Chombezo: Baba P… Baba Pili… Baba Pilima!

Chombezo: Baba P… Baba Pili… Baba Pilima!

Kanungila Karim

JF-Expert Member
Joined
Apr 29, 2016
Posts
20,746
Reaction score
25,662
SEHEMU YA 01

Samahani kaka, sijui hiki kiti kina mtu?” aliuliza Kate au maarufu kwa jina la mama Pilima!
Ilikuwa kwenye baa ya Dolphin, iliyopo kwenye Jiji la Tanga maeneo ya Kwaminchi…
“Hapana anti, unaweza kuchukua tu maana aliyekaa ameshaondoka,” alijibu mwanaume mmoja aliyekutwa amekaa kwenye kiti pembeni ya meza hiyo.
Mama Pilima alikichukua kiti hicho na kuanza kutafuta meza nyingine tupu ili akae lakini akaikosa, akarudi na kiti mpaka kwenye meza hiyo kwa sababu mwanaume huyo alikaa peke yake…
“Samahani tena! Naweza kukaa hapa!”
“Unaweza kukaa tu maana hakuna mtu mwingine atakayekuja kukaa.”
Mama Pilima aliweka kiti hapo na kukaa kisha akaangalia upande walipokaa wahudumu lakini kwa bahati, mhudumu mmoja alisimama nyuma yake akisubiri akae ili amsikilize…
“Anti naomba bia ya baridi sana.”
“Bia gani?”
“Ooo! Lete Mount Meru.”
Wakati mhudumu ameondoka, mama Pilima alimgeukia yule mwanamke huku akijipepea kwa kitambaa kupunguza jasho…
“Samahani kwa usumbufu lakini,” alisema mama Pilima.
“Wala usijali,” alisema yule mwanaume huku akimwangalia mama Pilima kwa macho ya kumtathmini. Kila jicho lake lilipotua, ilikuwa moyoni akis ema, ‘lakini umeumbwa! Utakuwa umeolewa kweli wewe? Mbona kama nimevutika na wewe!’
Na mama Pilima naye alipokutana macho na mwanaume huyo alimwangalia kama anayesema, ‘ukinitongoza nitakubali, lakini siwezi kukuanza maana naona unanitamani sana.’
Wakati wawili hao kila mmoja akimuwaza mwenzake kufuatia kumtamani kimahaba bia ililetwa.
Mama Pilima aliimimina yote kwenye glasi kubwa maana alikuwa na kiu sana. Aliipiga yote kwa mpigo huku macho yakiwa kwa mhudumu kama anayesema, ‘usiende sasa, si unaona namaliza hii.’
“Nikuongeze anti?” mhudumu alimuuliza kwa sauti iliyojaa mshangao mkubwa. Mama Pilima alikubali kwa kutingisha kichwa.
Hata hivyo, kuondoa usumbufu alimwambia amletee mbili kabisa.
“Du! Kweli wanawake wengine ni balaa… yaani huyu dada kaikata bia yote tena ya baridi bila kupumzika? Hii ni hatari!” yule mduhumu aliwaza.
Mhudumu alipoondoka, mama Pilima akamwangalia yule mwanaume na kusema…
“Sikukeri?”
“Wala!”
“Basi nashukuru sana…maana kuna watu wakikaa kwenye meza kama hivi wanapenda kukaa wenyewe tu.”
“Mimi wala,” alirudia kusema yule mwanaume…
“Oke, mimi naitwa Keti au mama Pilima…mwenzangu?” alianza kujitambulisha mama Pilima hata bila ya kuombwa…
“He! Kweli ndiyo jina lako?” alishtuka yule mwanaume…
“Ndiyo! Kwani vipi?”
“Mimi mke wangu pia anaitwa Keti lakini yeye ni mama Pili…”
“Mh! Hayo kweli maajabu! Ilikuajekuaje mpaka kufanana majina yetu na ya watoto?” aliuliza mama Pilima…
“Ndiyo nashangaa.”
“Kwa hiyo wewe ni baba Pili..?”
“Eee baba Pili!”
“Unaitwa nani ukiachana na jina la mwanao la baba fulani..?”
“Mimi naitwa Sam…”
“Hamna bwana,” alisema yule mwanamke huku akisimama na kuweka glasi ya bia mezani…
“Hamna nini sasa?”
“Yaani mimi nifanane majina na mkeo, wewe ufanane na mume wangu! Inawezekana kweli?”
“Kwani mumeo naye anaitwa Sam?”
“Eee! Ndiyo nashangaa hapa…”
“Mh! Hiyo kweli kali. Si ajabu hata makabila mimi na mumeo ni sawa?”
“Inawezekana baba Pili. Wewe kabisa gani?”
“Natoka Mkoa wa Dodoma…”
“Unaona sasa baba Pili…na mimi Sam mwenzako anatoka mkoa huohuo? Mkeo je?”
Baba Pili aliachia tabasamu na kusema…
“Aaa! Haiwezekani na wewe ukafanana kabila na mke wangu bwana. Itakuwa too much sasa!”
“We nitajie…wewe unatoka Mkoa wa Dodoma, mume wangu pia hukohuko. Je mkeo anatokea mkoa gani?”
“Yeye mke wangu anatokea Mkoa wa Dodoma pia…”
“Noo! Noo! Napingana na wewe baba Pili. Kinachoonekana hapa kuna kitu unakitengeneza…”
“Kwa nini? Kwani mimi nakujua wewe?”
“Inawezekana unanijua kiroho au kimwili,” alisema mama Pilima akiwa amesimama bado tangu aseme zile noo zake!
“Mimi sijawahi kukuona hata siku moja. Lakini jua Mungu ana makusudi yake mama Pilima. We fikiria ni kwa nini ulikuja kuomba kiti kwangu? Halafu ukakosa pa kukiweka ukaja kukiweka hapahapa ulipokitoa?”
“Asee kweli kabisa baba Pili. Hapa nadhani pana neno tunaambiwa,” alisema mama Pilima…
“Eee! Nyie mnaishi wapi?” aliuliza baba Pili…
“Magomeni Kagera…”
“Ah! Nimechoka sana jamani…”
“Kwa nini?”
“Sisi tunaishi Magomeni Mwembechai!”
“He! Kwa hiyo wote ni Magomeni?”
“Ndiyo maana yake.”
“Watoto wako wanasoma wapi?”
“Watoto mtoto? Mimi nina mtoto huyohuyo mmoja tu…”
“Aaa! Noo bwana…nooo!”
Je, nini kilitokea?
 
SEHEMU YA 02


“Sisi tunaishi Magomeni-Mwembechai!”
“He! Kwa hiyo wote ni Magomeni?”
“Ndiyo maana yake.”
“Watoto wako wanasoma wapi?”
“Watoto mtoto? Mimi nina mtoto huyohuyo mmoja tu…”
“Aaa! Noo bwana…nooo!”SASA JIACHIE MWENYEWE…

Mhudumu alitokea na kuingilia mazungumzo yao kwa kumuuliza baba Pili kama anataka kuongezea kinywaji…
“Tuongezee tafadhali,” alisema baba Pili…
Baada ya mhudumu kuondoka, waliendelea…
“Ina maana tunaweza kufanana kwa kila kitu kiasi hicho?” aliuliza baba Pili…
“Na mimi ndiyo nashangaa,” alijibu mama Pilima…
“Mh! Yaani hadi eneo la kuishi, yaani wote Magomeni?”
“Ndiyo hapo sasa.”
Moyoni baba Pili aliamini ile ndo’ ilikuwa fursa pekee ya kumnasa mwanamke huyo aliyeonekana kwake ana mvuto…
“Lakini kama mwingi wa habari…maana ukiona mwanamke unaongea naye na anakukodolea macho bila kufumbafumba, ogopa,” alijisemea moyoni mwanaume huyo.
Sasa wakawa kama marafiki waliojuana siku au miaka mingi sana. Walipiga stori nyingine za kifamilia na za nje ya familia. Za kifamilia zilikuwa hizi…
“Sasa mama Pilima, kama kuna baba Pilima unawezaje kutoka kukaa baa peke yako?” aliuliza baba Pili…
“Ah! Unajua ukifanya utafiti utagundua kuwa, wanaopenda kulewa, katika kila watu kumi, sita wana stresi zao, wanne tu ndiyo wanakwenda kwa matakwa yao…”
“Sasa wewe mama Pilima upo kundi gani?”
“La watu sita…teh! Teh! Teh!” alijibu mama Pilima na kucheka kidogo…
“Una stresi?”
“Ndiyo maana yake!”
“Zaidi ni nini?”
“Ah! Unajua tena mambo ya ndoa baba Pili…”
“Yamefanyaje?”
Mama Pilima akaachia tabasamu kidogo kisha akamwangalia baba Pili kwa macho ya mlegezo…
“Mambo ya aibu bwana,” alisema mama Pilima…
“Mh! Sisi wanandoa hatuna mambo ya aibu. Labda kama tungekuwa mabachela…teh! Teh! Teh!”
Mama Pilima aliamua kuachia ukweli kama kawaida ya wanawake…
“Unajua mimi na mume wangu, hata kuzaa ni kama Mungu tu…”
“Kwa nini iwe kama Mungu tu…”
“Ah! Yaani ningejua…wala…”
“Nini tena jamani mama Pilima?”
“Unajua mimi nilifunga ndoa bila kukutana kimwili na mume wangu…”
“Enhee..?”
“Tukiwa honeymoon ndiyo nikabaini tatizo…”
“Tatizo gani mama Pilima?” aliuliza baba Pili macho yote yakiwa kwenye uso wa mwanamke huyo ambaye katika kuongea alikuwa akibinua midomo, mara alegeze macho, mara aachie tabasamu la huba. Ilimradi tu!
“Nilishangaa sana, mume wangu alipoanza tu palepale akamaliza. Na mbaya zaidi akimaliza hawezi kuendelea tena mpaka upite mwezi na siku kadhaa…”
“Lo! Kweli hilo tatizo mama Pilima…”
“Umeona ee?”
“Basi bora angekuwa anasubiri hata dakika mbili, yaani yeye ni sekunde saba tu.”
“Sekunde saba!” alishangaa baba Pili…
“Ndiyo sekunde saba…siku nyingine hata kabla ya kuanza kwa mechi.”
Hapo baba Pili alijikuta akiangalia pembeni kwa aibu. Maana alimwona mama Pilima kama ameenda ndani sana. Halafu na yeye na vile alishamtamani, ikawa kwake ni kama anapunguziwa kazi…
“Lo! Kwa hiyo unahisi kulewa ndiyo sababu ya kukufanya uweje?”
Kwa kweli nikilewa, nikifika nalala zangu tu…teh Teh! Lakini nisipolewa, da! Namsumbua nikijua wazi kwamba, atanitesa tu.”
“Mimi naomba kukushauri,” alisema baba Pili. Mama Pilima akakaa mkao wa kusikiliza kwa undani zaidi…
“Enhe! Nasikiliza wazo lako baba Pili…”
“Badala ya kunywa pombe mpaka kulewa, ungetafuta wa pembeni ili awe mkata kiu yako,” alisema baba Pili huku akiangalia chini. Alijua si ushauri mzuri lakini kwa sababu yeye anafukuzia mzigo ilibidi aseme hivyo ili apime!
“Mh,” aliguna mama Pilima huku na yeye akiangalia upande mwingine kwa walipokuwa wamekaa wahudumu…
“Nimekukwaza kwa ushauri wangu mama Pilima?”
“Kwa kiasi fulani umenikwaza sana…”
“Kwa nini?”
“Sijawahi kusaliti na wala sipendi. Ingawa kama mwanamke naweza nikawa katika hali ya kujisikia kufanya hivyo lakini huwa najionya.”
Baba Pili alihema kwa nguvu na kumwangalia mwanamke huyo kisha akasema…
Je, nini kilitokea?
 
SEHEMU YA 03


ILIPOISHIA..
“Sijawahi kusaliti na wala sipendi. Ingawa kama mwanamke naweza nikawa katika hali ya kujisikia kufanya hivyo lakini huwa najionya…”
Baba Pili alihema kwa nguvu na kumwangalia mwanamke huyo kisha akasema;
SOGEA NAYO…
“Unafikiri unaweza kukaa hivyo kwa kipindi gani?’ aliuliza baba Pili.
“Kwa kipindi kirefu lakini kumsaliti mume wangu naona ngumu sana,” alisema mama Pilima, kwa kumwangalia tu ungegundua kwamba aliamua kukaza kidogo, yaani kama gari, lilijifanya kutowaka ili litekenywe zaidi…
“Kwani kuna ubaya gani kama utatafuta kitu cha kukuridhisha hasa unapoona hauridhiki? Mama Pilima, tafuta haki yako, kufikishwa unapotaka kufika ndiyo kitu cha msingi kwenye mwili wako,” alisema baba Pili, sasa aliamua kumkazia macho mwanamke huyo, macho yenye kuelezea hisia zote za kimapenzi….
“Jamani mimi naogopa, atajua tu,” alisema mama Pilima….
“Atajuaje sasa? Au utamwambia?”
“Nimwambie! Sijitaki!”
“Sasa atajuaje? Hiyo itakuwa siri yako wewe na huyo mtu, yaani mtakuwa mkipiga shoo kimyakimya, hata majirani hawatajua,” alisema baba Pili….
Mama Pilima akanyamaza, alimwangalia baba Pili kwa macho ya kuita, yaliyolegea kama nyanya, alijitahidi kuyarembua kwa ishara ya kumwambia baba Pili, ‘sasa inakuwaje? Upo fiti nikupe chansi?’
Baba Pili alikuwa na mawazo yake, alichokifikiria kichwani mwake kilikuwa ni kumtega mwanamke huyo, kwanza ajue kama alikuwa mwepesi au laini.
Alishaanza kuchombeza, mifano mingi ya kumwambia amchukue mwanaume yeyote pasipo kujiweka wazi kwamba alitaka huyo mwanaume awe yeye.
“Kwa hiyo?” aliuliza baba Pili mara baada ya kupita ukimya kidogo.
“Ndiyo najifikiria hivyo mwenzio…”
“Jifikirie basi halafu chukua maamuzi, kila mwanamke anataka kuridhishwa bwana…” alisema baba Pili.
Waliendelea kuzungumza kwa muda huku taratibu wakiendelea kunywa pombe zao, walipomaliza, wakaagana tayari kwa kuondoka.
“Jamani! Kwa hiyo ndiyo basi hivyo?” aliuliza baba Pili.
“Kivipi tena?”
“Hata namba ya simu, sasa tutawasiliana vipi baada ya hapa?”
Mmh! Aya, subiri nikupe, andika..” alisema mama Pilima, hapohapo akampa namba ya simu baba Pili kisha kuondoka.
Njiani, baba Pili alichanganyikiwa, akawa hoi, mama Pilima alimuweka kwenye wakati mgumu, kwa kumwangalia tu, alionekana kuwa mwanamke mtundu sana kwenye sita kwa sita, kichwa chake kilimfikiria sana.
Kwa upande wa mama Pilima sasa, alipagawa, akasahau kama alikuwa mke wa mtu, mwanaume aliyekutana naye baa, alimuweka njia panda. Kiukweli hakutaka kabisa kumsaliti mumewe lakini kwa kile kilichokuwa kikiendelea, alishindwa kuvumilia.
“Kwa hiyo? Jitahidi tu, hatajua,” mama Pilima alisikia sauti ya baba Pili kichwani mwake.
“Nitajaribu…” alijikuta akiongea kwa sauti.
Wakati akifikiria hayo, ghafla simu yake ikatoa mlio wa kumjulisha kwamba kuna meseji ilikuwa imeingia, hapohapo akaifungua, alipoliona jina la baba Pili, akahisi mapigo yake ya moyo yakidunda kwa nguvu.
“Umefika?” iliuliza, harakaharaka akajibu…
“Ndiyo, nimejifungia chumbani tu, mpweke kweli…”
“Kwani baba Pilima hayupo?”
“Hayupo, amekwenda kuchukua mizigo yake ya ofisini, aliniambia kwamba kesho anasafiri, anakwenda Tanga kikazi, atakaa kwa wiki moja, hapa ndiyo nimechanganyikiwa, sijui itakuwaje,” aliandika mama Pilima.
Baba Pili hakutaka kuvumilia kuchati tu kwenye simu, alijiona anachelewa, hapohapo akamtwangia, alitaka kuzungumza naye zaidi.
“Umesemaje vile?” aliuliza baba Pili.
“Mume wangu anasafiri kesho…”
“Kweli?”
“Ndiyo! Sasa sijui itakuwaje…”
“Kwani huyo mtu umeshampata? Au mpaka umtafute?” aliuliza baba Pili.
“Bado…yaani sijui nitampata wapi! Kwanza najua leo hapa huyu mzee sijui kama atanipa haki yangu, na hata akinipa, sitaridhiki mie…” alisema mama Pilima kwa sauti ya kulalamika.
“Mmmh! Kwa hiyo itakuwaje? Au tuonane sehemu tulizungumzie hilo…”
“Lini?”
“Kesho.”
“Saa ngapi?”
“Muda wowote…yaani mimi nipo free, siendi popote pale, yaani popote pale sitokwenda,” alisema baba Pili, alisisitiza zaidi ili aonekane kweli alikuwa free.
“Basi tutapanga tuone inakuwaje…”
“Sawa..nimekuelewa, ninatamani sana nikuone, tena nimekumisi mno….” alisema baba Pili.
“Mmh! Yaani kipindi kifupi hiki umenimisi?”
“Ndiyo! Niliipenda sana kampani yako, umechangamka sana, unapendeza na unajua kuzungumza na mwanaume, naamini baba Pilima anafaidi sana dodo…” alisema baba Pili na mama Pilima akatoa kicheko kilichomwambia baba Pili, ‘na wewe unataka kula dodo? Basi karibu sisi twala…’
Itaendelea
 
