China kujenga kambi za kijeshi ndani ya Tanzania na Kenya

S V Surovikin

JF-Expert Member
Aug 8, 2015
13,616
32,723
China 'kujenga' kambi za kijeshi Tanzania na Kenya
Jeshi la China
e801a8a2-050e-4b5c-8b99-d1e3352969af.jpg

Getty ImagesCopyright: Getty Images
China inafikiria kujenga kambi za kijeshi katika nchi nne za Afrika, kwa mujibu wa ripoti ya idara ya ulinzi ya Marekani.

Tanzania, Kenya, Ushelisheli na Angola zimetajwa kuwa miongoni mwa nchi kadhaa ambazo China inapania kujenga kambi za kijeshi.

Serikali za nchi hizo nne za Afrika zilizotajwa na Marekani hazijatoa tamko lolote kuhusiana na suala hilo.

Ripoti hiyo iliyochapishwa wiki iliyopita imeangaziwa sana na vyombo vya habari wikendi iliopita, huku baadhi ya nchi ambazo kambi hizo zitajengwa zikikanusha kufanya mazungumzo na China.

"Kando na kambi yake ya sasa nchini Djibouti, Jamhuri ya watu wa China ina mpango wa kuongeza kambi zake za kijeshi ughaibuni kusaidia vikosi vya majini, angani na ardhini," sehemu ya ripoti hiyo ilisema.

Pia imeongeza kuwa China huenda ameamua sehemu itakapojenga vituo vyake vya kijeshi nchini Myanmar, Thailand, Singapore, Indonesia, Pakistan, Sri Lanka, Umoja wa Falme za Kiarabu,(UAE), Kenya, Ushelisheli, Tanzania, Angola, na Tajikistan.
 
China 'kujenga' kambi za kijeshi Tanzania na Kenya
Jeshi la China
View attachment 1561440
Getty ImagesCopyright: Getty Images
China inafikiria kujenga kambi za kijeshi katika nchi nne za Afrika, kwa mujibu wa ripoti ya idara ya ulinzi ya Marekani.

Tanzania, Kenya, Ushelisheli na Angola zimetajwa kuwa miongoni mwa nchi kadhaa ambazo China inapania kujenga kambi za kijeshi.

Serikali za nchi hizo nne za Afrika zilizotajwa na Marekani hazijatoa tamko lolote kuhusiana na suala hilo.

Ripoti hiyo iliyochapishwa wiki iliyopita imeangaziwa sana na vyombo vya habari wikendi iliopita, huku baadhi ya nchi ambazo kambi hizo zitajengwa zikikanusha kufanya mazungumzo na China.

"Kando na kambi yake ya sasa nchini Djibouti, Jamhuri ya watu wa China ina mpango wa kuongeza kambi zake za kijeshi ughaibuni kusaidia vikosi vya majini, angani na ardhini," sehemu ya ripoti hiyo ilisema.

Pia imeongeza kuwa China huenda ameamua sehemu itakapojenga vituo vyake vya kijeshi nchini Myanmar, Thailand, Singapore, Indonesia, Pakistan, Sri Lanka, Umoja wa Falme za Kiarabu,(UAE), Kenya, Ushelisheli, Tanzania, Angola, na Tajikistan.
Tanzania wasahau kabisa. Marais wa Marekani walikuja karibia wote kila mmoja kwa wakati wake kuomba hilo suala lakini JWTZ walikataa katu katu ! Hapa huwa naiona Tz yetu ambayo sisi wananchi wake tunaichukulia poa huko nje tuna msimamo kwenye masuala ya kijeshi!!
 
Tanzania wasahau kabisa. Marais wa Marekani walikuja karibia wote kila mmoja kwa wakati wake kuomba hilo suala lakini JWTZ walikataa katu katu ! Hapa huwa naiona Tz yetu ambayo sisi wananchi wake tunaichukulia poa huko nje tuna msimamo kwenye masuala ya kijeshi!!
Safari ya China itajengwa!kumbuka ni marafiki wetu kwelikweli 😂😂hata Amerika alikataliwa kwasababu ya ushawishi wa Best wetu China
 
Safari ya China itajengwa!kumbuka ni marafiki wetu kwelikweli hata Amerika alikataliwa kwasababu ya ushawishi wa Best wetu China
Ni kama unataka kunishawishi we jamaa maana kuna warships/destroyers kadhaa zimenunuliwa toka China mwaka huu huu, zilikuja baada ya order ya zile airbus helicopters kama ile ilobeba Mwili wa Mkapa! Huu urafiki huu....
 
