Chiku Abwao ajiunga rasmi na ACT - Wazalendo

Chiku Abwao ajiunga rasmi na ACT - Wazalendo

CDM mmeshuka thamani haraka sana make hata huku mtaani watoto watakuwa wanawacheka sana ..hii ndo inaitwa kuvua nguo ukaamua kujifunika majani ya miti
 
safi sana japo ulipoenda sawa na bulaya malengo yako adi mwaka 2035,
 
Hivi Huyo mama mbona amechelewa sana angewahi ACT walikuwa wanatafuta mgombea urais mwanamke
 
Mie(in jk's voice) ni mfuatiliaji mzuri sana wa bunge ila sijapata kumsikia huyo mama...kwanza ndio nimemjua leo
 

Chiku-28July2015.jpg



Aliyekuwa Mbunge wa Viti Maalumu mkoani Iringa kupitia Chama cha Demokrasia na Maendeleo( Chadema), Chiku Abwao, amehamia chama cha nne cha siasa, baada ya jana kujiunga na ACT-Wazalendo.

Abwao alijiunga na chama hicho na kutangaza nia ya kugombea ubunge katika jimbo la Iringa Mjini.
Alisema amesukumwa na dhamira njema ya kuendelea kuwatumikia wananchi wa mkoa huo.

Abwao aliwahi kuwa mwanachama na kiuongozi katika vyama vya CCM, baadaye kuwa mbunge wa viti maalum NCCR-Mageuzi na jana alijiunga na chama cha nne.

Akikabidhiwa kadi na Katibu wa Mipango, Mkakati ACT-Wazalendo, Mchange Habibu, jana jijini Dar es Salaam, Abwao alidai kuwa historia ya kuhama kutoka chama kimoja hadi kingine inatokana na vyama alivyotoka kushindwa kupambana na ufisadi na umaskini.

“Umaskini uliopo nchini unasababishwa na viongozi waliopo chama tawala, ndiyo maana nikahamia vyama vya upinzani tangu miaka ya 90, lakini dhamira yao inabadilika na hawana nia tena ya kupambana na ufisadi pamoja na kuwa na uongozi bora. ACT-Wazalendo ni chama sahihi,” alidai Abwao.

Alisema kuwa yeye ni mpambanaji ambaye kutokana na kuwa katika siasa kwa kipindi kirefu, na imani yake ni kuhakikisha anawatumikia vyema wananchi baada ya kuwa mbunge aliyegombea tofauti na awali alipokuwa mbunge wa viti maalum.

“Kabla sijaamua kujiunga na chama hiki, nilisoma ilani yao, katiba na Azimio la Tabora nikagundua huku kuna nia ya dhati ya kutupeleka Watanzania katika mabadiliko ya siasa safi, na niueleze umma kuwa sijaingia ACT-Wazalendo kwa kubahatisha na kwa kufuata upepo kama bendera,” alisema Abwao.



CHANZO: NIPASHE

 
jamani muwe mnaangalia HABARI .....HII NAYO NI HABARI.........? HUYU NA MREMA WANATOFAUTI GANI.......?
Wakuu habari yenu,

Mbunge viti maalum Iringa Mjini mh. Chiku Abwao amejiunga rasmi ACT-Wazalendo.

Chanzo: ITV Habari

View attachment 271585
Katibu wa Mipango na mikakati wa ACT-Wazalendo,Habib Mchange akimkabidhi kadi ya mwanachama,aliyekuwa mbunge wa viti maalum Iringa Mjini mh. Chiku Abwao baada ya kujiunga rasmi na ACT-Wazalendo

View attachment 271586


View attachment 271587
Mh. Chiku Abwao akiongea na waandishi wa habari,makao makuu ACT-Wazalendo


View attachment 271588
Sehemu ya waandishi wa Habari.
 
Chiku Abwao,wewe nenda salama,lakini kilichosababisha ni mkubwa wa wangombe wapya,umeona huwezi kupita kwenye kura za maoni,
 
Chiku Abwao,wewe nenda salama,lakini kilichosababisha ni mkubwa wa wangombe wapya,umeona huwezi kupita kwenye kura za maoni,

Sidhani kama unayeongea ni kweli unafuatilia siasa hapa nchini kwa undani zaidi au huenda ni changa kwenye siasa huyo mama ni mmoja ya kinamama wakwanza kimageuzi hapa nchini na amefanya mengi sana kwenye ulimwengu wa siasa na kaisaidia sana chadema Kanda ya kusini na istoshe amechangia sana kumfikisha Mchungaji Peter msigwa hapo alipo kupitia chadema ..Fuatilia utaniambia kuwa huyo ni mpambanaji haswaa mi ni mwana CCM ila kwa wachapakazi wa kweli lazima niseme ukweli na Hata Zitto anatambua uzito wa huyo mama..! Hauwezi kuzungumzia historic ya mageuzi Tanzani Bila kumtaja CHIKU ABWAO..MREMA NA TIMU YAKE YOTE HAPA NCHINI...kama wewe kweli ni mfuatiliaji wa siasa kiundani na sio ushabiki..
 
Mkuu yani huyo ni boya tu hana mchango wowote.

Fuatilia siasa acha ushabiki kiukweli hata mimi Kada wa CCM nakushangaa kwa kauli yako nyepesi sana tena ya kitoto sana! Na istoshe inaonesha haujua historia ya Chadema.. Amechangia sana kukiinua kile chama na kumbuka CHIKU ABWAO alikiw na nyadhfa gani chadema Toka ajiunge nacho ndio ungejua hata uzito wake ni sio kuropoka vitu usivyovijua..! Usioneshe uchanga wa elimu kisiasa kaka..! Huyo ndio aliyekuwa miongoni mwa viongozi wajuu kabisa kwa kina mama CHADEMA..! NA nyadhfa zingine nyingi katika chama.. Amekisaidia sana kwa kweli Ingawa ni vigumu asiyemfuatiliaji kutambua..Coz Wapo viongozi waneno na wa uchapakazi lazima ujue Hilo..!
 
anasema eti asingekuwa yeye mchungaji peter msigwa asingeshinda ubunge 2010!!na kama angekuwa ana tamaa yeye ndio angekuwa mbunge wa iringa mjini, amechoka na siasa za visasi za tindu lisu!!! acha mizigo ipungue, na wabunge wengi wa viti maalum wa cdm walikuwa ni mizigo tu kama tindu lisu alivyowahi kusema.

Agombee Ubunge sasa Iringa mjini Ashinde kama ana uwezo
 
Fuatilia siasa acha ushabiki kiukweli hata mimi Kada wa CCM nakushangaa kwa kauli yako nyepesi sana tena ya kitoto sana! Na istoshe inaonesha haujua historia ya Chadema.. Amechangia sana kukiinua kile chama na kumbuka CHIKU ABWAO alikiw na nyadhfa gani chadema Toka ajiunge nacho ndio ungejua hata uzito wake ni sio kuropoka vitu usivyovijua..! Usioneshe uchanga wa elimu kisiasa kaka..! Huyo ndio aliyekuwa miongoni mwa viongozi wajuu kabisa kwa kina mama CHADEMA..! NA nyadhfa zingine nyingi katika chama.. Amekisaidia sana kwa kweli Ingawa ni vigumu asiyemfuatiliaji kutambua..Coz Wapo viongozi waneno na wa uchapakazi lazima ujue Hilo..!

Hamna kitu boya ni boya tu, aonyeshe umwamba wake akagombee jimbo tujue kweli yeye ni jembe na kuna dalili hata viti maalum hawezi kupata... Hope dawa itafanya kazi.
 
Hamna kitu boya ni boya tu, aonyeshe umwamba wake akagombee jimbo tujue kweli yeye ni jembe na kuna dalili hata viti maalum hawezi kupata... Hope dawa itafanya kazi.
Aoneshe Mara mgapi na amesha sema anagombea teyari hiyo peke Yake ni ushindi toshaa kutoka na kupambana moja kwa moja..! Ashinde asi shinde bado kapambana na kaonesha dhamira na msimamo wake na kwa Hilo ataheshimika kisiasa koz ameshihirisha dhamira yake..Ndivyo mwanasiasa anavyotakiwa awe...! Haihitaji political science kujua hata hili..! Jambo linalokufanya wewe uwe boys na boys zaidi..! Kwa uchanga kimtazamo na mimawazo pia..! Yaonesha wewe ni benders fuata upepo no research huna facts na wala haujui siasa za bongo.. Kazana Sanaa.. Huwo ni mwanzo mzuri sana kwako.
 
Aoneshe Mara mgapi na amesha sema anagombea teyari hiyo peke Yake ni ushindi toshaa kutoka na kupambana moja kwa moja..! Ashinde asi shinde bado kapambana na kaonesha dhamira na msimamo wake na kwa Hilo ataheshimika kisiasa koz ameshihirisha dhamira yake..Ndivyo mwanasiasa anavyotakiwa awe...! Haihitaji political science kujua hata hili..! Jambo linalokufanya wewe uwe boys na boys zaidi..! Kwa uchanga kimtazamo na mimawazo pia..! Yaonesha wewe ni benders fuata upepo no research huna facts na wala haujui siasa za bongo.. Kazana Sanaa.. Huwo ni mwanzo mzuri sana kwako.

Kwikwikiw jipe moyo chiku abwao comment yako imeonyesha jinsi ulivyokamia ubunge, pole sana.
 
Back
Top Bottom