SEHEMU YA 04


“Ndiyo! Niliipenda sana kampani yako, umechangamka sana, unapendeza na unajua kuzungumza na mwanaume, naamini baba Pilima anafaidi sana dodo…” alisema baba Pili na mama Pilima akatoa kicheko kidogo kilichomwambia baba Pili, na wewe unataka kula dodo? Basi karibu sisi twala…
ENDELEA SASA…
Mama Pilima alifika nyumbani akiwa mchangamfu hasa baada ya kukutana na baba Pili. Aliamini ameingiza kitu kipya katika maisha yake ya siku hiyo.
Aliweka simu juu ya meza, wifi yake anaitwa Sonia, alikuwa amekaa sebuleni. Mama Pili alikwenda chooni.
Baba Pili alipofika nje ya nyumba yake, aliamua kumpigia simu mama Pilima halafu ndiyo aingie ndani…
“Ngoja nimcheki huyu kwa simu kwanza ndiyo niingie, sijui kafika salama? Yaani bonge la demu ila hajijui tu…mtu kaumbwa utadhani kilitumika kiwanda…mimi yale macho yake du…halafu ana mwanya f’lani hivi…lakini saa zile alipoinuka kwenda toileti ndiyo nikamkubali.
“Ile ndiyo shepu bwana! Kabinuka halafu katikati pameingia…kwa kweli ni demu bomba kama nitampata lazima awe nyumba ndogo yangu…”
Simu ya mama Pilima iliita, wifi yake Sonia akainuka kuangalia anayepiga…
“Wifi…” aliita kwa sauti…
“Bee…”
“Kaka anapiga,” alisema Sonia baada ya kuona jina la baba Pili kwenye skrini.
Mama Pilima alitoka mbio akijua kweli ni mume wake…
“Mh!” aliguna kwanza alipoona jina la baba Pili…
“Eee…niambie…” alisema huku akienda chumbani…
“Ndiyo nimefika salama bwana…wewe je? Ahaaa! Sawasawa…”
Wakati mama Pilima anaendelea kuongea kwa simu huku akiingia chumbani, wifi yake alishangaa kumwona kaka yake baba Pilima anaingia…
”Khaa! Sasa wifi anaongea na nani? Mbona kaka kafika yeye bado anaongea chumbani?” alijiuliza…
“Shikamoo kaka…”
“Marhaba za hapa?”
“Njema…pole na kazi…”
“Nimepoa.”
“Wifi yako yuko wapi?”
“Nadhani chumbani.”
Baba Pili alinyoosha chumbani. Mkewe, alipoona mlango unasukumwa, alikata simu kwani alijua anayeingia bila hodi chumbani kwake ni mume wake tu.
Baada ya salamu, mama Pilima alitoka sebuleni na simu, akakaa kwenye sofa na kuanza kuchati…
“Nimepanda sauti yako baba Pili…la! mama Pili anafaidi sana hiyo sauti. Sijui unaitoaga kila mahali…!”
“Teh! Teh! Wewe acha maneno…si wewe mwenyewe unaogopa kuifaidi,” alijibu baba Pili…
“Wala siogopi, mwenzi sijawahi kusaliti. Ni hilo tu…kama ingetokea siku moja nimewahi kufanya hivyo hapo sawa, ningekuwa na uzoefu,” alijibu mama Pilima.
Walichati mengi sana, walichati mpaka sasa ikawa mama Pili anaandaa chakula huku akiwa anachati, yaani na simu mkononi. Akawa anaonekana akicheka, mara akitabasamu, mara akionekana kukazia macho simu…
***
Siku iliyofuata, mama Pilima alikwenda kwenye shughuli zake, alipomaliza jioni akiwa anarudi nyumbani kwake, alimkumbuka baba Pili…
“Si ajabu hata leo yuko pale pa jana…ngoja nimpigie,” alisema moyoni huku akiweka simu sikioni…
“Niambie mama Pilima,” alipokea baba Pili…
“Wapi?”
“Pana jana…”
“Ah! Nakuja…niagizie nusu rosti na ndizi moja…nakuja,” alisema mama Pilima…
“Sawa mama Pilima.”
Baada ya nusu saa, mama Pilima aliwasili. Alipofika, alimsogelea baba Pili, akambusu…
“Mmmwaaa…mmwaaa.”
“Da! Asante sana mama Pilima, nimejihisi nipo peponi leo. Nakupenda sana,” alisema baba Pili…
“Nakupenda pia baba Pili,” alijibu mama Pilima huku akivuta kiti na kukaa.
Walianza kuongea, wakaongea sana mambo yao. Ilifika mahali baba Pili akaanza kukumbushia ya jana yake…
“Vipi mama Pilima, bado una msimamo uleule?” aliuliza baba Pili…
“Da! Baba Pili unajua nikwambie kutoka moyoni kwamba mimi sijawahi kusaliti hata siku hii…moja! Sasa leo hii nikisema nijaribu huoni kuwa, siku ikitokea umenimwaga nitaanza kutafuta wanaume wengine, mwisho wake nitakuwa malaya…”
“Mh! Mimi mpango wangu ni kukufanya uwe nyumba ndogo yangu,” alisema baba Pili, mama Pilima akacheka sana…
“Sasa niwe nyumba ndogo yako baba Pili si utakuwa unapata shida? Mimi najua nyumba ndogo lazima iwe free…ukitaka kwenda unakwenda muda wowote ule.”
“Hapana si lazima…unaweza kuwa mke wa mtu halafu bado ukawa nyumba ndogo yangu,” alifafanua baba Pili akionekana yuko siriasi kabisa na maneno yake…
Je, nini kiliendelea?
 
SEHEMU YA 05


“Sasa niwe nyumba ndogo yako baba Pili si utakuwa unapata shida? Mimi najua nyumba ndogo lazima iwe free…ukitaka kwenda unakwenda muda wowote ule.”
“Hapana si lazima…unaweza kuwa mke wa mtu halafu bado ukawa nyumba ndogo yangu,” alifafanua baba Pili akionekana yuko siriasi kabisa na maneno yake…
JIACHIE MWENYEWE…
“Mh! Mimi nadhani au napendekeza tuendelee kuwa kama hivi…marafiki wakubwa lakini wa siri…mume wangu baba Pilima asijue wala mke wako mama Pili asijue…tutafurahi sana,” alisema mama Pilima huku akionekana kuachia tabasamu la mbali sana.
Hapo bia zilikuwa zikimiminika mezani. Ilifika wakati walianza vituko wakiwa wamekaa, mama Pilima alimkanyaga baba Pili, naye baba Pili akamkanyaga mama Pilima, wakaangaliana, wakachekea ndani kwa ndani, mama Pilima akamsogelea baba Pili, akatoa ulimi kuelekea kwake, baba Pili akaudaka…
Waligugumia, mihemko ilitawala, baba Pili akapeleka mkono kwenye kifua cha mama Pilima maana eneo hilo la baa walilokaa lilikuwa halina watu hata kidogo.
Kumbe mkono wa baba Pili kwenye kifua cha mama Pilima ulifanikiwa kushika nido za mwanamke huyo, akashtuka kwa maumivu ya mahaba. Ilimpa picha baba Pili kwamba, udhaifu wa mapenzi wa mama Pilima upo kifuani, akautoa mkono maana alijua kweli si mahali pake, pale ni baa.
Mama Pilima kuona amegundulika udhaifu wake, naye akawa anautafuta udhaifu wa mwanaume huyo, akapeleka mkono kifuani na kuchezea ‘bustani’ ya hapo lakini baba Pilima wala!
Akautoa mkono hapo, akamshika shingoni, wala! Akaupeleka mkono mgongoni, wala! Akaushusha, baba Pilima akalainika sana lakini hakushtuka kama alivyoshtuka yeye mama Pilima alipoguswa nido.
Mama Pilima akajua kumbe udhaifu wa mwanaume huyo upo huko, akatoka na kushika glasi ya bia lakini hakuipeleka kinywani, aliendelea kubakiza ulimi wake ndani ya kinywa cha baba Pili huku akisikika kwa sauti ya…
“Mmm…mmm…mmm!”
Waliachana kwenye denda baada ya miguu ya mhudumu kutembea kuelekea walipokaa…
“Niongeze?” aliuliza mhudumu.
Mama Pilima alishika chupa ya bia ya baba Pili, akaitingisha, akaiweka chini, akashika ya kwake, akaitingisha, akaiweka chini…
“Ongeza kwa bili yangu tafadhali,” alisema.
Mhudumu alipoondoka tu, mama Pilima akaanza, akapeleka mkono kulekule alikogundua ndiko kwenye udhaifu wa baba Pili. Safari hii akaonesha hana mpango wa kuutoa haraka.
Huku akiangalia upande atakaotokea mhudumu, mama Pilima alifanya yake huku baba Pili akisinzia kwa starehe. Na vile alikuwa tayari yuko vizuri, looo!
Hali ya baba Pili ilimnasa hata mama Pilima mwenyewe aliyekuwa akisababisha. Naye akawa anaguna, anagugumia, anahemuka na anasinzia.
Kuna wakati wote walijikuta wamesinzia lakini mkono wa mama Pilima ukiwa bado kazini. Wakashtuka mhudumu alipoweka chupa za bia mezani kwa kuliza puu!
Mama Pilima ili asionekane alikuwa anafanya jambo baya, aliendelea kuuacha mkono kule…
“Fungua chapuchapu!” alisema.
Mhudumu alifungua, lakini alijua nini kilikuwa kinaendelea kwenye meza ile.
Baada ya mhudumu kuondoka, mama Pilima akakazana, baba Pili akahisi anaonewa, naye akarudia kwenye udhaifu wa mama Pilima. Sasa wakakaa kwa kuangaliana, mama Pilima kule, baba Pili pale. Walisisimka, wakashindwa kuvumilia hivyo, waliamua kuacha kwa mama Pilima kutoa kauli…
“Basi bwana! Tunakwenda kubaya,” alisema kwa sauti ya kukatakata ikitoka nje kwa njia ya puani.
Mama Pilima alivuta pumzi kwa nguvu, akazishusha huku akimwangalia baba Pili bila kusema lolote.
Baada ya hapo, waliendelea kunywa bila kusemezana, ilionekana kila mmoja alikuwa akiwaza yake moyoni kuhusu walikofikia awali.
Muda wa kufunga baa ulifika, mhudumu alikwenda kuchukua pesa yake, akalipwa! Wawili hao waliondoka huku wakiyumbayumba, wakashikana mikono ili kusaidiana kutembea.
Mama Pilima hakuwa na usafiri, baba Pili alikuwa nao, akampakia mwanamke huyo katika hali ya uleviulevi…
Baba Pili yeye ni mzima akiwa barabarani, aliendesha gari hadi Magomeni Kagera, akamshtua mama Pilima…
“Oho! Twende hadi mbele, kata kushoto, mbele utasimama. Baba Pili akafanya hivyo.
Walifika eneo la kusimama, gari likasimamishwa…
“Sasa?” aliuliza mama Pilima…
“Umefika bado?” aliuliza baba Pili…
“Nikishuka natembea kidogo mpaka kule mbele, lakini hapa panatosha,” alisema mama Pilima, wakaangaliana kwa muda mle ndani ya gari.
Wakasogeleana kama watu waliokuwa wakisikiliza maelekezo ya pamoja. Wakakutanisha midomo, wakaifungua, wakaanza kucheza na denda. Wakawa wanaguna ndani kwa ndani mpaka baba Pili akazima gari…
“Sogeza gari kwa pale mbele basi,” alisema mama Pilima kwa sauti ya kuchoka sana.
Baba Pilima akawasha tena gari, akalisogeza mpaka eneo aliloambiwa na mama Pilima…
“Hapa?”
“Yes! Hakuna mtu anayepita eneo hili muda huu,” alisema mama Pilima hali iliyomfanya baba Pili aamini kwamba huenda wanakwenda kutimiza ndoto yake…
“Egemea kiti,” alisema mama Pilima…
Je, unajua nini kilitokea hapo?
 
