MwanajamiiOne
Platinum Member
- Jul 24, 2008
- 10,470
- 6,588
Nchi zingine unapopanda public bus (au commuter) unatakiwa huwe na change kamili. Kama huna utakachopata ni ticket ikionyesha kuwa unadai kiasi fulani cha pesa, na ukiuliza utaambiwa ukachukuwe change yako makao makuu ya hiyo kampuni.
Kuepusha usumbufu mwenyewe utatafuta change mapema.
Makonda wengi wa daladala wanakuwa wamehajiriwa, na matajiri wa hayo mabasi na huwa hawawapi change wanapo anza kazi asubuhi, usishangae hata pesa ya mafuta ya kuendeshea hayo mabasi ni jukumu la dereva na kondakta wa siku hiyo.
Ni jukumu la abiria kutafuta change kamili, na litaepusha usumbufu na matusi ya asubuhi subuhi.
Jiulize kwanza wewe ni konda umeanza kazi na huna hizo change na abiria kama wawili hivi anakwupa noti za elfu kumi kumi, utafanyaje?
Nakuunga mkono kabisa katika hili. Lakini pia kuna wale abiria ambao haweki nauli yake karibu hadi konda adai ndo ataanza kusukumana na abiria wengine katika harakati za kuitafuta hiyo nauli hivi kuna ugumu gani mtu kupanda daladala ukiwa na nauli yako mkononi au sehemu ya karibu?
Sometimes ndo mana tunafuatwa na vibaka wanatupora mabegi/ wallets maana mtu hadi afungue lipochi lote kibaka anaona simu, nyekundu anaziona n.k