Chonde Chonde Ndugu zetu Wazanzibari, Msilete Fyoko Fyoko, Mtaumia bure!

Pasco mzee wangu nakulewa sana bandiko lako lkni najua unamkaanga huyo mropokaji, hajui madhara ya kauli zake za fyoko fyoko. akishauriwa na mkapa naye achanganye na zake hii ni karne ya 21 majeshi na polisi hawaogopewi aulize Libya,tunisia na Egypt watawala walikuwa na nguvu kama malaika leo wako wapi?
point
 
Wanabodi,

Baada ya lile tangazo la jana la Amiri Jeshi Mkuu wa nchi yetu, Dr. John Pombe Magufuli kumhusu yoyote atakayete fyoko fyoko popote alipo!.

Natoa wito kwa ndugu zetu Wanzibari, Chonde Chonde msilete fyoko fyoko!, upole, cheko cheko na bashasha za Jakaya Kikwete, zimetuponza Tanzania kama taifa, tukajiachia na kujisahau sana hadi kila siku kuleta fyoko fyoko na hakuna chochote ambacho kilifanyika!.

Magufuli sio Kikwete, jana katoa amri watu wasilete fyoko fyoko, ni kweli Watanzania katika umoja wetu tuitunze, tuienzi na kuithamini amani na utulivu uliopo, tusilete kabisa fyoko fyoko za aina yoyote!.

Naomba kukiri nimepandisha uzi huu kwa msipiration nilioipata kwenye mchango wa mwana jf huyu..

Magufuli atapeleka majeshi Zanzibar kwenda kusimamia amani na utulivu, ikitokea majeshi yakaua mtu, itakuwa mtu huyo ameleta fyoko fyoko!. Mtu akileta fyoko fyoko atashughulikiwa kikamilifu!. Ikitokea wengine wasi na hatia wakadhurika katika kututuliza hizo fyoko fyoko, then aliyesababisha madhara hayo ni muanzisha wa fyoko fyoko na sio mtulizaji au mdhibiti wa fyoko fyoko!.

Dawa ni moja tuu kwa Wanzanzibar, baada ya kumsikia Amiri Jeshi Mkuu akiwaonya msilete fyoko fyoko, hili sio ombi ni amri, hivyo msilete fyoko fyoko!.

Pasco
Hofu iko wapi Pasco, ulinzi upo na wakisusia kwenda kuchagua ZEC itawatangaza kuwa washindi, hata ukisusia uchaguzi ukijikuta umechaguliwa kuwa makamu wa kwanza wa rais, unaitwa kuapishwa na kusindikizwa kwenda kuapishwa? Hata wale masheha wa CUF watapitishwa na kuitwa kuwa masheha wateule, wasipojitokeza kuapishwa posho itaingizwa kwenye a/c zao kama kawaida, na makamu wa kwanza wa rais naye atapewa ulinzi na kupigiwa salute za kiitifaki hata asipokanyaga ofisini.
pasco take my words, na ninaomba uzi huu ubaki mpaka tarehe 25march.
 
magufuli-monduli.jpg


Katika mkutano wake na Wazee wa Dar es salaam aliwasibitishia wananchi wa Zanzibar kwakutumia mkutano huo kua Zanzibar anaikalia kijeshi na yoyote yule atakaye leta FYOKO FYOKO basi atashuhulikiwa na vyombo vya usalama (Dola).

VOICE OF ZANZIBAR
kutokana na vitendo vingi vya uvunjwaji wa haki za binadamu kwa upande wa Zanzibar vinavyo endelea kukisiri na kuwafanya wananchi wa Zanzibar kuishi kwa hofu na woga siku hadi siku bila kukemewa na kiongozi yoyote wa ccm na wahusika kufikishwa katika vyombo vya sheria bila kubaguliwa huyu ni wa chama gani au asili gani au wapi ana toka , imesibitisha zahiri kauli ya Mh Raisi John Pombe Makufuli kua kazi kubwa kwa Zanzibar si kuwatendea haki wananchi wa Zanzibar ,baali kazi yake kubwa nikulinda chama chake na sera zake kwa upande huo wa Muungano.

Hali hii na ukimya huu wa Mh Raisi wa Muungano na Amiri Jeshi Mkuu wa Tanzania imetufanya kuona kua hatutendei haki wananchi wa Zanzibar na kauli yake ya vitisho imezidisha kumuona kua anajaribu kutumia Jeshi lake ili kuwatisha wananchi wa Zanzibar na kuwatawala kimabavu kwa nguvu ya Vyombo vya Dola.

Ukiangalia wananchi wa Zanzibar tokea umalizike uchaguzi mkuu wa mwaka jana 2015 Oktober trh 25 wananchi wa Zanzibar wamekua watulivu na wenye kusikiliza viongozi wao kipi kinajiri zidi ya sito fahamu hii ya mkwamo huu wa kisiasa.

Lakini juu ya wananchi wengi wa Zanzibar na ukimya wao? viongozi wa chama tawala wameona ukimya wa wananchi wa Zanzibar hususani wafuasi wa cuf imekua ni udhaifu na ndio na kupata fursa ya kuwachokoza ili nchi ingie katika machafuko na mauwaji kama yalio tokezea tarehe 26/27 2001 wananchi wa zanzibar wasio pungua 60 kupoteza maisha yao na wengine kuwa na vilema vyakudumu na wengine kwenda kuomba ukimbizi nchi jirani ya Kenya katika kambi ya wakimbizi Shimoni.

VIAASHIRIO VYA UCHOKOZI ZIDI YA WANANCHI WA ZANZIBAR

Hivi sasa wananchi wa Zanzibar wamekuwa wakihujumiwa makazi yao sehemu zao zakutafutia riski na kupigwa ovyo ovyo na watu eti wasio fahamika ( Mazombi) huku vyombo vya dola vikishindwa kutoa kauli za kukemea kwa watu hao au kuwatafuta na kuwakamata na kuwafikisha kwenye vyombo vya Dola?.

Watu hao wanajulikana na wanatumia facilitate za Serekali zikiwemo magari ya Polisi na silaha za moto sabmashingani AK47 ambazo hupita mitani mchana kweupe na kufanya hujuma nyakati za mchana na usiku hufanya hujuma mbaya zaidi eti kuficha nyuso zao kwa kutumia soksi za kuficha uso.

Ziko njama nyingi tu zauchokozi wa viongozi wa ccm wanazo panga zidi ya raia na hususani maeneo wanayo kaa wafuasi wengi wa chama cha wananchi cuf, hivi karibuni katika maeneo ya Msumbiji Unguja walivuja mabanda ya biashara na kuiba mali za watu na kupiga watu ovyo ovyo huku serekali ya Smz na ile ya Muungano kushindwa kukemea kitendo hisho cha hujuwa kwa raia na mali zao.

MBINU NYENGINE ZINAZOPANGWA KUTUMIKA PEMBA LAKINI WANANCHI WAMEWEZA KUZIGUNDUAA

Hivi karibuni wafuasi wa ccm waliweka alama za X kuchoma shamba la kada wa ccm moto na banda la maskani ya ccm Kengeja , hii yote ni mbinu yaku weza kuwadisha wananchi na wafuasi wa chama cha wananchi cuf ili kupata kishingizio cha kuwakamata na kuwaweka ndani ili waweze kuwatesa .

Mbinu nyingine ambayo ilivuja na wanchi wakaweza kuigundua kabla ya kutumika , ilikuwa ni watu wenye asili ya unguja wanao ishi Pemba kupigiwa alama ya X na kuandikiwa maneno ya vitisho ili lengo kubwa la ccm nikutaka kuwagawa watu wa upande huu na upande mwengine kwa misingi ya kupandikiza chuki za kimaeneo.

lakini kutokana na mbinu hio kugundulikana na Wananchi wa wakazi wa Pemba ,walifanya jitihada za kupeana habari na kuambizana ili jambo hilo lisije likawa ni sababu za kuwagawa watu wenye asili ya unguja wanao ishi Pemba na ikawa wale wa Pemba wanao ishi unguja kufanyiana visasi na hujuma.

Kwa wakati huu tulonao kipindi kigumu cha Wananchi wa Zanzibar nilazima tushikamane na tusikubali kugaiwa kwa njia yoyote ile ya watawala watakayo weza kuitumia ili kuleta mtafaruki wa ubaguzi na fujo katikanchi yetu Zanzibar tuipendayo.

Hivi sasa yako mengi tu yanapangwa na kutayarishwa zidi yetu hususani yale maineo yenye wafuasi wengi wa cuf au sehemu zile zenye wananchi wengi wenye asili ya Pemba au ya kiarabu .

Hawa watawala wa ccm wameishiwa na hawana mbinu zozote zile njema na za herii zidi ya wananchi wa Zanzibar katika kuwafanyia wema na kuwasikiliza mamuzi yao nini wanataka , zaidi ya kuwatumia vitisho na nguvu eti wana nguvu za Dola?.

SIFA YA WANANCHI WA ZANZIBAR MILA NA UTAMATUNI WA WAZANZIBAR

Wananchi wa Zanzibar tokea hapo awali ni watu wenye kuishi kwa pamoja kwa udugu na upendo na ukarimu wa kuhurumianana na kupendana bila kujali huyu ana rangi gani na huyu ana toka wapi na ana dini gani na ndio ukaona wanzanzibar ni mchanganyiko wakila rangi na kabila .

Hii ndio sifa kubwa tulio risishwa wazanzibar kizazi hadi kizazi gererarion hadi generation ,sasa sifa hii tusikubali wananchi wa Zanzibar kuweza kuotoshewa kwa itikadi tu zakisiasa na utapia mlo wa madaraka na maslahi ya watu fulani, huu ndio utajiri wetu wananchi wa Zanzibar na ufahari wetu, tukija kukubali kulishwa matabishi haya basi itakua ni kizazi tulio kula hasara .

Lengo kubwa la watu wasio tutakia wema wazanzibar, Nikutuona wazanzibar tunaishi katika mazingira ya maisha ya chuki ,husdaa , visasi visivyo kwisha, ubaguzi na majungu , haya yote hayato tunufaisha sisi wala jamii yetu na kizazi chetu cha baadae.

Tushukulie mfano hai wa jirani zetu wa Tanzania bara?
Uchaguzi mkuu wa 25 oct ulifanyika na ukamalizika salama ? lakini tokea uchaguzi kumalizika hujasikia kua wananchi wa Bara wanaishi kwa hofu kutokana na kupigwa na kuvamiwa katika makaazi yao au sehemu zao zakufanyia biashara? why sisi Zanzibar wakati tunambiwa ni sehemu ya Muungano? na haliyakua Jeshi jingi lililopo hapa ni kutoka Tanzania Bara na mkuu wao wa Majeshi ni huyo tulio msikia jana anatutumi vitisho Amiri Jeshi mkuu ?.

RAMBI RAMBI ZA WAZANZIBAR KWA AMIRI JESHI MKUU JOHN POMBE MAKUFULI.

wananchi wa Zanzibar tunamtumia rambirambi Amiri jeshi Mkuu Makufuli kua sisi wananchi tulio wengi wa Zanzibar tunamwambia kua ukimya wetu sio udhaifu wetu ukaono tuko kimya ndio ukaleta chokochoko zako zakutuchokoza na kutaka kututawala kimabavu kwa nguvu za kijeshi ?

Sisi Wazanzibar kwa umoja wetu ambao tulionyesha katika uchaguzi mkuu wa oct 25 tunao uwezo huo huo wakuweza kuingia barabarani na kudai haki yetu ilio porwa na chama chako ,uwezo huo upo na ubabe wako na makeke yako basi waulize hao walio kutangulia kuwa wazanzibar ni watu gani ?

tutakapo amua kuingia barabarani usijidanganye kua utaua na kuweza kutusweka magerezani kama kweli mbabe wewe na Jeuri basi usingali ikimbiaa ikuluu na haliyakua uko mchini , ukepata kuwakaribisha wageni wako nyumbani kwako sio kuwakimbia huo ni uzaifu wa kuongopa hoja eti kwakuogopa maswala ya kulizwa kuhusu Zanzibar.