SEHEMU YA 06


“Yes! Hakuna mtu anayepita eneo hili muda huu,” alisema mama Pilima hali iliyomfanya baba Pili aamini kwamba huenda wanakwenda kutimiza ndoto yake…
“Egemea kiti,” alisema mama Pilima…
JIRUSHE MWENYEWE…
Baba Pili aliegemea kiti kwa haraka sana, akatumbua macho kusubiri hatua nyingine akiamini ataambiwa au ataelekezwa…
“Mmm! Baba Pili acha mi niende bwana. Muda umekwenda kwelikweli, si ajabu nyumbani wameanza kuingiwa na wasiwasi,” alisema mama Pilima akiwa tayari ameshika kitasa cha mlango ili kushuka…
“Kha! Yaani mbona haifanani?” alihoji baba Pili…
“Nini?”
“Kuniambia nilale mpaka kuaga kwamba unawahi nyumbani…”
“Teh! Teh! Ulidhani nini kitafuata baba Pili? Mbona mimi nimeshaongea mengi na wewe?” alisema mama Pili akiwa ameshafungua mlango wa gari na kushuka.
Mama Pilima alisimama mlangoni, akamwangalia baba Pili kwa sura yenye umakini wa hali ya juu…
“Bai baba Pili, usiku mwema, nafurahia kampani yako,” alisema mama Pilima akaanza kutembea.
Baba Pili akiwa bado ameegemea kiti, alishindwa kujifahamu. Kwa kutumia mwanga hafifu uliokuwa ukitoka kwenye taa za madukani, alimwangalia mama Pilima anavyotembea kuelekea mitaa ya kwake kisha akatingisha kichwa akisema…
“Da! Ameniweza kweli! Yaani kuegemea kiti na kuaga maana yake nini? Yule nadhani kuna kitu ameshtuka, si hivihivi tu.”
Aliwasha gari na kugeuza kurudi kwake.
***
Alipofika nyumbani kwake, mama Pilima alimtumia meseji baba Pili ya kumjulisha amefika salama na kumtakia usiku mwema…
“Nimefika baba Pili, usiku mwema kwako na kwa familia pia, tudumishe upendo wetu.”
“Mh!” aliguna baba Pili.
***
Kulikucha, mama Pilima alikwenda kwenye shughuli zake kama kawaida. Akiwa kwenye pilikapilika alishtuka maeneo f’lani, akaita…
“Baba Pili…baba Pili,” aligeuka mwanaume huyo, akamkazia macho mama Pilima, lakini hakuonesha kumchangamkia.
Mama Pilima alimsogelea huku akiachia tabasamu na kumkazia macho…
“Vipi? Uko sawa baba Pili?” alihoji mama Pilima baada ya kumwona mwanaume huyo akiwa hana uso wa bashasha. Yeye kwa akili zake aliamini hiyo ilisababishwa na kitendo alichomfanyia jana yake, cha kumlaza kwenye kiti cha gari kisha kumwacha…
“Niko sawa, sijakuelewa lakini,” alijibu mwanaume huyo…
“Utanielewa tu baba Pili. Unajua nilishakwambia mimi siwezi kusaliti. Kwa nini usinielewe jamani? Kwani tukiendelea kwa urafiki wetu kuna nini?” alisema mama Pili huku mwanaume huyo akiendelea kumkazia macho…
“Oke, basi tufanye hivi…leo tukutane hotelini, tupeane raha. Lakini iwe leo tu, tusirudie tena. Haya niambie tutakutana saa ngapi na wapi?” alisema mama Pilima na kuuliza swali.
Mwanaume huyo aliwaza sana, akamshangaa mama Pilima lakini hakutaka kumwambia jambo lolote. Ila alimtamani kwa namna mwanamke huyo alivyo mzuri wa umbo mpaka sura. Akaona ile ni bahati ya mtende kwake, kuota jangwani…
“Panga wewe,” alisema…
“Mimi napanga saa kumi, nitakuwa nimemaliza kazi zangu, lakini kuhusu hoteli gani, panga wewe sasa,” alisema mama Pilima.
“Nitakwambia, simu yangu ile nimeiacha, imeharibika kidogo, natumia nyingine hii na namba pia ni nyingine, nitajie upya namba zako,” alisema mwanaume huyo.
Mama Pilima alimtajia namba mwanaume huyo lakini huku akiona kama bado hajachangamka…
“Vipi jana ulifika salama? Nilikutumia meseji hukunijibu. Gari umepaki wapi?” mama Pilima aliuliza maswali mawili kwa mpigo…
“Si ndiyo maana nimekwambia simu ina matatizo kidogo, gari liko kule Mnazi Mmoja kwa mbele.”
Kidogo mwanaume huyo amuulize mama Pilima amsevu kwa jina gani, akashtuka…
“Basi baadaye.”
“Poa baba Pili, utanicheki. Lakini kama nilivyosema, iwe leo tu. Mara moja tu halafu basi, sawa baba Pili?”
“Sawa, nimekuelewa,” alijibu mwanaume huyo akianza kuondoka ili kukwepa maswali zaidi.
Mama Pili alikuwa na mawazo. Aliamini bado hajamridhisha mwanaume huyo kwani hata majibu yake yalionesha hivyo…
“Bado hayuko sawa. Kaniambia ‘basi baadaye’. Angekuwa sawa angeniambia ‘basi baadaye mama Pilima’. Nimemwambia atanicheki, akanijibu sawa, nimekuelewa’. Angekuwa sawa, angenijibu ‘sawa, nimekuelewa mama Pilima’. Nadhani hayupo sawa.”
***
Mbele ya safari, yule mwanaume alimuwaza mama Pilima…
“Kuna wanawake wameumbwa jamani! Yaani yule mwanamke ameumbwa! Nimepata bahati kubwa. Siwezi kumwacha hivihivi tu. Mi amenivutia yale macho yake bwana,” alisema moyoni mwanaume huyo.
***
Saa kumi juu ya alama, mama Pilima alipokea simu kwa namba asiyoijua, akajua ni baba Pili…
“Haloo…niambie baba Pili…wapi? Ooo…napajua…oke… we umeshafika? Haya nakuja sasa hivi mpenzi wangu…”



Itaendelea
 
SEHEMU YA 07

Saa kumi juu ya alama, mama Pilima alipokea simu kwa namba asiyoijua, akajua ni baba Pili…
“Haloo…niambie baba Pili…wapi? Ooo…napajua…oke… we umeshafika? Haya nakuja sasa hivi mpenzi wangu…”
BANJUKA NAYO MWENYEWE…
Mama Pilima alichukua usafiri mpaka kwenye hoteli aliyoelekezwa na mwanaume huyo. Akaingia ndani mpaka chumbani bila kupotea ambapo alimkuta mwenyeji wake amejaa tele japo alikuwa hajavua nguo kwa sababu machale yalimcheza…
“Unajua nini…saa zile nakuita pale nilijishtukia, nikasema ni mwenyewe kweli yule…si unajua tena kuonana kwetu ni usiku? Siku ya kwanza usiku, jana usiku, leo ndiyo nimekuona mchana,” alisema mama Pilima huku akikaa kitandani…
“Kweli kabisa…hata mimi mwenyewe sikukujua haraka…” alisema mwanaume huyo akiwa anafunga mlango kwa funguo yeye mwenyewe ili kama kuna mchezo unataka kuchezwa na mwanamke huyo audhibiti mara moja.
“Nilikuona…ulikuwa unanitafuta kwanza kichwani…unajua kukutana baa nako ni shida! Halafu hata sauti yako si ile ya baa…nadhani ile inakuwa ya pombe…kama jana tumezichapa sana,” alisema mama Pilima akiwa anaachia tabasamu…
“Sawa…loo!”
Walikaa kimya kwa muda wakiangaliana kisha mama Pilima akaachia tabasamu la mahaba, akamsogelea mwanaume huyo, akambusu, akamkumbatia, wakakumbatiana. Wakaenda kitandani, puu!
“Baba Pili,” aliita mama Pilima kwa sauti ya chini sana…
“Niambie mpenzi wangu,” alisema mwanaume huyo.
Hapohapo mama Pilima akajiuliza tena ni kwa nini mwanaume huyo hataki kutumia jina la mama Pilima kama alivyozea siku mbili za nyuma?
“Si leo tu lakini?” aliuliza mama Pilima, akimaanisha kwamba, baada ya siku hiyo wasipeane raha tena!
“Sawa, leo tu. Lakini si itategemea?”
Walicheka wote, wakaanza kuhamasishana kwa kushikana sehemu mbalimbali za mwili.
Mara, simu ya mama Pilima iliita lakini ilionekana huyo mtu aliyepiga kama alibip! Kwa hiyo hakuiendekeza, akaendelea na raha zake kitandani.
Walifika mahali wakachojoana ili safari iendelee. Mama Pilima akawa analalamika kwamba ni mara yake ya kwanza kuchepuka…
“Yaani mi leo jamani…yaani sijui itakuaje? Yaani wewe,” alisemasema mama Pilima.
Kazi ikaanza, shughuli ikapamba moto, safari ikakolea, mechi ikachezwa kwenye uwanja binafsi.
Mama Pilima akajikuta akiachana na kulalamikia kuchepuka, akaanza kusikilizia uhodari wa mwanaume huyo na kuzianzisha zile kelele zenyewe sasa.
Ilikuwa fujo, balaa na hekaheka. Ilibidi mwanaume huyo kumziba kinywa mama Pilima ili kelele zake zisiwafaidishe wapangaji wa kwenye vyumba vingine.
Shughuli ilipomalizika, walitulia, wakawa wanahema kwa kasi huku wakipongezana wenyewe kwa wenyewe…
“Hivi baba Pili, tutaweza kweli?” alisema mama Pilima…
“Kuhusu nini?”
“Kwamba baada ya leo na iwe basi?”
“Mh! We unasemaje kwani?”
“Mh! Ngoja tuangalie maana naona umenipa kitu kigeni sana mwilini mwangu. Leo nimesikia kama nabembea kwenye kamba iliyo chini ya mtu mkubwa wenye kutoa kivuli na upepo mwanana toka pwani,” alisema mama Pilima huku akitoka kitandani kuifuata simu yake ambayo ilikazana kuita…
“Sijui atakuwa nani? Labda mume wangu,” alisema kwa sauti mwanamke huyo huku akiishika simu hiyo.
“Hee! Mbona sielewi,” alishtuka. Ni baada ya kuona kwenye skrini jina Baba Pili ambaye yeye aliamini yupo kitandani, akaipokea huku akimwangalia kwa wasiwasi mwanaume huyo kitandani…
“Haloo…”
“Haloo, mama Pilima, mzima?”
“Mi…mzima…hebu subiri na…nakupigia,” alisema mama Pilima na kukata simu, akarudi kitandani…
“Hebu niambie ukweli…wewe siyo baba Pili?” aliuliza mama Pilima huku akionekana kuwa na sura iliyojaa hofu…
“Ni kweli,” alisema mwanaume huyo.
“Imekuaje ukanidanganya sasa?”
“Sijakudanganya, ila wewe uliingia kichwakichwa kwangu. Mimi si baba Pili,” alisema mwanaume huyo kwa sauti yenye unyenyekevu wa hali ya juu.
Mama Pilima alichuruzisha machozi, akajiinamia. Akamwangalia mwanaume huyo kwa macho yaliyojaa aibu akiwaza…
“Sasa huyu si amenielewa kuwa mimi ni mwanamke malaya. Lakini ni kwa nini nilimfananisha na baba Pili?”
“Usiumie mpenzi…tunaweza kuendelea na uhusiano…mimi nimekukubali sana. Hata muda ule unaniita, niliamua kuendelea kusimama na kuongea na wewe kwa sababu nilikupenda ghafla palepale, nikaona nimepata bahati ya mtende kuota jangwani,” alisema mwanaume huyo.
Mama Pilima alimwangalia weee, lakini moyoni akakubali kwamba, ni mwanaume mzuri kwake na amemtendea haki. Ina maana akiamua kusema basi, halafu akaendelea na baba Pili atakuwa ameanza tabia ya kurukaruka…
“Kwani wewe kwa jina la mtoto wako yeyote yule unaitwa baba nani?” mama Pilima alimuuliza mwanaume huyo huku akimwangalia kwa macho yaliyojaa mahaba mazito…
“Naitwa baba P.”
Je, unajua nini kilitokea hapo?
 
SEHEMU YA 08

Ina maana akiamua kusema basi, halafu akaendelea na baba Pili atakuwa ameanza tabia ya kurukaruka…
“Kwani wewe kwa jina la mtoto wako yeyote yule unaitwa baba nani?” mama Pilima alimuuliza mwanaume huyo huku akimwangalia kwa macho yaliyojaa mahaba mazito…
“Naitwa baba P.”

TAMBAA NAYO…
“He! Baba P! P ni kifupi au ndiyo jina lote?”
“Kifupi.”
“Kirefu chake?”
“Pilima. Kwa hiyo mimi unaweza kuniita baba Pilima.”
Mama Pilima alicheka sana, akasimama akiendelea kucheka na kusema…
“Haya ni maajabu makubwa kwangu…”
“Kwa nini?”
“Na mimi ni mama Pilima, nina mtoto anaitwa Pilima.”
“Hakuna kitu kama hicho.”
“Kweli kabisa, mtoto wangu anaitwa Pilima.”
“Kwa hiyo mimi mama Pilima, wewe baba Pilima?”
“Ndiyo maana yake.”
Mama Pilima alisahau yote yaliyopita. Alisahau alivyotendwa na mwanaume huyo! Moyoni alisema…
“Kwa hiyo sasa nina baba Pili, baba Pilima feki na baba Pilima orijino yule wa nyumbani.”
***
Uhusiano kati ya mama Pilima na baba Pilima ulipamba moto na kumsahau baba Pili kwa muda. Aliamua kumsahau baba Pili kwa sababu ya kukwepa kukutana naye kimwili wakati ameshajitolea kwa baba Pilima. Angekuwa mwanamke wa ajabu, wanaume watatu kwa wakati mmoja!
Kwa hiyo ikawa kila baba Pili alipompigia simu wakutane, mama Pilima alitoa sababu ya uongo ili kusogeza siku mbele.
Katika kipindi cha wiki mbili, akawa ameshakutana kimapenzi mara mbili na baba Pilima na alikolea kwelikweli. Wao sasa ndiyo walikuwa wakikaa kila jioni kwenye baa nyingine aliyoijua baba Pilima.
Mazungumzo yao walipokaa, mama Pilima alifurahia sana kumwita mwanaume huyo baba Pilima akijisikia kama anamuita mume wake nyumbani…
“Baba Pilima…”
“Niambie mama Pilima…”
“Hivi mapenzi yetu yatadumu kweli baba Pilima?”
“Kwa nini yasidumu mama Pilima, tatizo liko wapi kwani?”
“Sijaona tatizo, bali kama nilivyokwambia, sijazoea kusaliti na nimeshakusimulia mkasa mzima mpaka nilipokutana na wewe.”
“Mimi siwezi kuachana na wewe mama Pilima, kuwa na amani tu.”
Kuna siku, mama Pilima na baba Pilima wakiwa kwenye baa hiyo, mhudumu alijua ni wapenzi kutokana na mikao, kwani uzoefu wake, wanandoa hawakai kihasarahasara, lakini alikuja kushangaa, kumsikia mama Pilima akimuuliza baba Pilima…
“Eti baba Pilima, kwa nini usinywe pombe kali ukaachana na bia?”
“Mama Pilima, pombe kali zinataka watu wanene sana, mimi umbo langu si unaliona?”
“Mh! Kumbe hawa ni mke na mume? Mbona wako kama mtu na hawara yake?” alijiuliza mhudumu huyo baada ya kuwasikia wakiitana majina ya watoto wao.
***
Siku hiyo, akiwa nyumbani, sebuleni na mume wake, mama Pilima alijisahau katika mazungumzo…
“Baba Pilima…eee! Eti baba Pilima,” alikosea mama Pilima, akashtuka, lakini akaendelea kuita jina hilohilo bila mumewe kujua kwamba, hakumaanishwa yeye.
Usiku wa siku hiyo, wakiwa wamelala, baba Pilima alitaka haki yake, akafurukuta akafanikiwa. Lakini wakati mpambano ukiendelea, mama Pilima aliingiza mazoea yaleyale, alimwita mumewe kimahaba…
“Baba Pilima,” lakini alimaanisha yule feki…
“Niambie mke wangu,” aliitika kibabebabe baba Pilima bila kujua kuwa, hakukusudiwa yeye.
***
Ilikuwa Jumapili, mama Pilima alikuwa akijiandaa kwenda kanisani, simu yake ilikuwa mezani sebuleni. Baba Pilima alikuwa hajaamka. Wifi wa mama Pilima alishajiandaa kwa safari ya kanisani, kwa hiyo alikuwa akimsubiri yeye tu. Mara simu ya mama Pilima iliita, wifi yake akaitupia macho…
“Wifi kaka anapiga simu?” alisema wifi mtu huyo baada ya kuona Baba Pilima kwenye skrini ya simu.
Mama Pilima alikwenda mbio…
“Anapigaje wakati bado nipo humuhumu ndani?” aliuliza mama Pilima, akiamini ni kweli mume wake amepiga…
“Ooo! Kumbe huyu!” alisema mama Pilima, wifi yake akachezwa na machale. Kwamba, kwa nini mama Pilima aseme ‘ooo… kumbe huyu’.
Hata hivyo, mama Pilima hakupokea simu hiyo, akaikata na kutuma meseji…
“Ina maana si kaka aliyepiga?” aliuliza wifi huyo…
“Ngoja nitakwambia,” alisema mama Pilima akiwa na uso uliochunwa kwa kukosa aibu. Alijua nini ni nini!
“Mh!” aliguna wifi mtu huyo, lakini akaachana na maswali zaidi.
Ghafla, baba Pilima akatokea kutoka chumbani akiwa ndani ya nguo za kulalia…
“Mbona kama nasikia mimi nimempigia simu mama Pilima wakati sijashika simu yangu tangu kumekucha. Au sijasikia sawasawa?” alihoji baba Pilima huku akipiga miayo.
Je, unajua nini kilitokea hapo?
 
