anapenda kuwauliza "light and general questions" ambayo majibu yake tumeyazoea; mfano tumejenga barabara, mahospitali, shule za kata, mgao wa umeme utakuwa historia, n.k.
4. Wakati mwingine huwa inaonekana bayana kuwa yale maswali yote alishawapatia kabla hivyo hata kabla hajafikia swali husika utakuta waziri anatoa majibu ambayo unaona wazi kuwa ameyakariri kabla hajaingia studio.

Kwa mawazo yangu yule dogo hafai kwa kile kipindi aidha awekwe mtu ambaye ata-fit ama kipindi kibadilishwe jina.
Ni kweli. Kipindi kile wangepata mtu kama Jenerali, Kibanda, Ngurumo, Mbwambo, Mwanakijiji au hata Kubenea. Hawa wako huru na wanaijua nchi hii.
 
HAYA MAMBO NI YA KUANGALIA NA KUYAFANYIA KAZI ZAIDI YA KUZUNGUMZA
AMEZUNGUMZIA
kuwawezesha wakulima kutukia mbegu bora, utaalam bora wakilimo, na mechanization
ameishauri serikali kupunguza matumizi(kuachana na mashangingi)
kuongeza uzalishaji mali-katika kilimo n.k. ili kuongeza pato la taifa nahatimaye kupunguza kuporiomoka kwa shilingi yetu
NI NAMNA GANI HAYA YATAFANYIKA JE NI KUNUNUA POWER TILLER ZA KICHINA NA KUZIUZA KWA FEDHA NYINGI
AU NI KUHAKIKISHA ZINAWAFIKIA WANANCHI KWA BEI NAFUU
 
CD Msuya didn't abide by rule of the game when he was a player, he's now 'seeing' others not abiding by the rule of the same game while playing.
Badala ya kukaa dak 45 ITV angepeleka ushauri wake huo kwenye vikao vya chama chake tawala. Anajua hatosikilizwa!
Hivyo tuliyosikia jana kayasema ili tumwone yy si kati ya waharibifu. Kwani ni lini Tanzania tuliwahi ku export kingi kuliko tunach import?
Who knows how rich is Msuya anyway? Mwenye kujua naomba anijuze.
 
Tusiingize mambo ya fitna ya kuwachonganisha watu bali tujadili mada -Mzee CDM- unamkubali? Mimi huyu mzee namkubali sana na nimekuwa na msimamo huu tangu awali wakati akiwa waziri mkuu. Hata zile fitna za kupindisha maana na lengo la  kauli yake ya kila mtu kubeba mzigo wake haziwezi kufuta ukweli kuwa huyu mzee ni material tangu wakati huo hadi hii leo.
 
Tatizo watanzania ni wepesi sana wa kusahau. Huyu jamaa alivyokuwa kiongozi alipeleka umeme huko milimani kwao ambako kwa hali ya kawaida hakufikiki kabisa kwa gharama kubwa za serikali!!!!!!!!!!!!????????????

Kwani huko milimani kwao si kuna watanzania wanaishi pia au wao hawastahili kupelekewa umeme, inamaana ulitaka hizo gharama kubwa za serikali zitumike kwenye mashangingi(V8) na posho za wabunge wa viti maalum au sio!!!
 
Basi kwetu Mbagala, vile kipindi kinaanza tu, UMEME NAO HUOOOOOOOOOOOOO...kilipoisha tu mida ya nne na kitu hivi nao ukarudi, Asanteni TANESCO!
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom