serio
JF-Expert Member
- Apr 15, 2011
- 7,354
- 4,760
Kuna maswali kadhaa yanahitaji ufafanuzi:....basi nikiwa naisuuza ile chu pi mke wangu akaingia maliwatoni na kunikuta nikiisuuza ile chupi ya mpangaji mwenzetu....
Naunga mkono hojaBaba huo mzigo kuna dalili kuwa umechapa na kama huja uchapa kulikuwa na kila dalili ya si muda mrefu unge uchapa. Lakini mwishoni nimekupata tena umesema dada huyo yupo cngo na hujazoea kulala peke yako. Muombe huyo dada akupe hifadhi ya muda hadi mama watoto atakapo rudi.
Inachekesha kidogo inaonekana haupo serious na mkeo. Je ingetokea hivyo kwa mkeo si ungesha mng'oa meno.
Nimecheka sana hapa.maana mpangaj mwenzangu ni bachela nae akifua kuful zake huzianika nje,mvua ikinyesha na acpokuwepo huwa napata wakat mgumu sana!NIMUANULIE?au niziache?
Hapana sikufanya kusudi ila kuanguka kwa hii chu pi kumeniharibia sana.Haya mabafu ambayo ni ya ku-share na milango haina makomeo kaaz kwel!
Au ulifanya kusudi kutofunga mlango ili jirani aje kuchukua chupi yake?
Ha ha ha haa!
Hapana CD huyu binti chu pi yake ilianguka sasa ningeiacha angeniletea uzushi,nikaamua kufanya ustaarabu kwa kuisuuza. Nakwenda kuangukia nikitoswa nitaku PM.Vituko vya duniani na wewe. Unaonaje ungeokota ile chupi ukaitundika mlangoni bila kufua. Obvious una mahusiano nae mpaka chupi yake ikakuvutia kuishika na kufua.
Hama hiyo nyumba, mfuate mkeo huko alikoenda umrudishe, akikataa kurudi njoo kwangu mimi nitakupokea.
Nishapoa nashukuru.Uswahilini kuna vituko..
Pole sana.
Habari zenu wana JF,
Ni hivi mimi naishi nyumba ya kupanga na my wife wangu na kuna wapangaji wengine katika nyumba hiyo,sasa kuna binti single kahamia katika chumba kimoja katika hii nyumba,basi baada ya kuzoeana naye mke wangu anasema hamuamini ingawa nimemuhakikishia kuwa sijafanya naye mapenzi wala sifikirii,basi mke wangu akaanza kumletea vituko huyu binti mpaka wakagombana na hapa niandikapo ni kuwa hawaelewani.
Sasa tatizo leo hii yule binti kaingia maliwatoni na kuacha chu pi yake akining'inia nyuma ya mlango.
Basi mke wangu naye akaenda kuniwekea maji maliwatoni ili nikakoge,basi nilipoingia nikaiona ile chupi nyuma ya mlango na mie kuanza kujimwagia maji baridi.
Lakini nikiwa naendelea kukoga ile chupi ikaanguka kwenye yale maji ambayo ni machafu,basi nikaona ngoja niisuuze ili niirudishe tena nyuma ya mlango na nimtaarifu mwenye chu pi kwa kilichotokea,basi nikiwa naisuuza ile chu pi mke wangu akaingia maliwatoni na kunikuta nikiisuuza ile chupi ya mpangaji mwenzetu,basi likaanza bonge la zogo na kuniambia kuwa kumbe yule mpangaji mwenzangu nina uhusiano naye yaani mpaka chu pi namfulia!basi yeye kaamua kurudi kwao.