SEHEMU YA 09



Ghafla, baba Pilima akatokea kutoka chumbani akiwa ndani ya nguo za kulalia…
“Mbona kama nasikia mimi nimempigia simu mama Pilima wakati sijashika simu yangu tangu kumekucha. Au sijasikia sawasawa?” alihoji baba Pilima huku akipiga miayo.
JIACHIE MWENYEWE…
“Nilidhani umepiga kwenye simu ya wifi,” alisema dada yake huyo.
Baba Pilima aliporudi chumbani, mama Pilima alikaa sebuleni na wifi yake, wifi akaanza kusema…
“Wifi, huyo uliyemsevu kwa jina la baba Pilima kwenye simu yako ni nani? Maana simu ilipoita nikajua ni kaka, ndiyo maana nikakwambia kaka anapiga. Lakini pia nilishangaa kwa nini kaka apige wakati yumo humuhumu ndani?”
“Wifi yule anaitwa mama Sakina, anakaa mtaa wa mwisho kule. Siku namsevu sijui ilikuaje, nikaandika jina la kaka yako, lakini sikulifuta, tena ngoja nimpigie,” alisema mama Pilima huku akishika simu, akaiweka sikioni, baada ya muda akaongea…
“Ee mama Sakina…naona ulinipigia…aaa! oke…sawasawa…saa ngapi…oke sawa,” akakata simu na kumgeukia wifi yake…
“Kumbe alitaka niende nyumbani kwake, ana vitenge vizuri kutoka Zaire,” alisema mama Pilima. Lakini ukweli ni kwamba, hakupiga simu kwa mtu yeyote yule, achilia mbali mama Sakina…
“Oke, na siku ile ulipiga simu ikasomeka jina la baba Pili naye ni nani wifi?” wifi mtu huyo aliuliza tena.
Mama Pilima alianza kuhisi wifi yake huyo ana lake moyoni…
“Haiwezekani aniulize maswali kama yeye ndiyo kanioa?” alijisemea moyoni…
“Wifi, mbona unanichunga sana, kwani nimekufanyia kosa gani? Unaniuliza maswali kama wewe ndiyo baba Pilima bwana…aaah! wifi haifai hivyo,” alilalamika mama Pilima.
Ilibidi wifi yake awe mpole…
“Basi yaishe wifi.”
Lakini moyoni, wifi mtu huyo alikuwa ana maswali kibao kuhusu majina yale, hakukubali kama baba Pilima ni mama Sakina. Pia alitia shaka kwa baba Pili…
“Huyu wifi ameanza michepuko,” alisema moyoni wifi mtu huyo.
Walikwenda kanisani, walisali, wakatoka kurudi nyumbani. Wakiwa njiani, mama Pilima alipokea simu, wifi yake akawa makini kumsikiliza…
“Eee…mzima sijui wewe..? Hawajambo akina Pilima..?” hii hawajambo akina Pilima, wifi mtu huyo alijisahau, akashtuka sana na kukata simu kisha akatuma meseji…
“Tuchati, niko na wifi yangu.”
Wifi naye alishtuka kusikia ‘hawajambo akina Pilima’…
“Kumbe..! Kumbe kuna mtu anaitwa baba Pilima. Ndiyo nimejua sasa,” alisema moyoni wifi huyo.
“Nilitaka kujua kama leo unaweza kuwa free kidogo,” aliuliza baba Pilima feki.
“Natoka kanisani. Labda baadaye. Ulitakaje kwani?”
“Nilitaka tuonane mahali…”
“Kuonana kwa kuzungumza au zaidi ya kuzungumza?”
“Zaidi ya kuzungumza.”
“Mh! Baba Pilima bwana. Nitaachika mwenzako ujue.”
“Hamna bwana! Nimekumisi sana ujue. Da!”
“Mmh! Si jana tu tulikuwa wote my darling?”
“Si ndiyo maana ya kukumisi jamani! Hata kama tulikuwa wote lakini kila nikikukumbuka bado napenda tuwe wote.”
Mama Pilima alijikuta akiachia tabasamu la ndani kwa ndani ili wifi yake asijue.
“Basi mchanamchana nitakwambia.”
“Poapoa baby wangu.”
Baada ya muda, meseji iliingia kwenye simu ya mama Pilima ikiwa inatokea kwa baba Pili sasa…
“Upo?”
Mama Pilima baada ya kuisoma, hakuona sababu ya kutomjibu kama ilivyokuwa siku kadhaa nyuma…
“Nipo…wewe je?”
“Mimi nipo, hatuonani?”
“Ubize kidogo, lakini tutaonana tu, usijali,” alijibu mama Pilima huku moyoni akisema…
“Tatizo si kuonana, bali umeshawahiwa na mwenzako baba Pilima.”
***
Saa kumi jioni, mama Pilima alijipara tayari kwa kutoka. Ni baada ya mumewe kuondoka. Akabaki wifi mtu bado akiwa na mawazo kibao kuhusu mama Pilima.
Alipotoka tu mama Pilima, alimtumia meseji baba Pilima feki…
“Mimi ndiyo natoka nyumbani sasa, tunakutana wapi?”
“Njoo mpaka pale pa jana.”
“Oke.”
Mama Pilima alitembea hadi kituoni ili kuchukua Bajaj. Lakini ile anafika tu, gari dogo jeupe lilisimama mbele yake na kupiga honi mfululizo. Vioo vilikuwa na tinted kwa hiyo hakumwona dereva ndani.
Honi iliendelea kupigwa kisha kioo cha upande wa abiria kikafunguliwa nusu, dereva akaongea na mtu mmoja aliyesimama kituoni hapo akisubiri usafiri wa daladala. Kisha yule mtu akamgeukia mama Pilima aliyekuwa amesimama pembeni…
“Anti unaitwa kwenye gari,” alisema yule abiria.
“Na nani?”
“Eti anakuuliza wewe nani?” aliuliza yule abiria akiwa ameinama kidogo ili amuone vizuri yule abiria…
“Anasema anaitwa baba Pili,” yule abiria alimwambia mama Pilima.
Mama Pilima akatembea kwa kasi hadi mlangoni mwa gari…
“Mzima baba Pili?”
“Mzima, twende nikupe lifti.”
Je, unajua nini kilitokea hapo?
 
SEHEMU YA 09



“Eti anakuuliza wewe nani?” aliuliza yule abiria akiwa ameinama kidogo ili amuone vizuri yule abiria…
“Anasema anaitwa baba Pili,” yule abiria alimwambia mama Pilima.
Mama Pilima akatembea kwa kasi hadi mlangoni mwa gari…
“Mzima baba Pili?”
“Mzima, twende nikupe lifti.”
SHUKA NAYO MWENYEWE SASA…
Mama Pilima alijikuta akizama ndani ya gari hilo huku akisema…
“Kwani we unakwenda wapi?”
“Mbelembele kule…wewe unakwenda wapi?” alisema baba Pili…
“Nakwenda mahali mara moja.”
“Kufanya nini mama Pilima?”
“Kumwona mama mmoja hivi ni rafiki yangu, nimemmisi sana, nikasema leo niende…”
“Mh!”
“Mbona umeguna baba Pili?”
“Kumwona mama mmoja hivi…”
“Kwani uongo?”
“Wewe ndiyo unayejua…nakusikiliza zaidi wewe.”
“Ndiyo hivyo, labda kama huamini.”
“Nusu naamini.”
“Kwa nini?”
“Kwa vile umesema wewe… lakini mama Pilima ni kwa nini hutaki kuonana na mimi ghafla tu?” aliuliza baba Pilima huku akimkazia macho mwanamke huyo…
“Siyo sitaki bwana…mambo yanaingiliana kidogo,” alijitetea mama Pilima huku macho yakiangalia nje…
“Ndiyo unikache mpenzi wangu? Ilifika mahali nilijiuliza labda kuna kosa mahali.”
“Hamna kosa.”
“Kama kweli hamna kosa, basi tukakae mahali tuzungumze. Huyo mama najua unaweza kumwambia umebanwa, utaonana naye hata kesho.”
Mama Pilima aliguna, akaachia tabasamu huku moyoni akisema…
“Da! Nimebanwa. Ningejua ningetoa sababu nyingine kabisa kuliko kumwambia kuna mtu nimemmisi.”
“Wapi?” aliuliza mama Pilima…
“Popote pale. Lakini penye utulivu wa hali ya juu.”
“Oke, twende.”
Baba Pili aliendesha gari mpaka kwenye baa moja iliyopo kwenye hoteli maarufu, wakashuka hapo…
“Hapa naamini pana utulivu wa hali ya juu,” alisema baba Pili akiwa amemshika mkono mwanamke huyo.
Ilikuwa baa yenye utulivu wa hali ya juu. Wateja wengi walionekana si wale wa fujofujo. Wale waliokuwa na wenza wao, walikuwa wameinamiana wakizungumza kwa karibu ili mazungumzo yao yasisikike kwa wengine.
Baba Pili na mama Pilima walikwenda kukaa kwenye kona moja karibu na ukuta ambapo isingekuwa rahisi mtu aliyekuwa akiingia kuwaona…
“Hapa panafaa,” alisema mama Pilima huku akivuta kiti na kukaa. Wakati wakiingia, baadhi ya wateja, wake kwa waume walimtupia macho mama Pilima kwa jinsi umbo lake lilivyokuwa na mvuto. Wenyewe wanaita figa namba 8!
Wengine waliokuwa wakimtumbulia macho ni wanawake wenzake. Hali hiyo ilimfanya baba Pili azidi kuumia akiamini alifanya makosa makubwa sana kumwacha mwanamke huyo kwa zile siku za mwanzomwanzo…
“Nikimkosa leo, nitajilaumu sana. yaani huu mzigo wote niushindwe mimi kweli? Haiwezekani,” alisema moyoni baba Pili. Hapo sasa wameshakaa.
Walianza kunywa huku wakizungumza kwa kufuata mazingira waliyoyakuta. Maongezi yao ni kwa chini sana…
“Lakini mama Pilima, wewe ulijua wazi kwamba nakupenda sana. kwa nini sasa unitende vile? Yaani ni kama ulinionjesha mahaba yako kisha ukaingia mitini. Umekuwa ukinisababishia kukosa usingizi kiasi kwamba, najuta kukufahamu. Hata pale baa ilibidi niache kwenda, maana ningekuwa nakukumbuka wewe,” alisema baba Pili huku macho yake ya kiume yakikumbana na macho ya kulegea ya mama Pilima hali iliyozidi kumpa hamasa ya mahaba mwanaume huyo…
“Eee! Unajua kusema ule ukweli ni kama nilivyokwambia awali…kuna mambo yaliingilia kati mpaka nikawa siwezi tena kukaa baa jioni, nikitoka kwenye shughuli zangu ni nyumbani tu…”
“Sasa hayo mambo yameisha?” aliuliza baba Pili…
“Kwa mbali saana.”
Mara, mama Pili aliomba kwenda chooni, akavuta simu yake na kuiweka jirani na simu ya baba Pili, akaenda.
Huku nyuma, baba Pilima feki akapiga simu ili kujua mwanamke huyo amefikia wapi! Baba Pili alipoitumbulia macho, moyo ukamlipuka…lip!
“Da! Noma, mzee anapiga,” alisema mwenyewe huku akiangalia mlango wa chooni. Aliishika simu na kuigeuzageuza mpaka mama Pilima alipotoka. Baba Pili aliinua mkono juu kuashiria kwamba, simu yake inaita.
Mama Pilima alitembea kwa kasi mpaka pale…
“Ni nani?” aliuliza.
“Mista,” alisema baba Pili.
Mama Pilima alipoangalia jina, akajua ni baba Pilima feki kwani mumewe amemsevu kwa jina la My Husband!!
“Mbona hupokei?” aliuliza baba Pili…
“Ah! Achana naye huyu, tuendelee na yetu,” alijibu mama Pilima…
“Yetu ninayotaka kuendelea na wewe ni kukuomba twende tukachukue chumba hotelini japo kwa leo tu, naami nitafurahi sana kama utanikubalia.”
Je, unajua nini kilitokea hapo?
 
SEHEMU YA 10



“Eti anakuuliza wewe nani?” aliuliza yule abiria akiwa ameinama kidogo ili amuone vizuri yule abiria…
“Anasema anaitwa baba Pili,” yule abiria alimwambia mama Pilima.
Mama Pilima akatembea kwa kasi hadi mlangoni mwa gari…
“Mzima baba Pili?”
“Mzima, twende nikupe lifti.”
SHUKA NAYO MWENYEWE SASA…
Mama Pilima alijikuta akizama ndani ya gari hilo huku akisema…
“Kwani we unakwenda wapi?”
“Mbelembele kule…wewe unakwenda wapi?” alisema baba Pili…
“Nakwenda mahali mara moja.”
“Kufanya nini mama Pilima?”
“Kumwona mama mmoja hivi ni rafiki yangu, nimemmisi sana, nikasema leo niende…”
“Mh!”
“Mbona umeguna baba Pili?”
“Kumwona mama mmoja hivi…”
“Kwani uongo?”
“Wewe ndiyo unayejua…nakusikiliza zaidi wewe.”
“Ndiyo hivyo, labda kama huamini.”
“Nusu naamini.”
“Kwa nini?”
“Kwa vile umesema wewe… lakini mama Pilima ni kwa nini hutaki kuonana na mimi ghafla tu?” aliuliza baba Pilima huku akimkazia macho mwanamke huyo…
“Siyo sitaki bwana…mambo yanaingiliana kidogo,” alijitetea mama Pilima huku macho yakiangalia nje…
“Ndiyo unikache mpenzi wangu? Ilifika mahali nilijiuliza labda kuna kosa mahali.”
“Hamna kosa.”
“Kama kweli hamna kosa, basi tukakae mahali tuzungumze. Huyo mama najua unaweza kumwambia umebanwa, utaonana naye hata kesho.”
Mama Pilima aliguna, akaachia tabasamu huku moyoni akisema…
“Da! Nimebanwa. Ningejua ningetoa sababu nyingine kabisa kuliko kumwambia kuna mtu nimemmisi.”
“Wapi?” aliuliza mama Pilima…
“Popote pale. Lakini penye utulivu wa hali ya juu.”
“Oke, twende.”
Baba Pili aliendesha gari mpaka kwenye baa moja iliyopo kwenye hoteli maarufu, wakashuka hapo…
“Hapa naamini pana utulivu wa hali ya juu,” alisema baba Pili akiwa amemshika mkono mwanamke huyo.
Ilikuwa baa yenye utulivu wa hali ya juu. Wateja wengi walionekana si wale wa fujofujo. Wale waliokuwa na wenza wao, walikuwa wameinamiana wakizungumza kwa karibu ili mazungumzo yao yasisikike kwa wengine.
Baba Pili na mama Pilima walikwenda kukaa kwenye kona moja karibu na ukuta ambapo isingekuwa rahisi mtu aliyekuwa akiingia kuwaona…
“Hapa panafaa,” alisema mama Pilima huku akivuta kiti na kukaa. Wakati wakiingia, baadhi ya wateja, wake kwa waume walimtupia macho mama Pilima kwa jinsi umbo lake lilivyokuwa na mvuto. Wenyewe wanaita figa namba 8!
Wengine waliokuwa wakimtumbulia macho ni wanawake wenzake. Hali hiyo ilimfanya baba Pili azidi kuumia akiamini alifanya makosa makubwa sana kumwacha mwanamke huyo kwa zile siku za mwanzomwanzo…
“Nikimkosa leo, nitajilaumu sana. yaani huu mzigo wote niushindwe mimi kweli? Haiwezekani,” alisema moyoni baba Pili. Hapo sasa wameshakaa.
Walianza kunywa huku wakizungumza kwa kufuata mazingira waliyoyakuta. Maongezi yao ni kwa chini sana…
“Lakini mama Pilima, wewe ulijua wazi kwamba nakupenda sana. kwa nini sasa unitende vile? Yaani ni kama ulinionjesha mahaba yako kisha ukaingia mitini. Umekuwa ukinisababishia kukosa usingizi kiasi kwamba, najuta kukufahamu. Hata pale baa ilibidi niache kwenda, maana ningekuwa nakukumbuka wewe,” alisema baba Pili huku macho yake ya kiume yakikumbana na macho ya kulegea ya mama Pilima hali iliyozidi kumpa hamasa ya mahaba mwanaume huyo…
“Eee! Unajua kusema ule ukweli ni kama nilivyokwambia awali…kuna mambo yaliingilia kati mpaka nikawa siwezi tena kukaa baa jioni, nikitoka kwenye shughuli zangu ni nyumbani tu…”
“Sasa hayo mambo yameisha?” aliuliza baba Pili…
“Kwa mbali saana.”
Mara, mama Pili aliomba kwenda chooni, akavuta simu yake na kuiweka jirani na simu ya baba Pili, akaenda.
Huku nyuma, baba Pilima feki akapiga simu ili kujua mwanamke huyo amefikia wapi! Baba Pili alipoitumbulia macho, moyo ukamlipuka…lip!
“Da! Noma, mzee anapiga,” alisema mwenyewe huku akiangalia mlango wa chooni. Aliishika simu na kuigeuzageuza mpaka mama Pilima alipotoka. Baba Pili aliinua mkono juu kuashiria kwamba, simu yake inaita.
Mama Pilima alitembea kwa kasi mpaka pale…
“Ni nani?” aliuliza.
“Mista,” alisema baba Pili.
Mama Pilima alipoangalia jina, akajua ni baba Pilima feki kwani mumewe amemsevu kwa jina la My Husband!!
“Mbona hupokei?” aliuliza baba Pili…
“Ah! Achana naye huyu, tuendelee na yetu,” alijibu mama Pilima…
“Yetu ninayotaka kuendelea na wewe ni kukuomba twende tukachukue chumba hotelini japo kwa leo tu, naami nitafurahi sana kama utanikubalia.”
Je, unajua nini kilitokea hapo?
 
SEHEMU YA 11


“Yetu ninayotaka kuendelea na wewe ni kukuomba twende tukachukue chumba hotelini japo kwa leo tu, naami nitafurahi sana kama utanikubalia.”
SHUKA NAYO SASA…
Mama Pilima alishtuka kwanza, akamtumbulia macho baba Pili kisha akaachia tabasamu laini…
“Unajua unaniingiza kwenye majaribu makubwa sana?”
“Najua…lakini sina jinsi mama Pilima…unajua ninavyokupenda sana.”
“Najua…lakini kupenda huko kuendane na utayari wa kila mmoja wetu.”
“Kama mimi niko tayari,” alisema baba Pili…
“Hata mimi niko tayari ila kwenye eneo moja la kukutana kitandani nadhani ndilo kizingiti kwangu,” alisema mama Pilima.Moyoni alitamani sana kumridhisha mwanaume huyo kwani kusema ukweli alimpenda lakini sasa alishazidiwa kete na baba Pilima feki kiasi kwamba alijiona kama atakubali angeanza tabia mbaya ya uhuni kama si umalaya…
“Tulishaongea mimi na wewe ukasema kwamba, itakuwa mara moja tu na si vinginevyo. Sasa ninacholilia kutoka kwako mpaka sasa ni hiyo mara moja tu mpenzi wangu,” alisema baba Pili kwa sauti iliyojaa utulivu wa hali ya juu.
Palipita utulivu wa kama sekunde kumi nzima, mama Pilima alikuwa akimwangalia baba Pili kwa macho yaliyojaa kujiuliza na ugumu wa kutatua ya moyoni…
“Baba Pili,” aliita mama Pilima kwa sauti iliyojaa mahaba…
“Nakusikiliza…”
“Uko tayari kwa leo tu lakini?”
“Niko tayari hata kwa sekunde kumi tu,” alisema baba Pili, mama Pilima akacheka…
“Sekunde kumi!? Sekunde kumi umekuwa nanihii…”
Walicheka wote, mama Pilima akawahi kumaliza…
“Eee! Basi sawa baba Pili, hata mimi ni binadamu kama wewe. Kwa jinsi unavyolalamika sina namna. Uwezo wa kukufurahisha ninao, sababu ninazo na nia pia imebidi niwe nayo,” alimaliza mama Pilima.
Palepale baba Pili alisimama, akaenda upande wa mapokezi wa hoteli hiyo, akachukua chumba. Baada ya dakika tano tu akarudi, akamwinua mama Pilima. Wakaenda…
“Karibu sana chumbani,” alisema baba Pili huku akiwa amemshika mkono mwanamke huyo.
Walifikia kukaa, baba Pili hakuwa akiamini kama kweli mama Pilima yu mikononi mwake muda huo. Waliangaliana, mama Pilima akakimbiza macho kwa aibu ya kianamke.
“Mama Pilima,” aliita baba Pili…
“Abee,” mama Pilima aliitikia kwa kandokando…
“Eee! Usingenitendea haki kama usingenikubalia na zoezi hili linaloendelea,” alisema baba Pili kwa ile sauti yake ya upole na unyenyekevu.
Mama Pilima akaachia tabasamu na kumkumbatia baba Pili, akauweka uso wake sawa, akatoa ulimi lakini hakuupeleka kwa baba Pili akitaka amwone kama yeye mwenyewe ataupokea au la! Baba Pili naye hakuona sababu ya kuuchuna, alipeleka midomo mbele na kuupokea.
Walizama ndani ya denda la kiutuuzima huku wakisikika kuhema kwao tu.
Ghafla, baba Pili akajisindikizia na mkono kwa kumshika kifuani mwanamke huyo huku akikipapasa kifua hicho laini.
Mama Pilima alianza kutoa ishara kwamba anakoelekea siyo kuzuri hivyo baba Pili ajue hilo mapema. Kuhema kulikuwa kwa wingi sasa, macho yalikosa nguvu na kuona mazingira ya chumba kwa hafifu.
Hilo alipolibaini baba Pilima alizidisha ujuzi, alitoka kwenye kitanda na kupiga magoti kisha akaendelea na kuufanyia utalii mwili wa mama Pilima huku akimsifia kwa sifa mbalimbali za uumbwaji.
Mama Pilima hoi, hakuweza kusema wala kuangalia. Hakuwa amefumbua macho kumwangalia baba Pili. Mwili ulimuisha nguvu.
Baba Pili hakuona sababu ya kuwahi kuanzisha mechi, alizidi kumtesa mwanamke huyo kwa kumchezea mwili mzima, wakati fulani mpaka kwenye nyayo.
Mama Pilima alipoona hali inazidi kuwa mbaya aliamua kumvutia kwake baba Pili kama ishara kwamba mwili umeshapata moto tayari kwa mpira.
Mchezo ulianza bila mwamuzi, wawili hao waliingia uwanjani na kutikisa nyasi huku chumba kikirudisha utulivu wa hali ya juu.
Mama Pilima alianza kuweweseka, akapagawa, akapiga kelele zote huku akimwaga sifa kemkemu kama siyo nyingi. Ilifika mahali ilibidi atubu kwa mwanaume huyo kwamba, hatakubali siku ile iwe ndiyo ya kwanza na ya mwisho…
“Au we bado unataka leo ndiyo iwe siku ya kwanza na ya mwisho?” mama Pilima alisema kwa shidashida…
“Sawa…yaani nashukuru sana kwa kubadili msimamo wako wa awali,” baba Pili alishadadia kwa sauti ya kiume.
Walikaa kimya, sasa ikawa gwaride kwelikweli. Kwa vile baba Pilima alishajua ishu ya mama Pilima kuhusu ndoa yake, alitumia muda huo kuhakikisha hafanyi kosa lolote katika siku hiyo ya kwanza.
“Baba Pili… uwe basi baba Pilima moja kwa moja,” alisema mama Pilima akiwa na maana yake.
Baba Pili alikubali, akaitikia kwa kichwa huku akihema sana.
Ghafla, mama Pilima alimsukuma baba Pili, kule mpaka akaanguka chini!
Je, unajua nini kilitokea hapo?
 
SEHEMU YA 12


“Haitatokea baby. Unajua baby mtu ukitoka kufanya mambo kama haya halafu ukaongea kwa simu mtu anaweza kujua, maana kuhema kunakuwa kwingi ndiyo maana sitaki kupokea,” alisema mama Pilima, baba Pili akawa amemuelewa.
“Oke, nimekuelewa mama Pilima, lakini kuna jambo ambalo nataka kuzungumza na wewe kidogo,” alisema baba Pili…
SHUKA NAYO MWENYEWE SASA…
“Liseme tu baba Pili mimi niko tayari kukusikiliza…”
“Unajua mimi nafahamu ni kwa nini wewe ulikuwa hupokei simu wala hutaki mawasiliano na mimi…”
“Kama kweli ulikuwa unafahamu niambie ni kwa nini?”
“Ulibanwa mama Pilima…”
“Ndiyo nilibanwa, si nilikwambia lakini…hilo ndilo unalolifahamu?”
“Liko zaidi mama Pilima, ila oke…sasa siku nyingine uwe makini sana…”
“Na nini baba Pili..?”
“Unajua mimi ni baba Pili…”
“Najua baba Pili kuwa wewe ni baba Pili…enhee..?”
“Oke, lakini kuna pacha wangu anaitwa baba Pilima.”
Mama Pilima alitumbua macho, akavuta pumzi kwa ndani kisha akajiinamia huku uso wake akiuweka kwenye kiganja cha mkono…
“Baba Pili,” aliita mama Pilima…
“Niambie nakusikiliza…”
“Nisamehe sana! kama ni kweli, ina maana unajua kila kitu…lakini si kosa langu ndiyo maana hata wewe mwenyewe umesema ni pacha wako…
“Lakini naumia sana baba Pili na kitu kimoja…”
“Kitu gani hicho?”
“Nakulaumu…ina maana umekuwa tayari kabisa wewe na ndugu yako kutembea na mwanamke mmoja?”
“Hilo lisingeweza kuzuilika kwani ulitaka mwenyewe…”
Mama Pilima alishtuka kuambiwa alitaka mwenyewe…
“Nilitaka mwenyewe kwa njia gani?”
“Kwani mazingira yenyewe hayakukuonesha kuwa, yule mwanaume si mimi? Unajua ikitokea mimi nakutana na mwanamke aliyefanana na wewe, au ni pacha wako, nitajua tu. Kuna mazungumzo yatakuwa yanaachana.”
Mama Pilima alijikuta katika aibu kubwa baada ya kujua kuwa, mambo yake ya siri yamejulikana…
“Daa! Nimeumbuka mwanamke! Hivi kumbe siku zote hizi ananitafuta lakini anajua kila kitu! Anajua kwamba natembea na pacha wake! Da! Nimevuruga maisha na nimejivunjia rekodi…
“Sikuwa tayari kuwa na uhusiano wa kimapenzi zaidi ya mwanaume mmoja lakini ghafla tu imetokea nimekuwa na mapenzi na wanaume watatu. Baba Pili, baba Pilima yule na baba Pilima mume wangu… Da!” aliwaza sana moyoni mama Pilima.
Lakini moyoni mwanamke huyo alikiri kwamba, wanaume hao wawili ni kiboko kwenye kitanda. Alitamani hata mume wake angekuwa hivyo…
“Kweli ni mapacha, hata mapigo yao ni ya kipachapacha tu,” alisema moyoni mama Pilima.
“Sasa itakuaje baba Pili?” aliuliza mama Pilima…
“Kuhusu nini mama Pili..?”
“Mimi nimekubali kosa, ina maana ndiyo basi tena mimi na wewe au?”
“Nitakujibu,” alisema baba Pili akitoka kitandani na kuanza maandalizi ya kuondoka ndani ya chumba hicho. Mama Pilima naye alijiandaa kwa kuondoka.
***
Alipoachana na baba Pili, mama Pilima hakutaka kukutana na baba Pilima feki, alirudi nyumbani huku uso wake ukijaa aibu kwa kila aliyekutanisha naye uso njiani.
Alifikia kwenye kochi kubwa, akajilaza amechoka ile mbaya. Lakini zaidi sana ni kwamba, atawezaje kuwa mbali na wanaume hao wawili mapacha?
“Nikisema nibaki na baba Pili, baba Pilima naye yuko vizuri sana. nikisema nibaki na baba Pilima, hivyohivyo kwa mwenzake. Hili limeshatokea, kama watakubali nitabaki na wote tu,” aliwaza moyoni mwanamke huyo mwenye umbo nambari nane.
Aliishika simu yake na kubadili muundo wa majina. Baba Pilima feki akamsevu kwa jina la baba P, baba Pili akaendelea kuwa hivyohivyo. Kwa hiyo kwenye simu yake kuwa na baba P, baba Pili na baba Pilima ambaye ni mume wake.
Kwa upande wake, baba Pilima alipokuwa nyumbani kwake alimfikiria mama Pilima kwa maana kwamba, kwa vile si mkewe, aliamua kuendelea naye kimapenzi hata kama pacha wake naye ataendelea naye…
“Kwani mi ni mke wangu yule? Dawa yake ni kupita tu kila nitakapojisikia,” alisema moyoni.
***
Kwa upande wake, baba Pilima hali ilikuwa tofauti kidogo. Yeye alijua penzi lake na mama Pilima limekwisha ndiyo maana mwanamke huyo hakumpokelea simu.
Lakini kwa maneno aliyoambiwa na pacha wake, baba Pili alijua hana chake kwa mama Pilima. Akajuta kwa nini alimsimulia kisa chote pacha wake, angemficha maana wakati anakutana na mama Pilima alijua amemchanganya na baba Pili…
“Da! Ama kweli hakuna siri ya watu wawili. Siri inayodumu ni ile ya wewe peke yako. Sasa kumshirikisha pacha imekuwa nongwa. Je, tungezaliwa kwa kupishana miaka miwili?” alisema moyoni baba Pilima.
***
Usiku, baba Pilima aliwasili nyumbani kwake na kufikia sebuleni. Baada ya kuvua viatu na soksi, alizungumza na mkewe, mama Pilima…
“Anko wako kanipigia simu, anasema nimpigie, ana shida na mimi…sasa simu yangu haina pesa, niazime ya kwako,” alisema baba Pilima huku akiwa tayari ameshanyoosha mkono kuipokea.
Je, nini kilitokea hapo?
 
SEHEMU YA 13



Kulipokucha kabisa, ndiyo kwa mbali akapitiwa na usingizi. Mama Pilima wakati anaamka alishangaa kumwona mumewe bado kitandani wakati anavyojua, huwa anatangulia kuamka siku zote. Alimwamsha…
SHUKA NAYO MWENYEWE SASA…
“Baba Pilima…baba Pilima.”
Baba Pilima alishtuka na kumtumbulia macho mke wake…
“Mbona leo mpaka muda huu bado umelala, una nini mume wangu?”
“We mama Pilima aisee ni kiboko,” alisema baba Pilima huku akiendelea kumwangalia mkewe…
“Kwa nini mume wangu?”
“We tambua hivyo tu.”
Maneno ya baba Pilima yalimsumbua sana mke wake kiasi kwamba, muda huohuo aliwaza mambo yasiyopungua mia kidogo…
“Mh! Au amejua kitu? Lakini kama amejua kitu amejuaje? Mbona ni mambo ya siri sana?”
Alikuwa na shida ya shilingi elfu hamsini asubuhi hiyo lakini akashindwa kumwambia mume wake.
Dakika zilipita, mambo mengine yakaendelea huku baba Pilima akiamua kuingi mzigoni yeye mwenyewe.
Akiwa mjini, baba Pilima alishika simu yake akasachi namba ya baba Pili, akamwendea hewani…
“Haloo,” alipokea baba Pili…
“Mkubwa salama?” alisalimia baba Pilima…
“Salama bwana…nani?”
“Mimi naitwa Emmanuel, nimepewa namba yako na jamaa anaitwa Sudi, kuna biashara fulani alisema unaweza kunielekeza.”
“Sudi? Sudi…Sudi…Sudi…Sudi yule wa Kigamboni?”
“Sijajua anaishi Kigamboni au la!” alijibu baba Pilima…
“Wewe uko wapi?” aliuliza baba Pili…
“Kariakoo…”
“Na mimi nipo Kariakoo. Nipo hapa DDC, njoo basi tuonane ana kwa ana,” alisema baba Pili…
“Oke.”
Lakini wakati baba Pili akimsubiri baba Pilima aliamua kumpigia simu Sudi aliyemjua yeye ili amuulize vizuri kuhusu baba Pilima, lakini jamaa simu yake haikuwa hewani.
Mara, baba Pilima aliingia kwenye Ukumbi wa DDC Kariakoo na kumpigia baba Pili. Naye baba Pili alipoona simu hiyo, akaangalia geti kubwa na kumwona baba Pilima simu ikiwa sikioni huku akishangaashangaa, akamwonesha ishara ya mkono kwamba, yeye yuko pale.
Baba Pilima alitembea hadi pale, akavuta kiti ili kukaa huku akimpa mkono baba Pili na kusema…
“Naitwa Emmanuel.”
“Oke, karibu sana. mimi naitwa Mutu.”
“Oke sawa.”
Kabla baba Pilima hajaanza kusema ya uongo, simu ya mama Pilima ikaingia kwa baba Pili…
“Sore bwana Emmanuel, ngoja nipokee simu ya nyumba ndogo yangu…”
“Sawa…sawa…”
“Haloo mama Pilima…eee! una shida na shing’ ngapi? Oke…mimi nipo DDC Kariakoo, njoo basi nikupe,” alitiririka baba Pili…
“Oke…oke,” akakata simu baba Pili…
“Unajua bwana Emmanuel kuwa na nyumba ndogo ni gharama sana! Yaani huwezi kumwambia huna pesa. Si unataka kulinda uhusiano!” alisema baba Pili huku akimwangalia baba Pilima…
“Enhe, umesema umepewa namba yangu na Sudi?” aliuliza baba Pili akikaa sawasawa pale kwenye kiti huku akijiona ni mwenye bahati ya madili ya mjini.
Kabla baba Pilima hajajibu, naye simu yake iliita…
“Sore, ngoja nipokee simu ya shemeji yako…halooo…eee! Nipo Kurasini….kuna nini..? haya…sawa,” akakata…
“Unajua bwana Mutu kuwa na mke ni lazima utumie akili sana! Na ni lazima umdanganye kidogo. Haitakiwi akajua sehemu rasmi uliyopo…si mmeshajuana tabia,” alisema baba Pilima huku akimwangalia baba Pili…
“Enhe, ulitaka kujua kama namba yako nilipewa na Sudi wa Kigamboni siyo?”
“Eee!”
“Mimi sijui kama anaishi Kigamboni, ila nilikutana naye Sinza,” alisema baba Pilima na kukohoa kidogo.
Lakini sauti yake ilionekana kuwa nzito tofauti na alivyofika, huenda ni baada ya kuuona usaliti wa waziwazi wa mkewe mama Pilima…
“Oke. Lakini chamsingi nadhani si anakoishi Sudi, ni hilo unalotaka nikusaidie maana mimi nina dili na mambo mengi sana, nadili na madini, nadili na ngozi, nadili na mbao, ila tu sidili na madawa ya kulevya,” alisema baba Pili na kuangalia lango kuu.
Kwa baba Pilima hiyo ilikuwa kama kumsukuma mlevi maana alijiuliza sana aingie na gia gani kwa mwanaume huyo ili amuelewe…
“Mimi nina biashara ya madini, madini orijino kabisa. Sasa Sudi akanipa namba na kusema nikikupigia tukikutana unaweza kunisaidia.”
“Unayo hapo?”
“No! Yapo nyumbani, ila nilitaka tukutane kwanza, maana naweza kuyafuata muda wowote ule,” alisema baba Pilima. Kabla baba Pili hajasema kingine chochote, simu yake iliita…
“Sore bwana Emmanuel, nina mgeni nadhani kafika, acha nimwambie aingie huku ndani…”
“Sawasawa, aingie tu,” alikubali baba Pilima…
“Ee mama Pilima mpenzi wangu…geti kubwa..? Oke…sasa ingia ndani basi, ukiingia tu utaniona nimekaa na jamaa yangu mmoja ni mfanyabiahara,” alifunguka baba Pili.
Je, unajua nini kilitokea hapo?
 
SEHEMU YA 14


“Sawasawa, aingie tu,” alikubali baba Pilima…
“Ee mama Pilima mpenzi wangu…geti kubwa..? Oke…sasa ingia ndani basi, ukiingia tu utaniona nimekaa na jamaa yangu mmoja ni mfanyabiashara,” alifunguka baba Pili.
SHUKA NAYO SASA…
Baba Pili akakata simu haraka, kisha akawa anaangalia geti kuu wanaloingilia wateja akiamini mama Pilima ataingia muda huohuo ili ampe ishara kuwa, yeye amekaa palepale.
Mara, uso wa baba Pili ambaye alipokaa alikuwa akiangalia geti kuu, ulionekana kujaa tabasamu laini kuashiria kwamba, mgeni aliyemtarajia, sasa alikuwa anaingia ndani ya ukumbi huo wenye kukusanya watu wengine jijini Dar.
Mama Pilima alitangulia kumwona baba Pili kwani alipokaa uso wake ulikuwa dhahiri, lakini hakumwona mumewe aliyekaa kwa vile mgongo ndiyo uliangalia getini.
Mpaka anafika pale, alikuwa hajamtambua mumewe, hasa kutokana na mkao wake wa kuinamia meza. Inaonekana baba Pilima aliamua kukaa hivyo ili asigundulike haraka.
Mama Pilima, akiwa na uso uliojaa tabasamu la kujua anavuta mkwanja aliouomba, alianza kupeleka mkono kwa baba Pilima kwanza huku akisalimia kwa sauti yenye bashasha, tamu, ya kumtoa nyoka kwenye shimo lake…
“Mambo baby wa miye?”
“Poapoa, karibu sana mpenzi wangu…”
“Oke asante sweet,” alisema kisha akaachana na mkono wa mwenyeji wake huyo na kupeleka mkono kwenye mkono wa mumewe…
“Mambo anko?”
Mumewe aligeuka kiufasaha na kumwangalia mama Pilima usoni ili amwone sawasawa…
“Haaa!” alishtuka mama Pilima.
Mwili wote ulimwisha nguvu, akahisi kizunguzungu, akaanguka chini…puu! Mkoba kule, viatu huko!
“Bwana Emmanuel vipi tena? Mbona huyu mgeni wangu alipokuona wewe tu amepatwa na mshtuko?” aliuliza baba Pili huku akimtumbulia macho baba Pilima…
“Hata mimi sijui, aulizwe yeye, labda amenifananisha.”
Wateja wa baa hiyo walianza kujaa wakimzunguka mwanamke huyo, wengine wakisema ameshafariki dunia, wengine amezimia tu. Wapo waliobashiri kuwa, lazima mgeni wa baba Pili atakuwa anajuana naye tu.
Baba Pilima alitulia kimya akijifanya kweli hajui lolote lakini akimwangalia mkewe kwa macho yaliyojaa mshangao na kujikaza jambo f’lani la ndani sana!
Huduma ya kwanza ilitembea, watu wakatakiwa kukaa pembeni ili mwanamke huyo apate upepo kwa maana ye hewa safi ya oksijeni.
Baada ya dakika kumi na tano hivi, mama Pilima alishtuka. Kijasho chembamba kikimtoka. Alianza kwa kufumbua macho kwa kupepesapepesa huku akiendelea kulala kisha baadaye, akakaa.
Baada ya muda, baba Pili akamsaidia kumkalisha kwenye kiti huku akimpa pole nyingi au tuseme za kumwaga. Si mpenzi wake, sasa je?
“Mama Pilima,” aliita baba Pili kwa sauti ya kumdekeza aliyemwita.
Mama Pilima alikuwa amejiinamia tu kwenye meza. Muda huo, uso wake ulikuwa bado una aibu maana alitambua kwa nini alianguka na kuzimia. Mkoba wake na viatu vyake viliwekwa katika hali ya usalama…
“Mama Pilima,” aliita tena baba Pili, safari hii kwa sauti ya kubembeleza…
“Abee…”
“Pole sana…”
“Asante.”
“Pole sana,” safari hii alisema baba Pilima.
“Asante,” mama Pilima, bila aibu wala soni, achilia mbali haya, eti aliitikia pole ya mumewe…mh!
“Kwani ulijisikiaje?” aliuliza baba Pili.
Kabla mama Pilima hajajieleza, baba Pilima akadakia…
“Bwana Mutu…”
“Naam bwana Emmanuel…”
“Mimi nadhani acha niende, shemeji akiwa ametengemaa, nipigie simu nikuletee mzigo mahali popote pale utakapokuwa…”
“Bwana Emmanuel naweza kukuruhusu, nitakujulisha kila kitu,” alisema baba Pili huku baba Pilima akisimama na kuondoka zake…
“Pole sana,” alimpa pole nyingine mke wake na kuanza kutembea.
Nyuma sasa, baada ya kupita kama dakika tano nzima bila kuwepo wa kuongea, ukimya ulikatika…
“Mama Pilima…”
“Abee…”
“Ni nini kwani mpenzi wangu?”
Mama Pilima kabla hajajibu, aligeuka kuangalia geti kuu, nadhani kujiridhisha kama mumewe alishaondoka kabisa eneo lile…
“Baba Pili, unamjua yule?”
“Eee…anaitwa Emmanuel.”
Mama Pilima alitingisha kichwa cha kukataa kwamba, yule si Emmanuel…
“Yule anaitwa Marco…”
“Marco? We unamjua? Au umemfananisha?”
“Namjua…”
“Ni nani?”
Kabla mama Pilima hajafunguka simu ya baba Pili iliita, aliyepiga ni baba Pilima kwani aliseviwa kwa jina la Emmanuel…
“Subiri kwanza nimsikie huyu mgeni aliyeoondoka,” aliomba baba Pili…
“Haloo bwana Emmanuel…”
“Mimi si Emmanuel, naitwa Marco au baba Pilima…”
Je, unajua nini kilitokea hapo?
 
SEHEMU YA 15


Kabla mama Pilima hajafunguka simu ya baba Pili iliita, aliyepiga ni baba Pilima kwani aliseviwa kwa jina la Emmanuel…
“Subiri kwanza nimsikie huyu mgeni aliyeoondoka,” aliomba baba Pili…
“Haloo bwana Emmanuel…”
“Mimi si Emmanuel, naitwa Marco au baba Pilima…”
SASA ENDELEA…
Baba Pili alikata simu ghafla, akamtumbulia macho mama Pilima…
“Ina maana huyu jamaa ni mumeo?” alimuuliza mama Pilima…
“Ndiyo,” mama Pilima alijibu kwa mkato.
“Mh! Usitake kuniambia mama Pilima. Ina maana amejua kila kitu?” aliuliza tena baba Pili…
“Siyo amejua kila kitu, bali nahisi amepanga kufanya hivi…we unafahamiana naye?” mama Pilima alimuuliza baba Pili…
“Simfahamu…yaani ilikuwa hivi…”
Baba Pili alianza kumsimulia kila kitu mama Pilima huku akionekana kuwa na wasiwasi sana. Mama Pilima naye alikuwa na wasiwasi mkubwa. Kwanza alijua mume wake hakwenda mbali na angerudi kwa njia ya fumanizi sasa.
Hivyo alikuwa na mchecheto…
“Sasa mimi naona niondoke zangu,” alisema mama Pilima huku akisimama. Ni baada ya maelezo ya baba Pili ambapo ilibainika wawili hao siyo watu wanaojuana, hivyo mama Pilima akajua kuna kitu.***
Baba Pilima alipotoka hapo alimpigia simu baba Pilima feki…
“Mambo ndugu yangu?”
“Poapoa, nani mwenzangu?”
“Mimi naitwa Juma Ally. Namba yako nimepewa na rafiki yako, anaitwa Juma kama mimi…uko wapi nikuone? Nina biashara nataka kufanya na wewe!”
Alipoulizwa hivyo, awali alijiuliza Juma Ally alikuwa nani na alitaka kufanya naye biashara gani, hakupata jibu.
Kwa kuwa alipozi sekunde kadhaa bila kuendelea kuzungumza na aliyempigia simu, baba Pilima akamwambia;
“Vipi ndugu yangu mbona huzungumzi, muhimu sana tuonane leo kwani kesho natarajia kusafiri.”
Baba Pilima feki alipoambiwa hivyo akaona kabla ya kuendelea na mazungumzo amwulize ni Juma yupi aliyempatia namba yake;
“Oke…namba yangu amekupa Juma yupi? Maana kuna Juma wa Kimara na Juma wa Mbezi Beach!”
“Mh! Yule sijajua anaishi Mbezi ipi!”
“Anyway, wewe njoo mpaka Buguruni, kuna baa inaitwa Sewa, mimi nipo hapa.”
“Hapo Sewa unatarajia kukaa kwa muda gani maana nipo mbali kidogo?” baba Pilima feki alimwuliza.
“Mimi nitakusubiri muda wowote, kikubwa nataka kuonana na wewe leo,” baba Pilima alimwambia.
“Sawa.”
Baba Pilima aliharakisha kufika Buguruni mpaka kwenye baa hiyo, akazama ndani na kumkuta baba Pilima mwenzake amekaa na washkaji wake watatu, akiwemo Juma mmoja.
Baada ya salamu, baba Pilima feki akasema…
“Sasa wewe namba yangu utakuwa umepewa na Juma wa Mbezi Beach, maana Juma wa Kimara ni huyu hapa…”
“Oke…oke…oke! Sawa.”
“Sasa jamani ngoja nikae na mgeni wangu pembeni kidogo,” alisema baba Pilima huku akisimama, akaenda kukaa meza nyingine na baba Pilima mwenyewe…
“Enhee, niambie ndugu yangu…ulisema unaitwa..?”
“Juma Ally.”
“Haya Juma Ally niambie.”
***
Mama Pilima kule Kariakoo hakupenda kurudi nyumbani bila kukutana na mumewe kwanza na kuzungumza naye ili ikibidi mambo yaishe ndipo aweze kufika nyumbani…
“Yaani bila kumaliza haya mambo sidhani kama nitaweza kurudi nyumbani. Hali yangu itakuwa mbaya mimi,” alisema moyoni mama Pilima. Alimpigia simu…
“Sorry… ngoja nipokee simu ya mke wangu kwanza,” alisema baba Pilima…
“Oke…oke…”
Baba Pilima alimpokelea mkewe…
Lakini wakati huohuo, simu ya baba Pilima feki iliita, aliyepiga ni baba Pili, pacha wake. Alitaka kumpasha kilichomtokea lakini baba Pilima feki hakupokea kwa sababu baba Pilima au Juma Ally alikuwa akiongea na mkewe, akamtumia meseji…
“Nitakupigia niko na mgeni wangu mara moja.”
“Poa,” alijibu baba Pili…
“Uko wapi baba Pilima?” mama Pilima alimuuliza mke wake…
“Niko Buguruni…”
“Naomba nije tuonane please…”
“Njoo.”
“Oke, Buguruni sehemu gani?”
“Kuna baa inaitwa Sewa.”
“Poa.”
Baba Pilima mwenyewe alimshukuru Mungu wake akijua amemaliza kazi maana mkewe amejiingiza mwenyewe kwenye mtego wake…
“Enhe, niambie bwana Juma,” alisema baba Pilima feki huku akikaa sawasawa au akikaa vizuri.
“Mimi ninashughulika na biashara ya mbao, sasa niliambiwa wewe unajua wateja wanaolipa sawasawa…sijui ni kweli?” alianza kusema baba Pilima mwenyewe.
Baba Pilima feki alimtumbulia macho pima, maana yeye si mfanyabiashara kabisa, sasa hata kama ni kweli alipewa namba na Juma wa Mbezi Beach, mbona naye anajua yeye si mfanyabiashara!!
“Da! Umenipeleka mbali sana bwana Juma Ally…kwanza kama kweli Juma ndiyo amekupa namba yangu mbona anajua mimi siyo mfanyabiashara au alikosea akakupa namba yangu?”
“Mimi sijui,” alijibu baba Pilima mwenyewe. Alishaanza kuwa na wasiwasi sasa.
Akashika simu yake na kuandika namba za rafiki yake Juma wa Mbezi Beach ili amuulize kisa cha kutoa namba yake kwamba anawajua wateja wa mbao wakati anajua yeye si mfanyabiashara.
Baba Pilima mwenyewe alitaka kumzuia, lakini moyoni akasema aache tu, atapambana mpaka mwisho na vile mkewe yuko njiani, mshindi atakuwa yeye tu…
“Haloo Juma…” alianza kwa kuita baba Pilima feki…
Je, unajua nini kilitokea hapo?
 
SEHEMU YA 16


“Mimi sijui,” alijibu baba Pilima. Alishaanza kuwa na wasiwasi sasa. Akashika simu na kuandika namba ya rafiki yake Juma wa Mbezi-Beach ili amuulize kisa cha kutoa namba yake kwamba anawajua wateja wa mbao wakati anajua yeye si mfanyabiashara.
JIACHIE MWENYEWE SASA…
Baba Pilima mwenyewe alitaka kumzuia, lakini moyoni akasema aache tu, atapambana mpaka mwisho na vile mkewe yuko njiani, mshindi atakuwa yeye tu…
“Haloo Juma…” alianza kwa kuita baba Pilima feki…
“Haloo, niambie…”
“Eti unamfahamu jamaa anaitwa…”
Kabla hajamaliza kusema, simu yake ilikatika kwa sababu ya mtandao, akapiga tena.
Simu iliita sana, lakini haikupokelewa upande wa pili.
Simu ya baba Pilima mwenyewe ikaita, mkewe alishafika…
“Nipo hapa nje ya Baa ya Sewa…”
“Ingia ndani sasa.”
“Poa.”
Mama Pilima alizama ndani na kushtuka kumwona baba Pilima mumewe akiwa amekaa na baba Pilima feki…
“Ha!” alihamaki mama Pilima, akaanguka tena.
Baba Pilima feki alishtuka sana. Alishtuka kwa mambo mawili. Kwanza kwa kumwona mama Pilima, pili kwa kuanguka…
“He! Huyu mwanamke namfahamu, ni mwanamke wangu, sasa sijui imekuwaje tena na sijui amekuja kufuata nini hapa?” alihoji baba Pilima feki huku akimtumbulia macho mama Pilima pale chini…
“Wewe ni mwanamke wako, mimi ni mke wangu,” alisema baba Pilima mwenyewe. Baba Pilima feki naye akaanza kuweweseka huku jasho jembamba likimtoka…
“Ina…ina…ina maana…ina maana,” alisema baba Pilima feki ambaye kwenye simu ya mama Pilima aliseviwa kwa jina la Baba P…
“Usisumbuke sana ndugu, kaja hapa kwa sababu yangu na mimi nimekutafuta wewe kwa sababu ya yeye. Wewe ndiye Baba P, unatembea na mke wangu huku ukijua ana mume…muda si mrefu nimetoka kwa Baba Pili…nadhani ni mapacha maana hata sura zenu zinafanana,” alisema baba Pilima huku akiwa amekasirika sana.
Watu walimzunguka mama Pilima, baba Pilima mwenyewe akiwa anamsaidia mkewe akae kwenye kiti maana safari hii hakupoteza fahamu kama kule DDC-Kariakoo…
“Pole sana jamani…pole,” watu walimpa pole mama Pilima akiwa amekaa kwenye kiti…
“Baba Pilima mume wangu,” aliita mama Pilima kwa sauti ya chini sana ikiashiria kuchoka na mambo yalivyokwenda…
“Nini?” baba Pilima alimjibu hivyo mke wake…
“Nimekukubali mume wangu. Hata kama leo utanipa talaka lakini nitakuheshimu kuliko mwanaume yeyote hapa duniani. Najua kukutana wewe na yule mwanaume Kariakoo ilikuwa mbinu yako, lakini pia kukutana na huyu hapa pia ni mbinu yako japokuwa mimi nimejikuta nikiingia kichwakichwa…
“Sikutaka kukusaliti. Imetokea tu! Lakini si kwamba sikupendi na huenda labda ni kwa sababu ya mambo yetu ya siri nyumbani…nisamehe kwa utangulizi lakini uamuzi ni wako ingawa mimi kama mimi ningependa unisamehe,” alisema mama Pilima huku akiona aibu kwa watu waliokuwa wakimsikiliza.
Baba Pilima alimwangalia mkewe kwa macho ya kumshangaa sana kisha akasema…
“Umemaliza kusema?”
“Nimemaliza baba Pilima mume wangu.”
“Kwa hiyo kama kuna matatizo nyumbani ndiyo ukaamua kutembea na mapacha?”
“Hiyo nayo ni stori ndefu mume wangu, inataka nafasi ya kusimulia kwa mapana,” alisema mama Pilima huku akizidi kuona aibu.
Baba Pilima alisimama, akamuaga baba P kwamba anaondoka huku akisema…
“Mkubwa mimi sifanyi biashara yoyote. Sina mbao wala miti. Ila nilitaka kukuona. Nimejikaza sana katika hii ishu.
Ningekuwa mwanaume mwingine nadhani ningeua mtu au ningeua watu. Lakini mjue kwamba mimi ni binadamu kama binadamu wengine, sijapenda mlichonifanyia. Nasema sijapenda kwa sababu wote mlijua huyu ni mke wa mtu japokuwa hata yeye alitakiwa kujijua kwamba ni mke wa mtu. Naye ana nafasi yake ya lawama.”
Wakati baba Pilima akimalizikia kutoka nje ya baa hiyo, mama Pilima kule ndani aliangua kilio huku naye akisimama…
“Nilishasema mimi sijawahi kusaliti jamani. Sijui shetani gani amenikuta katika kipindi hiki cha kuelekea uzeeni. Kwani kama ningemvumilia mume wangu na udhaifu wake nini kingenipata mama Pilima!”
Watu waliojua kisa hicho walimzomea mama Pilima huku baba P akibaki kushangaa. Simu yake ikaita, alipiga baba Pili…
“Haloo,” alipokea baba P…
“Ndugu yangu yamenikuta mazito,” alisema baba Pili…
“Nadhani hayo yako ni madogo, mimi zaidi…mwenzako si nimefumaniwa na mume wa mama Pilima…” alisema baba P.
yaani we acha tu…haya wewe mwenzangu yamekupata makubwa yapi?” alisema baba P…
“He! Mume wa mama Pilima?”
“Ndiyo…”
“Mbona hata mimi pia imekuwa hivyo…”
“Wewe lini?”
“Muda si mrefu ndugu yangu.”
Simu ya mama Pilima iliita akiwa nje ya baa hiyo, alipoangalia mpigaji ni mume wake…
Je, unajua nini kilitokea hapo?
 
SEHEMU YA 17


“He! Mume wa mama Pilima?”
“Ndiyo…”
“Mbona hata mimi pia imekuwa hivyo…”
“Wewe lini?”
“Muda si mrefu ndugu yangu.”
Simu ya mama Pilima iliita akiwa nje ya baa hiyo, alipoangalia mpigaji ni mume wake…
SASA JIACHIE KIVYAKO…
Aliipokea huku akitetemeka…
“Halo baba Pilima…”
“Najua umeona ushatani wako ulipokuwa. Umekuwa mwaminifu miaka yote unakuja kuanguka mbeleni huku mke wangu…”
“Nisamehe baba Pilima…”
“Kwanza ujasiri wa kutembea na wanaume wawili umeutolea wapi mke wangu?”
“Baba Pilima ni hadithi ndefu, wale akina kaka ni mapacha. Walitumia nafasi hiyo kunipata wote nikiwa sijui kama ni mapacha,” alisema mama Pilima akitumia sauti ya chini sana yenye kuonesha majuto ni mjukuu…
“Sikiliza mama Pilima, mimi kutoka moyoni mwangu nimekusamehe!”
Mama Pilima alianguka chini nje ya kituo cha mabasi, watu wakaanza kutafutana. Habari za kuanguka kwake zilifika hadi ndani ya Baa ya Sewa ambapo, baba Pilima feki ni mmoja wa watu waliosikia, lakini hakujua ni nani!
Alipotoka kuangalia na kumkuta ni mama Pilima alishtuka sana. Lakini kwa sababu ya mambo yaliyotokea hakutaka kumsaidia wala kuendelea kusimama kuendelea kuangalia pale…
“Mh! Huu ni msala. Jamaa yake akitokea inaweza kuwa balaa,” alisema moyoni baba Pilima feki huku akiondoka zake eneo hilo.
Baba Pilima alishangaa sana mkewe kukatika hewani ghafla halafu huku akisikia kishindo kikubwa cha puu! Alipojaribu kumpigia hakuwa hewani…
“Khaa! Sasa huyu amekumbwa na kitu gani tena?” alijiuliza baba Pilima.
Baadhi ya vijana wa kihuni waliinyakua simu ya mama Pilima na kutokomea nayo wakiwa wameshaizima na ndiyo maana mume wake hakumpata tena hewani.
Kutokana na tukio hilo la aina yake, baba Pilima mwenyewe aliamua kurudi nyumbani kupumzisha akili siku hiyo huku akimuwaza mkewe na alichokifanya. Lakini bado ndani ya moyo wake aliamini, yaliyotokea yamekuwa funzo kwa mwanamke huyo.
***
Ndani ya dakika kumi, mama Pilima naye aliamka. Au alizinduka. Ama fahamu zilimrejea, akakaa na kuangalia kulia na kushoto, mbele na nyuma na kubaini nini kilimtokea muda mfupi nyuma.
Mkoba wake ulikuwepo, lakini simu hakuiona. Miongoni mwa watu waliokuwa wakimfuatilia pale chini ni wanawake wenzake na watu wazima tu, vijana wote, wakiwemo wa kihuni walikuwa hawana habari…
“Simu yangu,” alisema mama Pilima…
“Watakuwa wameikwapua vibaka,” walisema watu.
Mama Pilima alisimama kwa kujizoazoa, akapanda basi na kukaa siti ya nyuma kabisa akiwa peke yake. Baadhi ya sehemu za nguo zake zilichafuka kutokana na kuanguka…
“Kweli baba Pilima anaweza kunisamehe kwa kosa kubwa kama hili? Hata siamini! Labda nilimsikia vibaya,” alisema mwanamke huyo akiwa kweli haamini kama amesamehewa.
Alipofika nyumbani, alimkuta mumewe, baba Pilima, wifi yake pia alikuwepo sebuleni. Msichana wa kazi akiendelea na kazi za kupika. Watoto, akiwemo Pilima walikuwa hawajarudi toka walikokwenda.
Wifi mtu alishtuka sana kumwona mama Pilima amechafuka vile…
“Ha! Wifi…umekutwa na jambo gani? Mbona umechafuka?”
Mama Pilima alimwangalia mumewe badala ya aliyemuuliza swali. Alijua mumewe atasema yote…
“Wifi nilianguka nikapoteza fahamu,” alisema mama Pilima na kuanza kulia.
Ikawa hekaheka nyingine, wifi mtu huyo akiwa anataka kujua kwa undani kuhusu wifi yake kuanguka ghafla na kupoteza fahamu…
“Haa! Kaka! Wewe unajua lolote?”
“Nilikuwa naongea naye, lakini ghafla akapotea hewani. Nilipokuwa nampigia tena, hakuwa hewani. Nadhani ndiyo alianguka hapo.”
“Wifi…”
“Abee…”
“Pole sana. Sasa simu iko wapi?”
“Imeibiwa wifi,” alisema mama Pilima.
Baba Pilima alimshika mkono mke wake mpaka chumbani. Alimvua nguo, akamvalisha kanga na taulo na kumtaka akaoge.
Baada ya kuoga, mama Pilima na mumewe wakakaa chumbani…
“Mume wangu, asiyefunzwa na mamaye hufunzwa na ulimwengu. Kwa haya yaliyonikuta mimi nimefunzwa tayari. Nataka kusikia kauli yako kwa mara ya pili kama kweli umenisamehe.”
“Nimekusamehe mama Pilima. Ila likijirudia jambo hilo tena, itakuwa tiketi yetu ya kutengana moja kwa moja,” alisema baba Pilima.
Mama Pilima alipiga magoti, akaweka mikono pamoja kaka anayesali, akamsihi mumewe kuwa na amani. Ujinga ule hautajirudia tena.
“Naomba iwe hivyo katika maisha yako yote.”
“Nakuahidi itakuwa hivyo baba Pilima.”
***
Kwa upande wa wale mapacha, baba Pilima feki na baba Pili walikwenda kukutana sehemu. Wakaongelea lile tukio, wakakubaliana kuzitupa laini zao na kununua mpya ili wasitafutwe. Walijuta na kujuta na kujuta!
MWISHO.
 
Shu
SEHEMU YA 17


“He! Mume wa mama Pilima?”
“Ndiyo…”
“Mbona hata mimi pia imekuwa hivyo…”
“Wewe lini?”
“Muda si mrefu ndugu yangu.”
Simu ya mama Pilima iliita akiwa nje ya baa hiyo, alipoangalia mpigaji ni mume wake…
SASA JIACHIE KIVYAKO…
Aliipokea huku akitetemeka…
“Halo baba Pilima…”
“Najua umeona ushatani wako ulipokuwa. Umekuwa mwaminifu miaka yote unakuja kuanguka mbeleni huku mke wangu…”
“Nisamehe baba Pilima…”
“Kwanza ujasiri wa kutembea na wanaume wawili umeutolea wapi mke wangu?”
“Baba Pilima ni hadithi ndefu, wale akina kaka ni mapacha. Walitumia nafasi hiyo kunipata wote nikiwa sijui kama ni mapacha,” alisema mama Pilima akitumia sauti ya chini sana yenye kuonesha majuto ni mjukuu…
“Sikiliza mama Pilima, mimi kutoka moyoni mwangu nimekusamehe!”
Mama Pilima alianguka chini nje ya kituo cha mabasi, watu wakaanza kutafutana. Habari za kuanguka kwake zilifika hadi ndani ya Baa ya Sewa ambapo, baba Pilima feki ni mmoja wa watu waliosikia, lakini hakujua ni nani!
Alipotoka kuangalia na kumkuta ni mama Pilima alishtuka sana. Lakini kwa sababu ya mambo yaliyotokea hakutaka kumsaidia wala kuendelea kusimama kuendelea kuangalia pale…
“Mh! Huu ni msala. Jamaa yake akitokea inaweza kuwa balaa,” alisema moyoni baba Pilima feki huku akiondoka zake eneo hilo.
Baba Pilima alishangaa sana mkewe kukatika hewani ghafla halafu huku akisikia kishindo kikubwa cha puu! Alipojaribu kumpigia hakuwa hewani…
“Khaa! Sasa huyu amekumbwa na kitu gani tena?” alijiuliza baba Pilima.
Baadhi ya vijana wa kihuni waliinyakua simu ya mama Pilima na kutokomea nayo wakiwa wameshaizima na ndiyo maana mume wake hakumpata tena hewani.
Kutokana na tukio hilo la aina yake, baba Pilima mwenyewe aliamua kurudi nyumbani kupumzisha akili siku hiyo huku akimuwaza mkewe na alichokifanya. Lakini bado ndani ya moyo wake aliamini, yaliyotokea yamekuwa funzo kwa mwanamke huyo.
***
Ndani ya dakika kumi, mama Pilima naye aliamka. Au alizinduka. Ama fahamu zilimrejea, akakaa na kuangalia kulia na kushoto, mbele na nyuma na kubaini nini kilimtokea muda mfupi nyuma.
Mkoba wake ulikuwepo, lakini simu hakuiona. Miongoni mwa watu waliokuwa wakimfuatilia pale chini ni wanawake wenzake na watu wazima tu, vijana wote, wakiwemo wa kihuni walikuwa hawana habari…
“Simu yangu,” alisema mama Pilima…
“Watakuwa wameikwapua vibaka,” walisema watu.
Mama Pilima alisimama kwa kujizoazoa, akapanda basi na kukaa siti ya nyuma kabisa akiwa peke yake. Baadhi ya sehemu za nguo zake zilichafuka kutokana na kuanguka…
“Kweli baba Pilima anaweza kunisamehe kwa kosa kubwa kama hili? Hata siamini! Labda nilimsikia vibaya,” alisema mwanamke huyo akiwa kweli haamini kama amesamehewa.
Alipofika nyumbani, alimkuta mumewe, baba Pilima, wifi yake pia alikuwepo sebuleni. Msichana wa kazi akiendelea na kazi za kupika. Watoto, akiwemo Pilima walikuwa hawajarudi toka walikokwenda.
Wifi mtu alishtuka sana kumwona mama Pilima amechafuka vile…
“Ha! Wifi…umekutwa na jambo gani? Mbona umechafuka?”
Mama Pilima alimwangalia mumewe badala ya aliyemuuliza swali. Alijua mumewe atasema yote…
“Wifi nilianguka nikapoteza fahamu,” alisema mama Pilima na kuanza kulia.
Ikawa hekaheka nyingine, wifi mtu huyo akiwa anataka kujua kwa undani kuhusu wifi yake kuanguka ghafla na kupoteza fahamu…
“Haa! Kaka! Wewe unajua lolote?”
“Nilikuwa naongea naye, lakini ghafla akapotea hewani. Nilipokuwa nampigia tena, hakuwa hewani. Nadhani ndiyo alianguka hapo.”
“Wifi…”
“Abee…”
“Pole sana. Sasa simu iko wapi?”
“Imeibiwa wifi,” alisema mama Pilima.
Baba Pilima alimshika mkono mke wake mpaka chumbani. Alimvua nguo, akamvalisha kanga na taulo na kumtaka akaoge.
Baada ya kuoga, mama Pilima na mumewe wakakaa chumbani…
“Mume wangu, asiyefunzwa na mamaye hufunzwa na ulimwengu. Kwa haya yaliyonikuta mimi nimefunzwa tayari. Nataka kusikia kauli yako kwa mara ya pili kama kweli umenisamehe.”
“Nimekusamehe mama Pilima. Ila likijirudia jambo hilo tena, itakuwa tiketi yetu ya kutengana moja kwa moja,” alisema baba Pilima.
Mama Pilima alipiga magoti, akaweka mikono pamoja kaka anayesali, akamsihi mumewe kuwa na amani. Ujinga ule hautajirudia tena.
“Naomba iwe hivyo katika maisha yako yote.”
“Nakuahidi itakuwa hivyo baba Pilima.”
***
Kwa upande wa wale mapacha, baba Pilima feki na baba Pili walikwenda kukutana sehemu. Wakaongelea lile tukio, wakakubaliana kuzitupa laini zao na kununua mpya ili wasitafutwe. Walijuta na kujuta na kujuta!
MWISHO.
Ahsante sana mkuu kwa kutuletea genye lakini pia kwa kumaliza chombezo lako
 
SEHEMU YA 17


“He! Mume wa mama Pilima?”
“Ndiyo…”
“Mbona hata mimi pia imekuwa hivyo…”
“Wewe lini?”
“Muda si mrefu ndugu yangu.”
Simu ya mama Pilima iliita akiwa nje ya baa hiyo, alipoangalia mpigaji ni mume wake…
SASA JIACHIE KIVYAKO…
Aliipokea huku akitetemeka…
“Halo baba Pilima…”
“Najua umeona ushatani wako ulipokuwa. Umekuwa mwaminifu miaka yote unakuja kuanguka mbeleni huku mke wangu…”
“Nisamehe baba Pilima…”
“Kwanza ujasiri wa kutembea na wanaume wawili umeutolea wapi mke wangu?”
“Baba Pilima ni hadithi ndefu, wale akina kaka ni mapacha. Walitumia nafasi hiyo kunipata wote nikiwa sijui kama ni mapacha,” alisema mama Pilima akitumia sauti ya chini sana yenye kuonesha majuto ni mjukuu…
“Sikiliza mama Pilima, mimi kutoka moyoni mwangu nimekusamehe!”
Mama Pilima alianguka chini nje ya kituo cha mabasi, watu wakaanza kutafutana. Habari za kuanguka kwake zilifika hadi ndani ya Baa ya Sewa ambapo, baba Pilima feki ni mmoja wa watu waliosikia, lakini hakujua ni nani!
Alipotoka kuangalia na kumkuta ni mama Pilima alishtuka sana. Lakini kwa sababu ya mambo yaliyotokea hakutaka kumsaidia wala kuendelea kusimama kuendelea kuangalia pale…
“Mh! Huu ni msala. Jamaa yake akitokea inaweza kuwa balaa,” alisema moyoni baba Pilima feki huku akiondoka zake eneo hilo.
Baba Pilima alishangaa sana mkewe kukatika hewani ghafla halafu huku akisikia kishindo kikubwa cha puu! Alipojaribu kumpigia hakuwa hewani…
“Khaa! Sasa huyu amekumbwa na kitu gani tena?” alijiuliza baba Pilima.
Baadhi ya vijana wa kihuni waliinyakua simu ya mama Pilima na kutokomea nayo wakiwa wameshaizima na ndiyo maana mume wake hakumpata tena hewani.
Kutokana na tukio hilo la aina yake, baba Pilima mwenyewe aliamua kurudi nyumbani kupumzisha akili siku hiyo huku akimuwaza mkewe na alichokifanya. Lakini bado ndani ya moyo wake aliamini, yaliyotokea yamekuwa funzo kwa mwanamke huyo.
***
Ndani ya dakika kumi, mama Pilima naye aliamka. Au alizinduka. Ama fahamu zilimrejea, akakaa na kuangalia kulia na kushoto, mbele na nyuma na kubaini nini kilimtokea muda mfupi nyuma.
Mkoba wake ulikuwepo, lakini simu hakuiona. Miongoni mwa watu waliokuwa wakimfuatilia pale chini ni wanawake wenzake na watu wazima tu, vijana wote, wakiwemo wa kihuni walikuwa hawana habari…
“Simu yangu,” alisema mama Pilima…
“Watakuwa wameikwapua vibaka,” walisema watu.
Mama Pilima alisimama kwa kujizoazoa, akapanda basi na kukaa siti ya nyuma kabisa akiwa peke yake. Baadhi ya sehemu za nguo zake zilichafuka kutokana na kuanguka…
“Kweli baba Pilima anaweza kunisamehe kwa kosa kubwa kama hili? Hata siamini! Labda nilimsikia vibaya,” alisema mwanamke huyo akiwa kweli haamini kama amesamehewa.
Alipofika nyumbani, alimkuta mumewe, baba Pilima, wifi yake pia alikuwepo sebuleni. Msichana wa kazi akiendelea na kazi za kupika. Watoto, akiwemo Pilima walikuwa hawajarudi toka walikokwenda.
Wifi mtu alishtuka sana kumwona mama Pilima amechafuka vile…
“Ha! Wifi…umekutwa na jambo gani? Mbona umechafuka?”
Mama Pilima alimwangalia mumewe badala ya aliyemuuliza swali. Alijua mumewe atasema yote…
“Wifi nilianguka nikapoteza fahamu,” alisema mama Pilima na kuanza kulia.
Ikawa hekaheka nyingine, wifi mtu huyo akiwa anataka kujua kwa undani kuhusu wifi yake kuanguka ghafla na kupoteza fahamu…
“Haa! Kaka! Wewe unajua lolote?”
“Nilikuwa naongea naye, lakini ghafla akapotea hewani. Nilipokuwa nampigia tena, hakuwa hewani. Nadhani ndiyo alianguka hapo.”
“Wifi…”
“Abee…”
“Pole sana. Sasa simu iko wapi?”
“Imeibiwa wifi,” alisema mama Pilima.
Baba Pilima alimshika mkono mke wake mpaka chumbani. Alimvua nguo, akamvalisha kanga na taulo na kumtaka akaoge.
Baada ya kuoga, mama Pilima na mumewe wakakaa chumbani…
“Mume wangu, asiyefunzwa na mamaye hufunzwa na ulimwengu. Kwa haya yaliyonikuta mimi nimefunzwa tayari. Nataka kusikia kauli yako kwa mara ya pili kama kweli umenisamehe.”
“Nimekusamehe mama Pilima. Ila likijirudia jambo hilo tena, itakuwa tiketi yetu ya kutengana moja kwa moja,” alisema baba Pilima.
Mama Pilima alipiga magoti, akaweka mikono pamoja kaka anayesali, akamsihi mumewe kuwa na amani. Ujinga ule hautajirudia tena.
“Naomba iwe hivyo katika maisha yako yote.”
“Nakuahidi itakuwa hivyo baba Pilima.”
***
Kwa upande wa wale mapacha, baba Pilima feki na baba Pili walikwenda kukutana sehemu. Wakaongelea lile tukio, wakakubaliana kuzitupa laini zao na kununua mpya ili wasitafutwe. Walijuta na kujuta na kujuta!
MWISHO.

Safi sana... Story nzuri...

Chapter Closed...



Cc: mahondaw
 
Back
Top Bottom