Swala la Zanzibar litakuganda kama Kupe na Ngombe na vitisho vyako havito tusababisha ku giveup katu, Ni wazanzibar tutapigania haki yatu kwa njia yoyote ile Zanzibar ni nchi yetu na vitovu vya bibi na babu zetu vimezikwa hapa na hapa ndipo kwetu hatuna kwengine kwakenda huo ubaguzi wenu wa uarabu,uhindi na uhatimu kuona kuwa wazanzibar mutawagawa kwa misingi hio basi mumesherewa .

Kama ni kutugawa kwa visingizio vya Ukabila ? basi jiangalieni huko Bara muna makabila mangapi ndani ya Tanganyika? sisi sote hapa ni Wazanzibar no matter rangi lakini Zanzibar ni ya wazanzibar wenyewe .

M/Mungu ibariki Zanzibar na watu wake.

chanzo.Mh Makufuli ame-declared kua Zanzibar anaikalia Kijeshi - Mzalendo.net
 
Zanzibar sio nchi bali ni sehemu ya JMT, hivyo JWTZ kutapakaa Zanzibar yote ni halali!. Utaikaliaje kijeshi nchi yako mwenyewe!.

Wanzanzibari siku zote wanaongea as if Zanzibar ni nchi!.

Zanzibar sio nchi!, ndani ya set up ya Muungano Zanzibar ni kama Lindi tuu au Singida!.

Pasco
 
Ujenzi dhaifu wa hoja. Hutakiwi kutumia hisia na fikra za ki juha katika mambo ya kisheria na facts zipo.

Unazingusha maneno na kupotosha ukweli kwa faida ya nani?
 
Zanzibar sio nchi bali ni sehemu ya JMT, hivyo JWTZ kutapakaa Zanzibar yote ni halali!. Utaikaliaje kijeshi nchi yako mwenyewe!.

Wanzanzibari siku zote wanaongea as if Zanzibar ni nchi!.

Zanzibar sio nchi!, ndani ya set up ya Muungano Zanzibar ni kama Lindi tuu au Singida!.

Pasco
Mkuu acha hizo bhana! Katiba ya JMT, Aya ya kwanza ya tafsiri ya Jina la Tanzania umeisoma? Singida ina rais? Singida ina katiba yake? Singida ina baraza la mawaziri?
 
Zanzibar sio nchi bali ni sehemu ya JMT, hivyo JWTZ kutapakaa Zanzibar yote ni halali!. Utaikaliaje kijeshi nchi yako mwenyewe!.

Wanzanzibari siku zote wanaongea as if Zanzibar ni nchi!.

Zanzibar sio nchi!, ndani ya set up ya Muungano Zanzibar ni kama Lindi tuu au Singida!.

Pasco


wewe kweli ni mzima wa akiri?


swissme
 
Zanzibar sio nchi bali ni sehemu ya JMT, hivyo JWTZ kutapakaa Zanzibar yote ni halali!. Utaikaliaje kijeshi nchi yako mwenyewe!.

Wanzanzibari siku zote wanaongea as if Zanzibar ni nchi!.

Zanzibar sio nchi!, ndani ya set up ya Muungano Zanzibar ni kama Lindi tuu au Singida!.

Pasco

Hizo ni fikra za bangi.
 
Tatizo la Zanzibar ni CCM kwa ujumla wake wala si Magufuli kama mtu. Hata kabla hajaingia madarakani tumeshuhudia aliyoyatenda BWM na baadaye tumeshuhudia unafki mkubwa wa JMK kulishughulikia tatizo la ZANZIBAR pamoja na kuahidi katika hotuba yake ya kwanza bungeni 2005 kuwa analifanya kuwa historia lakini ni yeye aliyechochea hali ya sasa

Magufuli kayakuta haya na anaimbishwa na chama chake hawezi kwenda kinyume nao kwa kuogopa kutopata saport ya chama.
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom