Jibaba Bonge
JF-Expert Member
- May 6, 2008
- 1,246
- 401
Mgombea urais wa Ccm amekuwa akifanya mikutano ya kampeni sehemu mbalimbali nchini. Mikutano hiyo imekuwa ikifanywa ionekane mikubwa sana kwa kusomba watu kwa mabasi na malori kutoka sehemu za mbali na mkutano husika.
Watu wengi katika mikutano hiyo wamekuwa katika mavazi ya rangi kijani na njano, rangi za ccm. Watu hawa wako katika makundi yafuatayo:- 1. Wanachama wa ccm wa jimbo ambapo mkutano unafanyika (wanaolipwa kanga, kofia na mashati yenye rangi za ccm) , 2. Wanachama wa ccm toka majimbo ya mbali (wanaolipwa kanga, kofia na mashati yenye rangi za ccm na zile elfu mbilimbili ua tanotano au hata kumikumi na petrol kama ilivyofanyika Arusha ), 3. Wasio wanachama wanaotafuta mlo wa siku kwa kufuata upepo unakovumia (hawa hufanyiwa ka no. 2 hapo juu), 4. Wanaofuata maonyesho ya wasanii waliopo kwenye mikutano hiyo.
Lengo la ccm kufanya hivi ni ili mikutano yake ionekane mikubwa sana na hivyo kuuhadaa umma kuwa inapendwa sana na wananchi. Hii inatokana na watu waliokuwa kwenye mkutano jimbo A ni haohao unawakuta Jimbo B na Jimbo C n.k , kazi ya malori na mabasi ya kukodiwa au ya wanaodaiwa wakereketwa.
Kama hawa watu ni wanachama wa ccm wa majimbo inapofanyikia mikutano ya kampeni, walikuwa wapi wakati wa kura za maoni? Mbona idadi ya kura zote za wagombea , nzuri na zile zilizoharibika hazifanani na idadi ya watu wenye sare katika mikutano? Sehemu nyingine jumla ya kura za maoni haikufika hata 10,000 kwa jimbo zima (na kutokana na jiografia ya sehemu hizo siyo rahisi wote wakawepo kwenye mkutano mmoja bila kuwezeshwa), hawa watu wengine wametoka wapi? Ni makundi mane niliyoeleza hapo juu.
Kwa sasa chama tishio kwa ccm ni chadema, kama alivyo sema memba mmoja humu kuwa mti wenye matunda ndiyo unaopopolewa mawe; hayo yamedhihirika kwa chadema kufanyiwa rafu mbalimbali wakati huu wa kampeni.
Chadema chonde chonde pamoja na kampeni zinazoendelea, muandae pia mikakati ya kulinda kura wakati wa upigaji na uhesabuji. Ccm wanaweza kuchakachua kura kwa kuingiza kura za mgombea wao wakati wa upigaji kura au kuondoa kura za wapinzani wakakti wa kuhesabu. Watajifanya kujastify matokeo yao na mahudhurio ya watu kwenye mikutano yao. Yalishafanyika hayo miaka ya nyuma kule zanzibar, Ubungo na sehemu nyingine nyingi. CHADEMA MUWE MAKINI KULINDA KURA.
Watu wengi katika mikutano hiyo wamekuwa katika mavazi ya rangi kijani na njano, rangi za ccm. Watu hawa wako katika makundi yafuatayo:- 1. Wanachama wa ccm wa jimbo ambapo mkutano unafanyika (wanaolipwa kanga, kofia na mashati yenye rangi za ccm) , 2. Wanachama wa ccm toka majimbo ya mbali (wanaolipwa kanga, kofia na mashati yenye rangi za ccm na zile elfu mbilimbili ua tanotano au hata kumikumi na petrol kama ilivyofanyika Arusha ), 3. Wasio wanachama wanaotafuta mlo wa siku kwa kufuata upepo unakovumia (hawa hufanyiwa ka no. 2 hapo juu), 4. Wanaofuata maonyesho ya wasanii waliopo kwenye mikutano hiyo.
Lengo la ccm kufanya hivi ni ili mikutano yake ionekane mikubwa sana na hivyo kuuhadaa umma kuwa inapendwa sana na wananchi. Hii inatokana na watu waliokuwa kwenye mkutano jimbo A ni haohao unawakuta Jimbo B na Jimbo C n.k , kazi ya malori na mabasi ya kukodiwa au ya wanaodaiwa wakereketwa.
Kama hawa watu ni wanachama wa ccm wa majimbo inapofanyikia mikutano ya kampeni, walikuwa wapi wakati wa kura za maoni? Mbona idadi ya kura zote za wagombea , nzuri na zile zilizoharibika hazifanani na idadi ya watu wenye sare katika mikutano? Sehemu nyingine jumla ya kura za maoni haikufika hata 10,000 kwa jimbo zima (na kutokana na jiografia ya sehemu hizo siyo rahisi wote wakawepo kwenye mkutano mmoja bila kuwezeshwa), hawa watu wengine wametoka wapi? Ni makundi mane niliyoeleza hapo juu.
Kwa sasa chama tishio kwa ccm ni chadema, kama alivyo sema memba mmoja humu kuwa mti wenye matunda ndiyo unaopopolewa mawe; hayo yamedhihirika kwa chadema kufanyiwa rafu mbalimbali wakati huu wa kampeni.
Chadema chonde chonde pamoja na kampeni zinazoendelea, muandae pia mikakati ya kulinda kura wakati wa upigaji na uhesabuji. Ccm wanaweza kuchakachua kura kwa kuingiza kura za mgombea wao wakati wa upigaji kura au kuondoa kura za wapinzani wakakti wa kuhesabu. Watajifanya kujastify matokeo yao na mahudhurio ya watu kwenye mikutano yao. Yalishafanyika hayo miaka ya nyuma kule zanzibar, Ubungo na sehemu nyingine nyingi. CHADEMA MUWE MAKINI KULINDA KURA.