Ngoja niweke story ndefu kidogo; wakati Sumaye anaondoka ccm kujinga na upinzani pale Silver sand hotel, alizungumza mengi but kuna 1 nililipenda sana. Alisema anataka kuja upinzani ili kutofautisha shughuli za ccm na za serikali, akatolea mfano wa OCD wa police jinsi gani hua anajikuta analazimika kufanya kazi za ccm badala ya serikali.
Wakati wa kampeni za urasi wa Marekani mwaka2008, Obama alinadi sana habari ya kulifunga gereza la Gwantanamo pamoja na kuondoa majeshi yake kule Iraq na Afganistan; Makain yeye alikua anasisitiza kuamini katika mkono wa chuma dhidi ya Iraq na sehemu zingine za dunia; CIA kama chombo cha serikali walikua wanawasikiliza wagombea wote hao 2 na walikua wanajua mmoja wao atakuja kua rais wa Marekani na itawalazimu kufanya nae kazi wapende au wasipende. Nakumbuka mara baada ya Obama kushinda KURA za Wamarekani, CID walimwita na kukaa nae zaidi ya saa 8 (hi ilikua kabla haja apishwa) nini waliongea hadi leo ni siri yao, ingawa inasemekana walimwambia madhara ya kulifunga gereza la Gwantanamo mapema kama alivyo ahidi kwenye kampeni, habari zinaendelea zaidi kua wao kama CIA walimwambia kua Osama bin Laden atapatikana through Gwantanamo (nimeiangalia ile scrip iliotengenezwa na CNN, kama asingekua yule mfungwa wa kule gerezani aliyesababisha Al Kuwait kupatikana hakika Osama hadi leo angekua HAI). NAdhani hadi leo Obama hajatekeleza mpango wake huo wa kulifunga lile gereza hadi sasa. Nacho taka kusema hapa ni hiki, wenzetu wanajua namna ya kutofautisha kati ya kazi za siasa na za kitaalam; kwetu hapa mwana siasa ana uwezo wa kumwambia Daktari asitubu kwa kutumia dawa Mseto badala yake atumie SP na still mambo yakaenda tu vizuri.