Chenji na karaha za konda

Chenji na karaha za konda

Herbalist Dr MziziMkavu

Platinum Member
Joined
Feb 3, 2009
Posts
43,067
Reaction score
34,829
UTUMWA mwingine wa ajabu sana, viburi vya makondakta vimewafanya watu sasa wanapotoka kazini kabla ya kufika nyumbani waanze kuchenji kwenye maduka ya jirani noti zao. Unajua kwa nini? Wanaogopa matusi ya makondakta asubuhi, bila hiyana makonda wengi wamekuwa wanatoa matusi kwa watu wanaotoa manoti kama Ntenze au wekundu wa Msimbazi.

Unakumbuka Nteze John alikuwa mchezaji wa Pamba na Simba miaka ya 90 akilisakata kabumbu nambari 10 hadi noti ya Sh 10,000 ikabatizwa jina la Nteze.

Wasiofahamu msamiati huo wawaulize wanahabari ni mabingwa wa kuutumia. Wanautumia wakati gani, sina jibu lakini Nteze ni moja ya lugha zao kubwa wanazozitumia katika utekelezaji wa majukumu yao ya kila siku.

Wanayo misamiati mingi mara kiasi cha vumbi, changarawe na kiasi cha lami, nisiendelee mbele wasije wakaona nawasakama bure. Sasa ukitaka kujua hasira ya konda wakati wa asubuhi wewe mpe hiyo Nteze au tu mpe nusu Nteze uone, atakakusakama hadi siku utaianza vibaya.

Akikusamehe sana atakusonya bila kificho. Ataanza ‘kwa nini utoe fedha kubwa asubuhi hii, yaani wewe unapotoka nyumbani kwa nini usijiandae kuchenji fedha yako au unataka kupanda bure”.

Maneno kama hayo yatamtoka kondakta kana kwamba una ugomvi naye. Mara nyingi anatafuta sapoti ya abiria wengine. Sasa ukute abiria wasio na ustaarabu nao watadakia, aha! Watu wengine bwana wasumbufu kweli asubuhi yote hii kwa nini atoe Nteze.

Fedha yako na nauli umetoa, lakini matusi yanakuandama. Juzi kwa macho yangu nimemshuhudia abiria aliyekuwa anashukia kituo cha Kongo akitoa noti ya Sh 5000, konda akakataa kumrudishia chenji yake kwa madai kuwa hakuwa nayo. “Kaka twende hadi mwisho wa safari ndo nitachenji wewe unatoa noti unafikiria mimi nitatoa wapi chenji asubuhi hii.”

Kijana akawa mpole, akawa hana budi akaendelea na safari aliyolazimishwa hadi Mnazi Mmoja. Konda akachenji kijana akaanza safari ya kupiga mguu kurudi Kariakoo. Hiyo ndio biashara ya usafiri wa Bongo ni karaha tupu! Hebu tujiulize hivi nani mwenye jukumu la kutafuta chenji ni la abiria au la kondakta. Sio kwamba nawapendelea abiria lakini jukumu lake ni kutoa nauli.

Kondakta anajua fika kuna abiria watatoa Nteze ni jukumu lao kuwa na chenji. Abiria anyongwe kama hana nauli lakini sio atoke kazini kachoka aanze tena kutafuta chenji, huo ni utumwa na unyanyasaji. Abiria kataeni kuburuzwa na makondakta wachacharike kuhakikisha wanakuwa na chenji.
http://www.habarileo.co.tz/safu/?n=3320
 
Kweli wanakera sana!! Wangekuwa makini na biashara yao, chenji ya jana yake wangeamka nayo ili waanze nayo asubuhi. Lakini cha ajabu asubuhi wanaanza kazi mikono mitupu! Halafu pamoja na uzoefu wa kupewa 'Nteze' asubuhi bado hawabadiliki! Siamini kama kuna abiria anafanya makusudi kutoa hela kubwa, kuna wakati unakuwa huna kabsaa hela ndogo!!
 
Uzuri wa abiria ni kabla ya kupanda kwenye daladala...ukishapanda wewe ni adui nambari wani...!
 
Ni kweli kabisa hawa makonda ni Mafisadi Wadogo,Nashauri Ukonda iwe taaluma ya kusomea ili kupunguza hii kero ya makonda.
 
Ni kweli kabisa hawa makonda ni Mafisadi Wadogo,Nashauri Ukonda iwe taaluma ya kusomea ili kupunguza hii kero ya makonda.

.........NI KWAMBA HAWAJIJUI WAO NI NANI NA WANAFANYA NINI,LABDA TUWAAMBIE KUWA WAO NI MAMENEJA MAHUSIANO AU AFISA MAUZO.
Chakufanya ni kuanzisha usafiri wa mabasi yaendayo kasi na tiketi kuwa zinauzwa kwenye vituo maalumu na kukuwezesha kununua tiketi za hadi mwaka mmoja.
Kuanzia hapo,konda na wapiga debe watakula jeuri yao.
 
harafu hawa makonda kweli hawana Adabu hata kidogo ,mie nadhani wawe wanpewa elimu ya kazi yao kwanza la ndo maana sie tusiokuwa na personal transport tunapata tabu sana
 
Na nyie abiria nimewashtukia wewe unajua kesho unawahi kazini badala kuwa na pesa kamili na utakuta lijitu lina jero kabisa mfukoni linatoa Msimbazi 10,000/= ili Konda ashindwe chenji lipande bure sio vizuri hivyo.
 
solution ni treni za umeme tu,*** makonda,*** daladala
 
Hilo Treni utalipitishia wapi bana?
Wameshindwa kuboresha reli ya kati ndo walete mjini hapa?

hilo sio tatizo letu.hiyo tenda wakipewa kampuni kama siemen,wao watajua lipite wapi.inawezekana.
 
hilo sio tatizo letu.hiyo tenda wakipewa kampuni kama siemen,wao watajua lipite wapi.inawezekana.


Mimi naamini sana kuwa uwezo wa kutumia treni kwa hapa mjini unawezekana. Njia ya treni imepita mpaka mjini hasa kwa watu wa Gongo la mboto. Inaweza ikawa inapita mara mbili asubuhi, na mara mbili jioni.....ADHA YA USAFIRI ITAPUNGUA KIASI FULANI...

HII NI CHALLENGE KWA SERIKALI, NAAMINI WENYE DHAMANA NA USAFIRI WANATUSIKIA...
 
hilo sio tatizo letu.hiyo tenda wakipewa kampuni kama siemen,wao watajua lipite wapi.inawezekana.

Kwa nini watendaji wa serikali wanasua sua katika maamuzi.
Wamekuja na mradi wa mabus yaendayo kasi wamebomoa nyumba Kimara mwisho pale miaka inaenda na pesa wajanja wanatia mfukoni utasikia upembuzi yakinifu unafanyika.
 
Jamani hawa makonda sijui wana nini,nakumbuka siku moja asubuhi nilitoa 5000 wakat naenda kazini akaanza kugomba nikamwuliza hivi unanigombezea nini je ningepanda halafu nikakwambia sina nauli ingekuwaje nakupa pesa na bado unanigombeza,alivyoona na mimi namjia juu akaniambia na utazunguka na hii gari mpaka chenji itakapo patikana nikamwambia sizunguki na nikifika kituo nachotakiwa kushuka nitashuka ukirudi utanikuta nakusubiri nikiwa na askari na utarudisha pesa zaidi ya hiyo uliotakiwa kunirudishia kusikia hivyo mbona alianza kutafuta chenji,na akapata na nikashuka kwenye kituo nilichotakiwa kushuka,wakati mwingine akiwa mbogo na sisi abiria tunapaswa kuwa wakali akiona hivyo atatafuta chenji lakini akikugombeza ukanyamaza anakuona wewe ni mnyonge wake.
 
Unataka uniambie Msindima jana yake wakati unanua mahitaji yako ulimaliza pesa zote ndogo ndogo au ulitaka jamaa akusamehe kwa kutoa noti kubwa? Sio vizuri hivyo unapo jua kesho unajihimu kwa nn usitenge pesa ndogo ya nauli utakuta mtu anaacha nyumbani anatoa wekundu au hilo dala.
 
Jamani hawa makonda sijui wana nini,nakumbuka siku moja asubuhi nilitoa 5000 wakat naenda kazini akaanza kugomba nikamwuliza hivi unanigombezea nini je ningepanda halafu nikakwambia sina nauli ingekuwaje nakupa pesa na bado unanigombeza,alivyoona na mimi namjia juu akaniambia na utazunguka na hii gari mpaka chenji itakapo patikana nikamwambia sizunguki na nikifika kituo nachotakiwa kushuka nitashuka ukirudi utanikuta nakusubiri nikiwa na askari na utarudisha pesa zaidi ya hiyo uliotakiwa kunirudishia kusikia hivyo mbona alianza kutafuta chenji,na akapata na nikashuka kwenye kituo nilichotakiwa kushuka,wakati mwingine akiwa mbogo na sisi abiria tunapaswa kuwa wakali akiona hivyo atatafuta chenji lakini akikugombeza ukanyamaza anakuona wewe ni mnyonge wake.
Nchi zingine unapopanda public bus (au commuter) unatakiwa huwe na change kamili. Kama huna utakachopata ni ticket ikionyesha kuwa unadai kiasi fulani cha pesa, na ukiuliza utaambiwa ukachukuwe change yako makao makuu ya hiyo kampuni.

Kuepusha usumbufu mwenyewe utatafuta change mapema.

Makonda wengi wa daladala wanakuwa wamehajiriwa, na matajiri wa hayo mabasi na huwa hawawapi change wanapo anza kazi asubuhi, usishangae hata pesa ya mafuta ya kuendeshea hayo mabasi ni jukumu la dereva na kondakta wa siku hiyo.

Ni jukumu la abiria kutafuta change kamili, na litaepusha usumbufu na matusi ya asubuhi subuhi.

Jiulize kwanza wewe ni konda umeanza kazi na huna hizo change na abiria kama wawili hivi anakwupa noti za elfu kumi kumi, utafanyaje?
 
ni vyema kusaidiana katika kazi kama unaweza kupata chenji kutoka nyumbani fanya hivyo basi.
 
Unataka uniambie Msindima jana yake wakati unanua mahitaji yako ulimaliza pesa zote ndogo ndogo au ulitaka jamaa akusamehe kwa kutoa noti kubwa? Sio vizuri hivyo unapo jua kesho unajihimu kwa nn usitenge pesa ndogo ya nauli utakuta mtu anaacha nyumbani anatoa wekundu au hilo dala.

Fidel80,nilitaka huyo konda anisamehe ili?Sometimes it happens kwamba umemaliza chenji zote kwa hiyo ningefanyeje?au ulitaka nisipande gari kwa kuwa nilikua na pesa kubwa? Elewa hili mpaka nifike napofanyia kazi napanda daladala mbili na pesa ndogo ya chenji niliokua nayo tayari nilishalipia kwenye daladala ya kwanza niliopanda kwa hiyo ulitaka nisipande gari kwa kuwa nina pesa kubwa?
Hivi wewe huwa siku zote unakuwa na chenji? nijibu hilo swali halafu nitakuuliza lingine.
 
ni vyema kusaidiana katika kazi kama unaweza kupata chenji kutoka nyumbani fanya hivyo basi.

Naungana na wewe ni vyema kusaidiana katika kazi lakini kuna wakati unajikuta huna chenji ndogo sasa hapo utafanyaje?
 
harafu hawa makonda kweli hawana Adabu hata kidogo ,mie nadhani wawe wanpewa elimu ya kazi yao kwanza la ndo maana sie tusiokuwa na personal transport tunapata tabu sana

Tena hawaelewi hata maana ya public transport. Konda anamtreat vibaya abiria wake as if ni mfungwa na nyapala. "kaa vizuri kule,rudi nyuma,sogea huko,fungua nauli yangu bana, piga chini upesi tuondoke zetu,.." kana kwamba abiria ni mkosefu vile. Anawakomesha na kuwasimanga kama manamba!
 
Back
Top Bottom