Ni kama unataka kunishawishi we jamaa maana kuna warships/destroyers kadhaa zimenunuliwa toka China mwaka huu huu, zilikuja baada ya order ya zile airbus helicopters kama ile ilobeba Mwili wa Mkapa! Huu urafiki huu....
China ina mizizi ndani ya nchi yetu kuliko Marekani. Hata viongozi wetu wanatamani kucopy mambo ya kisiasa kutoka kwa wakomunisti.... Tukienda na mwendo huu huu lazima mabeberu watutandike vikwazo kwa kumchagua China kama bwana wetu
 
Tutakuwa watu wa ajabu sana kukubali ujinga huo!

Najua Wachina watakuja na mihela kibao na kuhonga wanasiasa wetu, watu wenye ushawishi kwenye jamii, waandishi wa habari n. k ili kufanikisha hilo

Wataleta visafari kibao kupeleka watu China na kuwaweka kwenye hoteli nzurinzuri ili kulainishwa baadae waunge mkono mipango hiyo!

Naionya serikali ya Tanzania na nchi za afrika mashariki zisikubali ujinga huu. Haya majeshi ndo yatatumika kulinda maslahi ya wachina humu Afrika na yatasaidia kulinda mpango wa China wa kupopulate nchi hizi kwa kuleta mamilioni ya wachina. Hutoweza kuwagusa kwa sababu watakuwa na kambi za kijeshi zinazoweza kublackmail serikali zetu.

Kamwe tusikubali kuruhusu ujenzi wa kambi ya nchi yoyote hapa kwetu, Tutageuka kuwa Client State/Sattelite state na itakwamisha malengo yetu ya Kuunganisha Africa mashariki na Africa nzima kiujumla!
 
Wajenge kambi za kijeshi Afrika nzima ila sio Tanzania 🇹🇿 huu ushubwada hatuutaki awe marekani awe China hatutaki Kambi ya kisheji ya Kigeni
 
Watajenga kwenye jimbo lao jipya la kenya, hapo marekani anabweka tu maana anajua analetewa base mpya na lazima itajengwa maana kenya haiwezi kupindua takwa la china..... Kenya itageuka kama lebanon sasa.. kila nchi itaweka base hapo.
 
Pia imeongeza kuwa China huenda ameamua sehemu itakapojenga vituo vyake vya kijeshi nchini Myanmar, Thailand, Singapore, Indonesia, Pakistan, Sri Lanka, Umoja wa Falme za Kiarabu,(UAE), Kenya, Ushelisheli, Tanzania, Angola, na Tajikistan.
Aisee . . . the rise of the mighty China. Marekani wanaogopa kichizi hizi moves za China
 
Watajenga kwenye jimbo lao jipya la kenya, hapo marekani anabweka tu maana anajua analetewa base mpya na lazima itajengwa maana kenya haiwezi kupindua takwa la china..... Kenya itageuka kama lebanon sasa.. kila nchi itaweka base hapo.
Hahaha . . . Kenya kuwa Lebanon ? Siyo rahisi kiivyo
 
Hahaha . . . Kenya kuwa Lebanon ? Siyo rahisi kiivyo

Mkuu, hapo kuifananisha kenya na Lebanon sijui umeelewa vipi, ila tambua US ana base kenya tayari, China ana possibility kubwa ya kuweka base kenya maana ni kama jimbo lao hapo kenya haiwezi kupindua takwa la China kutokana na mikopo yao na collateral za mirani, British kuingia hapo kenya ndio kama nyumbani tu. Sasa huoni tayari kuna mgongano wa kimaslahi wa hizi block mbili east na west? Uzandiki na ujasusi utakaokuwa unachezeka hapo utakuwa sio wa kitoto.. na itakuwa base ya kenya inatumika kutafuta influence ya maeneo mengine ukanda huu.
 
Back
Top Bottom