CHAMI: Ekelege na Joyce wameniponza

mgeni wenu

JF-Expert Member
Jan 2, 2012
3,664
1,730
Wana JF baada ya badiliko la mawaziri lililopelekea aliyekuwa waziri wa viwanda na Biashara ndg Cyril Chami kutemwa,imedhihirika ripoti zote za CAG hazimtaji moja kwa moja ila ni Ekelege(mkurugenzi mkuu TBS na katibu mkuu wake bi Joyce Mapunjo ambao wamekuwa wakila dili
"Kilichoniponza ni kutoipitia taarifa ya CAG na kutoa mapendekezo kama waziri,pia nilimuamini sana katibu mkuu ambaye yeye na wenzake walinigeuka na kuanza kuwa makuwadi wa kampuni feki za ukaguzi ambazo ni zao wenyewe tena hewa..
Nimegundua kosa langu la kumtetea Mkurugenzi wa TBS na kampuni zao.
Najua kama alivyosema rais na wao wataniafuata"
Mwisho wa kunukuu.
Hizi habari toka kwa Mtumishi wa ofisi yake ambae walikuwa nae jana usiku wakisikitika.
 
Majuto mjukuu. Uchafu wa Elelege ulisemwa muda mrefu na kamati ya mashirika ya umma, wabunge wamekwenda far east, hawajakuta hata kampuni moja na walisema kwenye report zao. Alikuwa anasubiri nini kutoa recommendations kwamba jamaa hafai? Mwache apotee, na M4C itamng'oa ubunge come 2015
 
Huyu jamaa ni buege wa kutupa..Watafuata wapi? Kwa kauli ya jana JK amesema 'kwa misingi ya sasa', thats means from now on (from yesterday- 4 May 2012) ndio watafuata, manake kwamba dhambi ya kabla ya hapo zimesamehewa!
 
na ndio akome yeye kapewa mamlaka sasa kama mda wa kuisoma ripoti hana ndio atatia akili kwani ni uzembe
 
pumbavi maiti ya muswahili haikosi sababu yeye kama waziri kwanini alika kimya hadi kufika hapo ndo shida ya viongozi wetu akishapewa lile shangingi analewa kabisa kumbe anahitaji kua mfatiliaji wa karibu kwa kilakitu kama Magufuli pamoja na makosa yake he follows up everything in his ministry. huyo Chami alikua mtu waku authorize to wala asitafute sababu
aende zake
 
Wana JF baada ya badiliko la mawaziri lililopelekea aliyekuwa waziri wa viwanda na Biashara ndg Cyril Chami kutemwa,imedhihirika ripoti zote za CAG hazimtaji moja kwa moja ila ni Ekelege(mkurugenzi mkuu TBS na katibu mkuu wake bi Joyce Mapunjo ambao wamekuwa wakila dili
"Kilichoniponza ni kutoipitia taarifa ya CAG na kutoa mapendekezo kama waziri,pia nilimuamini sana katibu mkuu ambaye yeye na wenzake walinigeuka na kuanza kuwa makuwadi wa kampuni feki za ukaguzi ambazo ni zao wenyewe tena hewa..
Nimegundua kosa langu la kumtetea Mkurugenzi wa TBS na kampuni zao.
Najua kama alivyosema rais na wao wataniafuata"
Mwisho wa kunukuu.
Hizi habari toka kwa Mtumishi wa ofisi yake ambae walikuwa nae jana usiku wakisikitika.

Aache kujikosha, ni mshirika wao. haya mambo sio ya leo, waziri hajiweki wazi, dili zinafanywa na waliochini yake yeye anapata mgao. Tuna ndugu zetu wa kuzaliwa tunajua kinachofanyika humo mawizarani etc.........Ndio uwajibikaji
 
Uzembe wa hali ya juu. Napata picha kinachofanyika ktk hizi wizara kama waziri anakuwa careless namna hiyo na hasa ktk mambo yanayogusa utendaji wake binafsi.

So kwake yeye Chami faraja ni kuwa katibu na mkurugenzi watamfuata......too cheap for comfort.
 
Hawa ndio aina ya wale wanaokufa sio kifo cha kisiasa tu bali hata mortal one.

Natamani mwakani ingekuwa 2015, tufanye uchaguzi ili wang'olewe wote hawa na ccm yao. Kwa mahitaji halisi ya sasa CCM haitakiwi kuwa na wabunge 50 ktk bunge la 2015, na wala hatupaswi kubaki na aina ya katiba tulionayo sasa hata kwa mwezi mmoja zaidi.

