Chitanda ajiunga na CCM

Chitanda ajiunga na CCM

Anajiunga mara ngapi na CCM, wakati siku zote mharibifu huyo alikuwa CCM? Huo ni uthibitisho tu wa wazi kwamba yeye na wenzake kumbe walikuwa ni mbwamwitu wenye mavazi ya kondoo! KWAHERI YA KUTOKUONANA!
 
Kwani lini aliacha kuhama vyama, karibu kila chama keshahamia. Kaanzia CCM Kaja NCCR then NCCR Mageuzi, then TLP then Chadema now back CCM. Malaya atabaki malaya

LEMA - CCM -> NCCR ->TLP -> CHADEMA ->? Naye huyu ni malaya?
 
Hizi Njaa zitatumaliza,

Huyu si alikuwepo kwenye ule waraka, na ni miongoni mwa watu waliopiga pesa wakaahidi kujiuzuli ili kuhakikisha viongozi wote wa Chadema wanajiuzulu kwa wakati mmoja kumuunga mkono ZZK.

Mwambieani amchukue na jamaa yake ZZK wakale bata CCM na kusaidiana kuuza hii nchi.
 
Pole nadhani mfadhili baada ya kuchaguliwa naibu waziri amekata mawasiliano hakuna pa kunyonya mrija ha ha jamaa katoswa mchana peupe
 
Unajua kesho atajiunga na chama gani?

mara nyingi nimekuonya kuhusu kumkashifu MTUKUFU LEMA , kwa taarifa yako ni kwamba tumempa kazi MH LEMA ya kuhakikisha Lowasa anastaafu siasa , BAADA YA LEMA KUWAPA NENO LA UKOMBOZI WAFUGAJI .
 
Kilichopo ambacho watu wengi hasa vijana hawataki kuamini ni kwamba............kwawale woote walisoma shule za msingi kabla ya 1992....kulikuwa na siku maalumu katika wiki wanafunzi wanaapishwa kiapo cha kuitii na kuitumikia TANU/CCM kwa moyo na nguvu zote...........huku mwihoni tukisema ''eehhh Mwenyezi Mungu Nisaidie''..........kiapo hiki waliapa pia akina Slaa,Mtei,Lipumba,Mrema nk......so ni ngumu kuwa wapinzani wa kweli kutokaana na viapo walivyofanya awali ndio maana kila kukicha ni kufukuzana , kuitana wasaliti nk..........ukweli ni kwamba vijana wengi wenye miaka chini ya 25 wanaweza kuwa wapinzani wa kweli ila viongozi wengi wa upinzani sio wa kweli...........!
Hiyo shule yenu kiboko yaani mlikuwa mnalishwa kiapo kila wiki!shule ya msingi nimeanza wakati wa utawala wa Rais Nyerere na kumaliza wakati wa Utawala wa Rais Mwinyi sijawahi kushuhudia kitu kama hicho labda mlikuwa mnakula viapo shuleni kwenu tu.
 
[h=1]ALIYEKUWA Mwenyekiti wa CHADEMA Mkoa wa Lindi ambaye hivi karibuni alitangaza kuachia wadhifa huo, Ali Chitanda, ametangaza kujiunga na Chama Cha Mapinduzi (CCM).
Alifikia uamuzi huo juzi kwenye mkutano wa uzinduzi wa kampeni za CCM za udiwani wa Kata ya Namikango, Wilaya ya Nachingwea.
Alisema licha ya kuamua kuhamia CCM, pia aliahidi kukifanyia chama hicho kampeni katika mikutano yake yote itakayoifanya wakati wa kampeni iliyoizindua hadi atakapohakikisha kiti hicho cha udiwani kinarejea CCM.
"Nimekuwa kwenye vyama vya upinzani kwa miaka mingi lakini tatizo la CHADEMA kinaendeshwa kama kampuni ya mtu binafsi inayojali masilahi ya viongozi wachache, hivyo ndugu zangu wananchi naomba msikiunge mkono chama ambacho hakifuati masilahi ya watu hasa maskini,” alisema Chitanda.
Akizungumza baada ya kutambulishwa na Katibu wa CCM Mkoa wa Mtwara, Shaibu Akwilombe, Chitanda aliwataka vijana wanaokimbilia CHADEMA kuanza kujiuliza kabla ya kufikia uamuzi wa kujiunga na chama hicho.
"Chama hicho kimepoteza mwelekeo kutokana na viongozi wachache kukifanya chama hicho kuwa ni taasisi binafsi," alisema amekitumikia kwa miaka 10, sasa ameamua kuondoka. Chanzo-Majira
Aliongeza kuwa; “Kati ya watu ambao wamekaa muda mrefu na kushika nyadhifa mbalimbali kwenye vyama mbalimbali vya upinzani kuanzia NCCR-Mageuzi hadi CHADEMA, nimeamua kuachana na vyama hivyo baada ya kubaini kuwa ni mali ya wachache kwa masilahi yao.”
Kauli hiyo ya Chitanda iliungwa mkono na Akwilolmbe ambaye kabla ya kurejea CCM aliwahi kuwa Naibu Katibu Mkuu wa CUF na baadaye kuwa pia Naibu katibu mkuu wa CHADEMA na kuamua kuachana na vyama hivyo kwa kile alichosema kuchoshwa na vitendo vya ubinafsi. Chitanda inadaiwa alikuwa mmoja wa marafiki wa karibu wa aliyekuwa Naibu Katibu Mkuu wa chama hicho Bara, Zitto Kabwe, ambaye hivi karibuni alivuliwa wadhifa huo.
Chitanda alitangaza kujiuzulu wadhifa wake mkoani Lindi siku chache mara baada ya Zitto, kuvuliwa wadhifa wake kutokana na kudaiwa kufanya uasi ndani ya chama hicho[/h]
 
Back
Top Bottom