tatanyengo
JF-Expert Member
- Mar 30, 2011
- 1,133
- 282
Mbunge wa CHADEMA Halima Mdee alisema bungeni jana kuwa Chuo Kikuu Cha Dodoma (UDOM) kimekithiri kwa ubadhilifu wa fedha za serikali.
Akitoa mifano ya ubadhilifu huo alisema tangu chuo hicho kianzishwe mwaka 2007 kuna wafanyakazi takribani 250 wameisha acha kazi lakini mishahara ya baadhi yao bado inapelekwa chuoni hapo na kutafunwa na wajanja.
Pia alisema kuna baadhi ya watumishi wa chuo hicho wana mishahara miwili kinyume cha kanuni za utumishi wa umma. Na mbaya zaidi ni mishahara ya watumishi ambao ni marehemu mishahara yao kuendelea kupelekwa chuoni hapo.
Mdee aliendelea kusema kuwa mwaka 2010 uongozi wa chuo ulipopata fununu kuwa ukaguzi wa CAG ungefanyika chuoni hapo, uongozi wa chuo ukaandika barua serikalini kuomba mwongozo wa namna ya kutumia fedha zilizokuwa zimebaki.
My take:
Vyuo vikuu vinapaswa kuwa mfano wa kuigwa na taasisi nyingine nchini. Tunaomba pia wahusika kuimulika taasisi hiyo muhimu ili kusafisha uozo uliopo.
Akitoa mifano ya ubadhilifu huo alisema tangu chuo hicho kianzishwe mwaka 2007 kuna wafanyakazi takribani 250 wameisha acha kazi lakini mishahara ya baadhi yao bado inapelekwa chuoni hapo na kutafunwa na wajanja.
Pia alisema kuna baadhi ya watumishi wa chuo hicho wana mishahara miwili kinyume cha kanuni za utumishi wa umma. Na mbaya zaidi ni mishahara ya watumishi ambao ni marehemu mishahara yao kuendelea kupelekwa chuoni hapo.
Mdee aliendelea kusema kuwa mwaka 2010 uongozi wa chuo ulipopata fununu kuwa ukaguzi wa CAG ungefanyika chuoni hapo, uongozi wa chuo ukaandika barua serikalini kuomba mwongozo wa namna ya kutumia fedha zilizokuwa zimebaki.
My take:
Vyuo vikuu vinapaswa kuwa mfano wa kuigwa na taasisi nyingine nchini. Tunaomba pia wahusika kuimulika taasisi hiyo muhimu ili kusafisha uozo uliopo.