But all those are plain wishes!
 
Rais kasema kuanzia sasa sahani moja na wale wanaowakomoa mawaziri , iwe CEO au Board member.
 
Wana JF baada ya badiliko la mawaziri lililopelekea aliyekuwa waziri wa viwanda na Biashara ndg Cyril Chami kutemwa,imedhihirika ripoti zote za CAG hazimtaji moja kwa moja ila ni Ekelege(mkurugenzi mkuu TBS na katibu mkuu wake bi Joyce Mapunjo ambao wamekuwa wakila dili
"Kilichoniponza ni kutoipitia taarifa ya CAG na kutoa mapendekezo kama waziri,pia nilimuamini sana katibu mkuu ambaye yeye na wenzake walinigeuka na kuanza kuwa makuwadi wa kampuni feki za ukaguzi ambazo ni zao wenyewe tena hewa..
Nimegundua kosa langu la kumtetea Mkurugenzi wa TBS na kampuni zao.
Najua kama alivyosema rais na wao wataniafuata"
Mwisho wa kunukuu.
Hizi habari toka kwa Mtumishi wa ofisi yake ambae walikuwa nae jana usiku wakisikitika.

Mkuu lazima tukubaliane kwamba kuna wakati mawaziri ambao ni wanasiasa huwa wanawajibika kisiasa na si kwamba wameshiriki moja kwa moja kwenye uwivi ama ubadhirifu.

Katika Wizara mtu ambaye ni Afsa Uhasibu (Accounting Officer) ni Katibu Mkuu akisaidiwa na wakurugenzi. Kwa hiyo kwa mambo yote ya kitaalamu kuanzia fedha hadi utendaji KM ndiye mwajibikaji.

Jana JK amesema vyema. Kama kwa mfano Bodi za Mashirika yaliyo huru zikichukuliwa hatua tutaanza kuona uwajibikaji kwa kuwa hakuna wajumbe wa boadi watakao kubali kuwa rubber stamps kama ilivyo sasa.
 
Fungus zitakua zimeshapanda kichwani, inabidi doz ya ARV iongezeke, au akabadili blad kama mkul*...
 
rudi jimboni sasa ukae na wapiga kura toka umekuwa mbunge ulikuwa biz na uwaziri , tena sasa nadhani atapata fursa ya kujenga makazi ya uhakika (nyumba) jimboni kwake
 
Mpuuuzi huyu wacha atoke tu
Huyu nadhani ndio bungeni alikuwa anasema eti 'hajapewa' ripoti ya kamati/CAG, hapo ndo nilijua hi nchi imejaa watu bogus kabisa, ningekuwa prezidaa naangalia bunge lile palepale ningempigia simu na kumpoka uwaziri on the spot, lakini aah, hili linchi ni skio la kufa.
 
Nakumbuka alilaumu kuwa CAG kwapa ripoti wapinzani akina Nassari wakati yeye waziri hajapewa
Huyu nadhani ndio bungeni alikuwa anasema eti 'hajapewa' ripoti ya kamati/CAG, hapo ndo nilijua hi nchi imejaa watu bogus kabisa, ningekuwa prezidaa naangalia bunge lile palepale ningempigia simu na kumpoka uwaziri on the spot, lakini aah, hili linchi ni skio la kufa.
 
Huyu jamaa ni mbunge wa jimbo ninalotoka la moshi vijijini,nawahakikishia sielewi jamaa alishinda vipi pale maana kuna mwamko wa ajabu hakika 2015 hawatakua na chao pale,halafu anasema eti walimchagua kwa vile walijua raisi atampa uwaziri hivyo ccm ihesabu italipoteza jimbo lile ana wazimu kweli kwan na huo uwaziri kuna nini alichofanya pale,kahawa ina bei kubwa inafikia 7000 kwa kilo lakini wananchi pale hawajawezeshwa walime kilimo cha kisasa ili wafaidi hiyo bei ambayo majuz tu ilikua 1500
 
Rip ccm in moshi rural,kata nyingi zimekombolewa na mwamko ni wa ajabu sana yani kampeni za diwani tu ilikua ni kivumbi nguo kuchanika kuna kata mbili ambazo nilishuhudia mwamko usio wa kawaida nazo ni Kimochi na Mabogini na zote zilienda cdm kwa kishindo na awali zilikua za magamba magamba,magamba wamejeruhiwa vibaya
 
Back
Top Bottom