Cheo ni dhamana, tuwe na busara

Cheo ni dhamana, tuwe na busara

Kinachotokea sasa kwa viongozi vijana akina sabaya, makonda n.k. ni fundisho tosha kwa vijana wenye kuwa na ndoto za kuwa viongozi na smbao tyr ni viongozi. Taifa letu lilikuwa linaelekea kuzalisha viongozi wa ovyo wasio na maadili na wasiofuata misingi ya utawala bora. Ni bahati mbaya sana bado sheria na katiba za nchi zinaruhusu ukiukwaji wa misingi ya utawala bora ikiwemo watu kuwekwa gerezani holela n.k. matumizi mabaya ya vyombo vya usalama.
Wote ni uvccm kuna chuo wanapitia kabla
 
Sasa hapo Mungu anahusikaje?

Ccm itaendelea kutawala hii nchi hata miaka 100 ijayo maana ujinga bado ni tatizo kubwa sana Tanzania.
Kutawala CCM sio shida..., mbona sasa hivi angalau tunapumua na tunatawaliwa na hiyo CCM?


Nadhani tunaelewana...
 
Ila kale kabwana kaongooo!Sasa kudanganya kwamba anafufua watu maana yake nini?Alipigwa dongo bungeni akauchuna kama si yeye!🤣🤣🤣🤣🤣
Alitakiwa march ndio aonyeshe miujiza sasa afufue mtu, ila kauchuna kama sio yeye
 
Ali Hapi anaiogopa Twitter kama ukoma

Bashiru Ali is a dead man walking...
Waliokuwa bize kuuwa upinzani wengine tushawazika wengine wapo jela wengine wanachezea tumbuzi. Tuliomba Mungu awaaaibishe wote waliochezea uchaguzi Mkuu mikono juu.Tumeuona ukuu wa Mungu
 
Wenzetu waliona mbali sana watu washamba na masikini awafai kupewa madaraka watalewa. Maana madaraka ni sawa na Siti ya daladala usiweke kishoka kwenye daladala,we ni abiria na sio mmiliki
 
Hao vijana ni ibilisi kabisa, sijui Bashite wanamsubirisha vipi kumkamata.
 
Kuna hili la majambazi kuteka mabasi na kuwapora abiria lilisha sahaulika kabisa lakini ghafla bin vuu twaliona tena
Na naogopa sana kama kashfa za rushwa na wizi wa waziwazi wa mali za umma na za wale wanaowekeza utaendelea kuwepo. Kuna mambo inabidi yaishe sasa. Tutafute maendeleo kwa nguvui zetu zote.
Nchi hii ni yetu sote.. Sio ya watu wachache au kikundi cha watu fulani
 
Nilifikiri unaongelea ccm kutolewa madarakani kumbe kina Makonda?

Kama ni hivyo sijaona ukiwataja kina Lema au Sugu ambae alijita rais wa Mbeya na leo Lema yuko ukimbizini
 
Leo Magufuli hayupo

Makonda sio tena mtu wa kuogopwa na mtu kama PM na Siro.

Chalamila sio mtu wa kuchapa watoto wa watu viboko na kuwatisha wazazi wao.

Kelele za Mambosasa na Mruto hazipo tena.

Mabavu ya Sabaya leo ananyea ndoo na kulala saa 12 kama kuku gerezani.

Dunia uwanja wa Fujo lakini ardhi ya Mwenyezi Mungu tuikanyage kwa tahadhari sana.

Mungu atabaki kuwa fundi wa mafundi wote duniani.
Ubarikiwe sana Mkuu kwa kutumbusha kuwa tuwe watu wenye Unyenyekevu.
 
Leo Magufuli hayupo

Makonda sio tena mtu wa kuogopwa na mtu kama PM na Siro.

Chalamila sio mtu wa kuchapa watoto wa watu viboko na kuwatisha wazazi wao.

Kelele za Mambosasa na Mruto hazipo tena.

Mabavu ya Sabaya leo ananyea ndoo na kulala saa 12 kama kuku gerezani.

Dunia uwanja wa Fujo lakini ardhi ya Mwenyezi Mungu tuikanyage kwa tahadhari sana.

Mungu atabaki kuwa fundi wa mafundi wote duniani.
Ukishupaza shingo mbele za Mungu linakatika
 
Back
Top Bottom