Charles Kitwanga ni msiri wa Dk. Magufuli

Charles Kitwanga ni msiri wa Dk. Magufuli

PhD

JF-Expert Member
Joined
Jul 15, 2009
Posts
4,910
Reaction score
4,462
Ndugu zangu, mhe Rais amejipambanua kuwa atateua watu ambao ni wachapa kazi katika baraza lake la mawaziri. Naomba niwafahamishe tena kwa uhakika kuwa Charles Kitwanga aliyeteuliwa kuwa Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi ni mndani (msiri) wa mhe Rais.

Kitwanga alikwishaanza kujisifu kuwa atakuwa waziri wa wizara nyeti mapema kabisa na ushahidi upo. Lakini la pekee kubwa ni kuwa ni mtu asiyekuwa na rekodi ya utendaji wa kuwa waziri wa mambo ya ndani amepewa wizara hiyo sababu ya nepotism.

Muda utaamua na ni vema watanzania muelewe hata mhe Rais Magufuli na yeye pia kashindwa kuficha urafiki wa mtandao wake kinyume na kampeni zake.

Kitwanga atakuwa waziri wa kwanza kufukuzwa na bunge, ni suala la muda tu.
 
Huyu Mawe Matatu alishinda Ubunge mwaka 2005 na tangia hapo amekuwa Naibu Waziri/Waziri kwa kipindi chote cha JK hivyo hoja ya kwamba ni msiri wa Dr. Magufuli ingekuwa na mashiko kama angekuwa pia msiri wa JK. Aliibuliwa na JK na JPM amemkuta humo.
 
Kama Jf jukwaa la siasa litaendelea hivi hakika itapoteza wachangiaji wengi. Jukwaa juu mpaka chini linajaa majungu na fitina tu, limekuwa kama kijiwe cha kahawa badala ya kuwa sehemu ya watu kuweka hoja zenye mashiko na nzito. Sahivi hoja za Jf ni nyepesi mno kama nyimbo za kizazi cha miaka hii zinazojulikana kwa jina la big ji.
 
Ndugu zangu, mhe Rais amejipambanua kuwa atateua watu ambao ni wachapa kazi katika baraza lake la mawaziri. Naomba niwafahamishe tena kwa uhakika kuwa Charles Kitwanga aliyeteuliwa kuwa Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi ni mndani (msiri) wa mhe Rais.

Kitwanga alikwishaanza kujisifu kuwa atakuwa waziri wa wizara nyeti mapema kabisa na ushahidi upo. Lakini la pekee kubwa ni kuwa ni mtu asiyekuwa na rekodi ya utendaji wa kuwa waziri wa mambo ya ndani amepewa wizara hiyo sababu ya nepotism.

Muda utaamua na ni vema watanzania muelewe hata mhe Rais Magufuli na yeye pia kashindwa kuficha urafiki wa mtandao wake kinyume na kampeni zake.

Kitwanga atakuwa waziri wa kwanza kufukuzwa na bunge, ni suala la muda tu.

Wivu tuu unakusumbua, huna lolote!
 
Katika watu niliokuwa najua wataukwaa uwaziri ni huyu jamaa.Maana wakati wa kampeni jimboni kwake Magufuli alisema mbele ya watu,kwamba wasifanye masihara kutomchagua huyu jamaa kwani ana Kazi naye tena muhimu.Tangu hapo nilijua tu huyu jamaa ni waziri.

Kampa wizara ambayo ni nyeti,kumlinda yeye kama rais.Vita ya wahujumu uchumi si mchezo.
 
Ndugu zangu, mhe Rais amejipambanua kuwa atateua watu ambao ni wachapa kazi katika baraza lake la mawaziri. Naomba niwafahamishe tena kwa uhakika kuwa Charles Kitwanga aliyeteuliwa kuwa Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi ni mndani (msiri) wa mhe Rais.

Kitwanga alikwishaanza kujisifu kuwa atakuwa waziri wa wizara nyeti mapema kabisa na ushahidi upo. Lakini la pekee kubwa ni kuwa ni mtu asiyekuwa na rekodi ya utendaji wa kuwa waziri wa mambo ya ndani amepewa wizara hiyo sababu ya nepotism.

Muda utaamua na ni vema watanzania muelewe hata mhe Rais Magufuli na yeye pia kashindwa kuficha urafiki wa mtandao wake kinyume na kampeni zake.

Kitwanga atakuwa waziri wa kwanza kufukuzwa na bunge, ni suala la muda tu.

Wewe ni muongo na ni muongo sana. Urafiki wa Dr. Magufuli na Mh. Kitwanga siyo hoja ya kumteua kuwa waziri. Ingekuwa hivyo basi Masawe wa BOT naye angemteua maana naye ni rafiki yake wa karibu sana. Mimi namfahamu vizuri sana Charles Kitwanga. Ni moja ya viongozi wachache wenye msimamo na utendaji wa kazi. Ni mtu mwenye maadili na huwa hapendi uvivu na mtu wa maamuzi. Mi sema nilipenda angepewa wizara ya viwanda na biashara maana ni mtu anayeweza kufanya maamuzi. Ila hata huko mambo ya ndani anafaa tu Kwa sababu ni sehemu pekee inayohitaji mtu ambaye ana msimamo asiyeweza kuyumbishwa na mafisadi. Hivyo Charles Kitwanga ni Jembe!
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom