S V Surovikin
JF-Expert Member
- Aug 8, 2015
- 13,616
- 32,723
China 'kujenga' kambi za kijeshi Tanzania na Kenya
Jeshi la China
Getty ImagesCopyright: Getty Images
China inafikiria kujenga kambi za kijeshi katika nchi nne za Afrika, kwa mujibu wa ripoti ya idara ya ulinzi ya Marekani.
Tanzania, Kenya, Ushelisheli na Angola zimetajwa kuwa miongoni mwa nchi kadhaa ambazo China inapania kujenga kambi za kijeshi.
Serikali za nchi hizo nne za Afrika zilizotajwa na Marekani hazijatoa tamko lolote kuhusiana na suala hilo.
Ripoti hiyo iliyochapishwa wiki iliyopita imeangaziwa sana na vyombo vya habari wikendi iliopita, huku baadhi ya nchi ambazo kambi hizo zitajengwa zikikanusha kufanya mazungumzo na China.
"Kando na kambi yake ya sasa nchini Djibouti, Jamhuri ya watu wa China ina mpango wa kuongeza kambi zake za kijeshi ughaibuni kusaidia vikosi vya majini, angani na ardhini," sehemu ya ripoti hiyo ilisema.
Pia imeongeza kuwa China huenda ameamua sehemu itakapojenga vituo vyake vya kijeshi nchini Myanmar, Thailand, Singapore, Indonesia, Pakistan, Sri Lanka, Umoja wa Falme za Kiarabu,(UAE), Kenya, Ushelisheli, Tanzania, Angola, na Tajikistan.
Jeshi la China
Getty ImagesCopyright: Getty Images
China inafikiria kujenga kambi za kijeshi katika nchi nne za Afrika, kwa mujibu wa ripoti ya idara ya ulinzi ya Marekani.
Tanzania, Kenya, Ushelisheli na Angola zimetajwa kuwa miongoni mwa nchi kadhaa ambazo China inapania kujenga kambi za kijeshi.
Serikali za nchi hizo nne za Afrika zilizotajwa na Marekani hazijatoa tamko lolote kuhusiana na suala hilo.
Ripoti hiyo iliyochapishwa wiki iliyopita imeangaziwa sana na vyombo vya habari wikendi iliopita, huku baadhi ya nchi ambazo kambi hizo zitajengwa zikikanusha kufanya mazungumzo na China.
"Kando na kambi yake ya sasa nchini Djibouti, Jamhuri ya watu wa China ina mpango wa kuongeza kambi zake za kijeshi ughaibuni kusaidia vikosi vya majini, angani na ardhini," sehemu ya ripoti hiyo ilisema.
Pia imeongeza kuwa China huenda ameamua sehemu itakapojenga vituo vyake vya kijeshi nchini Myanmar, Thailand, Singapore, Indonesia, Pakistan, Sri Lanka, Umoja wa Falme za Kiarabu,(UAE), Kenya, Ushelisheli, Tanzania, Angola, na Tajikistan.