Chonde Chonde Ndugu zetu Wazanzibari, Msilete Fyoko Fyoko, Mtaumia bure!

Kwa nini anawatisha wakati kasema hilo hawezi kuliingilia?
Kwa nini asiwaachie wazanzibar walimalize wenyewe sasa,vitisho vya nini kwa suala lililojuu yake kimaamuzi?
Afrika lazima tuwarudishe wakoloni ili watutawale tena.....
Mpaka tupate uhuru wa kusema, hili ndiyo na hili hapana na si kuamliwa na viongozi ambao ni waajiriwa wetu! Lazima viongozi hawa watambue sisi ndo tumewaajiri!
Wao wapige tu hata Libya alisema hivi hivi...pigeni.....halafu jumapili mnakuwa mbele karibu na padre na Ijumaa kanzu nyeupeeee! jamani...Neno haki ni rahisi kweli kulitamka..lakini kulisimamia ni zito kama kubeba mlima....
Fyoko...pigeni......
Huyu MUNGU ataona mengi mwaka huu......
Mkileta mchezo Magu hana mchezo ata watandika.
 
Si alisema haingilii siasa ya zanzibar? Sasa anawatisha ili iweje? wawaache wazanzibar watafute haki yao. Kutumia mabavu kunaweza leta maafa makubwa
Kazi yake si kuingilia siasa za zanzibar bali ni kuhakikisha watanzania wote wako na amani na mipaka yote inalindwa na atakaye leta fyoko fyoko atatandikwa.
 
Ukweli utabaki magufuli hafai na wanaipeleka tz kubaya na anaiabisha tz na hatofanikiwa hilo analo taka kuwadanganya watu kama hakupewa msaada na jumuia ya kimataifa hawezi kuendesha nchi na letu hicho tutaona
Mlizoea kuwaita watu dhaifu eeeh! Mkileta fyoko fyoko mtatandikwa kabisa....
 
There is nothing in our book, the Qur'an, that teaches us to suffer peacefully. Our religion teaches us to be intelligent. Be peaceful, be courteous, obey the law, respect everyone; but if someone lays a hand on you, send him to the cemetery.
Malcolm X
 
Nimeamini Zanzibar siyo nchi,ni mkoa tuu ndani ya Tanzania.Sioni maana ya kuwa na rais wa zanzibar.Bora ateuliwe mkuu wa mkoa zanzibar
Mkuu Zanzibar kumejaa wachumia tumbo na ndo hao hao wanajidanganya kuwa Zanzibar ni nchi....

Iko wazi kabisa kwamba Zanzibar sio nchi...nmetokea kumdharau sana Shein .....ni kama zezeta flan hivi linalofuata upepo.....

poleni wazanzibar...na kama alivosema mtoa mada acheni fyoko fyoko...viongoz wa ccm Zanzibar ...kama wangekuwa na akili kidogo tu, wangehoji juu ya kauli ya Rais!!!!
 
Maneno mazur ameongea, ss ambao hatuogopi kutismwa tunaelekea somalia kumalizia masomo yetu, byebye Tanzania we will be back soon inshallah
Uko serious mkuu?.. Japo siafiki njia mnayotaka kutumia kudai Haki, lakini naamini ndiyo njia pekee ilobaki...

chondechonde mkuu....msije mkatulipua
 
Kazi yake si kuingilia siasa za zanzibar bali ni kuhakikisha watanzania wote wako na amani na mipaka yote inalindwa na atakaye leta fyoko fyoko atatandikwa.
Ishu ya mipaka ni tofauti na zanzibar. Hiyo ni ishu ya wizara ya mambo ya ndani. Sasa yeye kama nani kuwasemea wazanzibar
 
Hivi Jecha alishauriana na nani kabla ya kutoa uamuzi wa kufuta matokeo?

Namaanisha kama Maalim Seif alikuwa akifahamu kupitia mabandiko basi Jecha alipaswa kuwaita ndani wahusika wa pande zote na kuwataarifu juu ya uamuzi wake huo.

Lakini nafikiri ile solution ilotolewa mwaka 1995 haikuwezekana kutolewa.

Namuona Jecha kama mtu aliejitwika mzigo mzito sana ambao utamwandama sana.

Alishauriana na nani?
 
Pasco pilipili usoila yakuwashiani?

Waachie Wazanzibari na nchi yao. Tusiwaingilie katika maamuzi yao. Kukubali au kutokukubali kwao kushiriki kwenye uchaguzi unaorudiwa ni hiari yao. Haituhusu.

Sijawaona Wazanzibari wakiingilia mambo ya Tanganyika, kwa maneno, mawazo au hata vitendo.

Waache! Ni haki yao!
 
Pasco mzee wangu nakulewa sana bandiko lako lkni najua unamkaanga huyo mropokaji, hajui madhara ya kauli zake za fyoko fyoko. akishauriwa na mkapa naye achanganye na zake hii ni karne ya 21 majeshi na polisi hawaogopewi aulize Libya,tunisia na Egypt watawala walikuwa na nguvu kama malaika leo wako wapi?
 
wazungu wanamtafta sana huyu jamaa na hili zigo la mavi la zenji ndio mkwamo wake. we unahisi nchi unazozipigia magoti miaka yote kuwaomba leo mwataka kusimama wenyewe kwa ujeuri? sasa hawana pakumkomoa Zaidi ya zenji.
 
By definition chama chetu hakiwezi leta fyoko fyoko. Kwa sababu ni sisi tunao-amua fyoko fyoko ni nini na imetokea wakati gani. Mheshimiwa Chaje haingiliwi lakini Makamu wake alipoendelea kuhakiki kura na makamishina wenzake tuliona wanaleta fyoko fyoko tukawapelekea jamaa na Makamo akaondolewa chini ya ulinzi. UKAWA wakaanzisha kituo chao cha kuratibu kura tukaona hii ni fyoko fyoko tukawasomesha namba. Kituo cha "Marope afuatae December" kikaendelea kutesa hata JK alisema walijua wanaongoza. Wakati ule Pinda aliposema "wapigwe tu" mlilia lia sana sasa jemadari kasema leta fyoko fyoko uone. Hutaki ya ZEC nenda mahakamani -mahakama iko huru ingawa Fatma ana wasiwasi-lakini mimi nasema iko huru. Usipo amini hili ukitumia njia nyingine waleta fyoko fyoko. Mimi naona hata maandamano ni fyoko fyoko tu labda yale ya rangi niipendayo.
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom