Yani wewe ni Oves kabisa.Nimeapa na nimekata shauri ya kwamba sitakaa nipige kura tena katika maisha yangu. Mara ya mwisho kwangu kupiga kura ilikuwa 2015 na sitarudia tena. Wanasiasa wanawatumia "wananchi wapiga kura" kama ngazi za wao kufika juu kwenye mafanikio, wakati hao Wananchi wanabakia hapo hapo walipo bila ya kupata mafanikio yoyote yale. Binafsi nimekataa "kutumia kura" yangu kama daraja la kuwavusha Wanasiasa kutoka kwenye umaskini na kwenda kwenye UTAJIRI wakati mimi niliyepiga kura nabakia na UMASKINI wangu. Siku ya kupiga kura nitakaa zangu nyumbani nikiangalia movie, sina muda wa kupoteza. Atakaye chaguliwa na achaguliwe mimi I DON'T CARE!