GE2025 CHAUMMA yapokea wanachama wapya 250

GE2025 CHAUMMA yapokea wanachama wapya 250

Matukio, Taarifa, Habari na Mijadala ya Wananchi WAKATI wa Mchakato wa Uchaguzi Mkuu 2025

Mkalukungone Mwamba

JF-Expert Member
Joined
Aug 29, 2022
Posts
2,437
Reaction score
5,235
Chama cha Ukombozi wa Umma (Chaumma), kimepokea wanachama wapya 250 kutoka Jimbo la Kinondoni leo Jumapili, Julai 27, 2025 wakati chama hicho kilipofanya mkutano mkuu wa jimbo hilo.

Sera za chama, kushiriki uchaguzi, mabadiliko ni miongoni mwa sababu zilizofanya chama hicho kupokea wanachama wapya jimboni hapo kama alivyosema Katibu wa Jimbo la Kinondoni Chaumma, Amon Mwakasege.

Akizungumza katika mkutano huo, Katibu Mkuu wa Chaumma, Salum Mwalimu amesema hakina hiyana, ugomvi wala chuki na yeyote bali hasira za chama hicho zipo pale Watanzania wanapodhulumiwa haki zao.

"Chaumma hatuna shida na tunatamani tuwe daraja la kuunganisha vyama vyote. Sisi hatuna unyonge. Hatuna chuki, hasira zetu zipo pale Watanzania wanapocheleweshewa maendeleo yao," amesema.

Amesema akitokea kiongozi yeyote wa upinzani anayewahamasisha Watanzania kupiga kura wao Chaumma hawana shida naye.
 
Nakumbuka kambaya alishawahi kwenda chadema na wakina.mama 300 akiwaita want cuf. Baadae akaibukia ccm mwenyewe bila wale wanachama wake.
Leo kambaya ni mwana ccm bila wanachama wake.
Kambaya upo?
 
Chama cha Ukombozi wa Umma (Chaumma), kimepokea wanachama wapya 250 kutoka Jimbo la Kinondoni Jumapili, Julai 27, 2025 wakati chama hicho kilipofanya mkutano mkuu wa jimbo hilo

Sera za chama, kushiriki uchaguzi, mabadiliko ni miongoni mwa sababu zilizofanya chama hicho kupokea wanachama wapya jimboni hapo kama alivyosema Katibu wa Jimbo la Kinondoni Chaumma, Amon Mwakasege.

Akizungumza katika mkutano huo, Katibu Mkuu wa Chaumma, Salum Mwalimu amesema hakina hiyana, ugomvi wala chuki na yeyote bali hasira za chama hicho zipo pale Watanzania wanapodhulumiwa haki zao

"Chaumma hatuna shida na tunatamani tuwe daraja la kuunganisha vyama vyote. Sisi hatuna unyonge. Hatuna chuki, hasira zetu zipo pale Watanzania wanapocheleweshewa maendeleo yao," amesema.

Amesema akitokea kiongozi yeyote wa upinzani anayewahamasisha Watanzania kupiga kura wao Chaumma hawana shida naye

mn,.png

Chanzo: Mwananchi_official
 
Back
Top Bottom