kadoda11
JF-Expert Member
- Jan 6, 2011
- 21,453
- 20,712
Mimi ni shabaki wa kipindi chako cha The Chidy Benz Show kinachochorushwa na Eatv.Kwa mda sasa nimekuwa nikifatilia show yako,ila kuna wakati huwa naikosa kutokana na majukumu ya kikazi.Mda nilioitazama na kukuona ukizungumza,kuna jambo ambalo si vibaya tukikukosoa ili ujirekebishe.Linahusu uzungumzaji wako.Ukianza kuzungumzia jambo fulani unazungumza kama unabwabwaja bila nukta.Uzungumzaji wako wa hovyo hovyo unapelekea ushindwe kueleweka kirahisi.Unapoteza point ya msingi ya jambo unalozungumzia.Pia tabia yako ya kuvuta sigara mbele ya camera sio jambo zuri.Waungwana wanakuona mshamba.Unawafundisha nini vijana na watoto wanaotazama show yako?.Wale wanao unda zile sigara wanakulipa?.Umeingia nao mkataba wa kutangaza bidhaa yao katika show yako?.Kama sivyo basi uache kuvuta sigara mbele ya camera zinazo shoot show yako.Au ingia mkataba wa kibiashara na waundaji wa sigara ili utakapo anza kuugua maradhi yanayo sababishwa na uvutaji,uwe na pesa ya kutosha kujitibu.tembelea hapa upate elimu kidogo kuhusu madhara yatokanayo na uvutaji sigara:Madhara ya kuvuta sigara - Wikipedia, kamusi elezo huru.