Ndugu wanaJF, kwenye taarifa ya habari ya saa 3:30 usiku (October 26,2011), nilimsikia Mkuu wa Kikosi cha Usalama Barabarani (traffic police) kupitia Mlimani TV akielezea chanzo cha ajali ya Delux Bus Service akisema siyo mwendo kasi kama baadhi ya abiria walivyodai bali ni kupasuka kwa tairi kulikopelekea bus kupinduka na kuwaka moto. Alisema hayo yalibainika baada ya uchunguzi uliofanywa na Kikosi cha Usalama Barabarani. Kwa mawazo yangu, uchunguzi unapofanyika wanaoweza kutoa uhalisia wa tukio lenyewe ni eyewitnesses hawa ndio primary source of information. Kupata chanzo cha habari nje ya eyewitnesses inakuwa reconstruction ili kupata conclusion fulani inayoendana na lengo la wachunguzi. Kwa maelezo ya kamanda, alidai si rahisi kwa abiria kubaini mwendo kasi wa gari maana speed limit bus kubwa ni 80km/hr na kwamba bus linalokimbia ndani ya mwendo huo halikimbii mwendo kasi. Mwendo kasi ni pale bus linapokimbia zaidi ya mwendo huo. Kwangu mimi, inaleta maana kusema mwendo kasi unaweza kusababisha (na huenda ndio uliosababisha) tairi kupasuka na hivyo bus kupindika na kuwaka moto kuliko kusema mwendo wa kawaida unaweza kusababisha (au ndio uliosababisha) tairi la bus kupasuka na hivyo bus kupinduka. (Ingawa in rare cases inaweza kutoka na ndio maana tunasema ajali haina kinga). Wakati Mkuu wa Kikosi cha Usalama Barabarani akielezea ajali hii, nilihisi kuwa alikuwa anajaribu kulitoa jeshi la polisi (traffic police) kwenye lawama maana kama angesema ajali ilitokana na mwendo kasi kama eyewitnesses wanavyodai ingeonekana kama traffic police hawakufanya kazi yao vizuri (kama ni eneo ambalo wapo). I could be wrong or right. Whats your opinion?