Mwande na Mndewa
JF-Expert Member
- Feb 26, 2021
- 949
- 2,865
Wakati wa awamu ya kwanza enzi za Baba wa Taifa Mwalimu Julius Nyerere,na awamu ya pili iliyoongozwa na Rais Ali Hassan Mwinyi,katibu wa CCM Mkoa ndiye alikuwa Mkuu wa Mkoa,katika mfumo wa vyama vingi Mwenyekiti wa CCM hawezi kushika nafasi ya Mkuu wa Mkoa au Mkuu wa Wilaya,hivyo basi nani Mkubwa mwenye uwezo wa kumuagiza mwingine afanye jambo katika mfumo huu wa vyama vingi hivi leo,je nani kati ya Waziri na Katibu Mkuu wa CCM anaweza kumuigiza mwenzake? nani kati ya Waziri wa Serikali na Katibu Mwenezi wa CCM Taifa anaweza kumuagiza mwenzake?
Kwa mfumo tulio nao sasa hivi,Mwenyekiti wa CCM Mkoa ana nguvu zaidi ya Mkuu wa Mkoa,Fitina za Mwenyekiti zina nguvu kuliko za Mkuu wa Mkoa,kuna usemi "atakayemgusa mwanachama wa CCM atakiona lakini hausemi atakaemgusa muajiriwa wa serikali atakiona cha mtema kuni".Kwa utaratibu wa sasa Mwenyekiti wa CCM akipata uteuzi inabidi ajiuzulu aende kwenye utumishi mpya,wakati wa Awamu ya tano,enzi za Rais John Magufuli tuliona uteuzi wa Mh Zambi wa Lindi na Mh Chalamila kutoka Uenyekiti wa CCM Mkoa wa Iringa hadi Mkuu wa Mkoa wa Mbeya na leo Mkuu wa Mkoa wa DSM.Je, kiitifaki na kimadaraka yupi yuko juu ya mwenzie kati ya Mwenye ilani na yule anayetekeleza ilani.
Zamani uteuzi kama huo ulikuwa ni kushuka chini ila siku hizi kupanda ni kupanda juu,Jibu ni rahisi tu angalia mfano RC Dar, na mwenyekiti ccm Dar, kipato, fursa, status, ulinzi nk, Miaka ya 1980 hadi miaka ya 1990 Mnene wa Chama CCM ngazi ya Wilaya tu basi Mkuu wa Mkoa na Mkuu wa Wilaya walikoma kwenye kamati ya Ulinzi na Usalama ila siku hizi usishangae Mwenyekti wa CCM Mkoa anaomba mafuta ya gari kwa Mkuu wa Mkoa,je hapo nani atamnyenyekea mwenzie? Miaka hiyo ya 1980 hadi 1990 Usalama wa Taifa wa Wilaya DSO akitaka azungumze na Katibu wa CCM Wilaya alikuwa hamuiti ofisini kwake bali aliomba kuja ofisini kwa Katibu wa CCM tena kwa Appoitment, Chama kiliongoza Serikali na organ zake.
Nimalizie kwa pongezi nyingi kwa Mh Paul Makonda,Katibu wa Itikadi na Uenezi Taifa,kwa kukirudisha chama kwenye njia yake kusimamia uwajibikaji sawa sawa na ilivyokuwa enzi za Mwalimu Julius Nyerere,Mwenezi anaonyesha njia bora za utendaji kwa watendaji wa chama kuonyesha chama kinajali yale mapungufu viongozi wake wayoyatenda ili kuwavutia wananchi kubaki na matumaini kwamba chama kinamipango mizuri lakini watendaji ndio wanakiangusha hivyo anaibua matumaini mapya kwa wananchi kukionyesha chama kuwa kinaelekeza kwa usahihi yale yote yanapaswa kufanyika usawa, jinsia, utetezi, utendaji ulitukuka kwa wananchi kusilikiza kero zao na kuimarisha Serikali ili kuongeza wananchama na kuongeza mvuto na ushawishi kwenye chama cha mapinduzi,Makonda yuko sahihi sana kabisa na aendelee kabisa kutoa matamko.
Nikiishia hapa, Mimi ni
Msemakweli Chakubanga,
Dar es Salaam.
0755078854
-Bachelor of business administration in International business.
-Master of Leadership and Management.
Recent Publications;-
-Assessment on the Effects of Micro-financing on Poverty Reduction.
Kwa mfumo tulio nao sasa hivi,Mwenyekiti wa CCM Mkoa ana nguvu zaidi ya Mkuu wa Mkoa,Fitina za Mwenyekiti zina nguvu kuliko za Mkuu wa Mkoa,kuna usemi "atakayemgusa mwanachama wa CCM atakiona lakini hausemi atakaemgusa muajiriwa wa serikali atakiona cha mtema kuni".Kwa utaratibu wa sasa Mwenyekiti wa CCM akipata uteuzi inabidi ajiuzulu aende kwenye utumishi mpya,wakati wa Awamu ya tano,enzi za Rais John Magufuli tuliona uteuzi wa Mh Zambi wa Lindi na Mh Chalamila kutoka Uenyekiti wa CCM Mkoa wa Iringa hadi Mkuu wa Mkoa wa Mbeya na leo Mkuu wa Mkoa wa DSM.Je, kiitifaki na kimadaraka yupi yuko juu ya mwenzie kati ya Mwenye ilani na yule anayetekeleza ilani.
Zamani uteuzi kama huo ulikuwa ni kushuka chini ila siku hizi kupanda ni kupanda juu,Jibu ni rahisi tu angalia mfano RC Dar, na mwenyekiti ccm Dar, kipato, fursa, status, ulinzi nk, Miaka ya 1980 hadi miaka ya 1990 Mnene wa Chama CCM ngazi ya Wilaya tu basi Mkuu wa Mkoa na Mkuu wa Wilaya walikoma kwenye kamati ya Ulinzi na Usalama ila siku hizi usishangae Mwenyekti wa CCM Mkoa anaomba mafuta ya gari kwa Mkuu wa Mkoa,je hapo nani atamnyenyekea mwenzie? Miaka hiyo ya 1980 hadi 1990 Usalama wa Taifa wa Wilaya DSO akitaka azungumze na Katibu wa CCM Wilaya alikuwa hamuiti ofisini kwake bali aliomba kuja ofisini kwa Katibu wa CCM tena kwa Appoitment, Chama kiliongoza Serikali na organ zake.
Nimalizie kwa pongezi nyingi kwa Mh Paul Makonda,Katibu wa Itikadi na Uenezi Taifa,kwa kukirudisha chama kwenye njia yake kusimamia uwajibikaji sawa sawa na ilivyokuwa enzi za Mwalimu Julius Nyerere,Mwenezi anaonyesha njia bora za utendaji kwa watendaji wa chama kuonyesha chama kinajali yale mapungufu viongozi wake wayoyatenda ili kuwavutia wananchi kubaki na matumaini kwamba chama kinamipango mizuri lakini watendaji ndio wanakiangusha hivyo anaibua matumaini mapya kwa wananchi kukionyesha chama kuwa kinaelekeza kwa usahihi yale yote yanapaswa kufanyika usawa, jinsia, utetezi, utendaji ulitukuka kwa wananchi kusilikiza kero zao na kuimarisha Serikali ili kuongeza wananchama na kuongeza mvuto na ushawishi kwenye chama cha mapinduzi,Makonda yuko sahihi sana kabisa na aendelee kabisa kutoa matamko.
Nikiishia hapa, Mimi ni
Msemakweli Chakubanga,
Dar es Salaam.
0755078854
-Bachelor of business administration in International business.
-Master of Leadership and Management.
Recent Publications;-
-Assessment on the Effects of Micro-financing on Poverty Reduction.