#COVID19 China yaahidi dozi Bilioni 1 za Chanjo kwa Afrika

Analogia Malenga

JF-Expert Member
Feb 24, 2012
5,005
9,872
Rais wa China Xi Jinping ameahidi kutuma barani Afrika dozi bilioni moja za chanjo ya Covid-19 ili kusaidia kuziba "pengo la chanjo". Rais alitoa ahadi hiyo wakati wa mkutano wa kilele wa China na Afrika.

Kati ya bilioni moja, dozi milioni 600 zitatoka China moja kwa moja huku milioni 400 zitatoka kwa vyanzo vingine kama vile maeneo ya uzalishaji yatakayofadhiliwa. China tayari imekuwa ikitoa dozi kwa nchi za Afrika.

Ahadi ya hivi majuzi inakuja huku kukiwa na kuenea kwa aina mpya ya virusi kwa jina Omicron ambayo iligunduliwa kwa mara ya kwanza kusini mwa Afrika.

BBC Swahili
 
Africa kupiga hatua, tuombe vita ya tatu ya dunia itokee (Ya Nuclear itapendeza) kati ya USA na China

Hizo Global powers na washirika wake watwangane

Bila kuihusisha Africa after War

Civilization itaanza upya, ila this time tukiwa on the top

Juzi tu, Tanzania na China zilikua level moja ya uchumi, now China (Nchi moja) ina jeuri ya kutoa msaada Africa nzima

Serious?
 
Hela za wachina ni kama zile za wakopesha hela kwa riba kubwa ili wauze nyumba. Nasikia wanataka kuchukua kiwanja cha ndege cha Entebbe hapo Uganda Wachina walikua wale rafiki zake Mwalimu Nyerere sio hawa wa sasa hivi ma capitalists tu.
 
Back
Top Bottom