Marafiki watatu wameenda hotelini na na kulipa $30 ($10 kila mtu) kwa karani kukodi chumba. Alipofika Meneja wa hoteli, alimwambia karani, awarudishie $5, chumba ni $25 tu. Amefanya makosa.
Karani akaamua kufanya ujanja. Kwenye $5, Kawarudishia $1 kila Mtu, na kubaki na $2. yaani sasa wamelipa $27 ($9 kila Mtu) badala ya $30.
Swali. Kama gharama ni $27 na karani ana $2, kwa ujumla wa $29, $1 imeenda wapi?