Ninavyoona mara nyingi maneno yote mawili yanaweza kumaanisha jambo lilelile. "Asili" ni neno kutoka lugha ya Kiarabu (asl); "chanzo" ni neno la Kibantu kutoka kitenzi "ku-anza".
Kama ni tofauti nahisi ni swali la mwendo. "Asili" ni kama nukta katika wakati - pale nyuma, wakati moja. "Chanzo" kina mwendo ndani yake; ni harakati ya kuanza, si "nukta katika wakati" tu bali ule mwanzo pamoja na kile kilichotoka mle.
Kwa kutumia mifano yako: "Chanzo cha muziki" - Waarabu huimba kwa njia fulani, mtindo huu ulifika Uswahilini ukapokelewa ukawa "taarab" jinsi tunavyoijua leo. Yaani muziki si kitu imara bali staili zinakua na kubadilikabadilika. "Chanzo" kinaweza kutaja mwendo huu. Unaweza kusema pia "Asili ya muziki wa taarab" na ukisema hivyo unaangalia tu athira ya Kiarabu bila kuzingatia jinsi gani muziki huu wa Kiarabu ulibadilika kuwa uimbaji wa Kiswahili.
"Asili ya neno hili" - asili ya "asili" ni Kiarabu "asl" jinsi inavyoonekana katika konsonanti zake. Hapo sipendi kuangalia mabadiliko mengine ya neno hili naridhika kuona kuwa neno hili la Kiswahili limetokana na lile neno la Kiarabu.
Mfano tena: Asili ya Kiswahili iko pwani la Afrika ya Mashariki, chanzo chake ilikuwa kukutana kwa tamaduni za wafanyabiashara Waarabu na za wenyeji asilia wa pwani hili.
Je wenzangu manonaje?