Chama gani mbadala kwa CCM?


Dr Bana tangu lini akweka bayana wakati yupo kwenye payroll ya magamba? Redet nayo tangu imeanzishwa ni kwa ajili ya kutoa matokeo ya yasiyo na tija kwa umma. Hawafiki huku kwetu Ihambingeto au ifiyo au itunundu wawaone wananchi wawaambie kama hakuna chama mmbadala. hizo tafiti za mezani hazina tija.
 
Hao ndiyo chadema bwana hataki hata ukiwaambia ukweli kupinga ni jadi yao. ila kwa hapa nakupongeza kwa kuwaomba waelewe manaa ya neno Mbadala maana tutaruka Maji na kukanyaga matopeee

Mkuu kwa hapa tulipofokia kama watanzania, umuhimu wa kubadili utawala ni kurejesha nguvu ya utawala kwa wenye nchi ambao ni watanzania na kuondokana na kasumba ya leo ambavyo watanzania wamesukumizwa kwenye kona na watawala na mafisadi wakiwa hawana sauti ya kuhoji wala kugomea ubaya wowote unaofanywa na watawala hawa . Watanzania wamekuwa kama watumwa kwenye nchi yao, wanalima na kuzalisha kwa ajili ya matumbo ya watawala na mafisadi. Hawana ujasiri wa kuhoji wala kikataa uovu wanaotendewa na watawala wa sasa. Ni nchi gani ambayo wananchi waka hawawezi kulalamika hata kama ukipandisha bei ya kila kitu? Hawawezi hata kugomea huduma mbovu za afaya na elimu ili hali watawala wanatesa na maV8 wakizunguka kwa kodi zao?

Nchi hii tuko huru lakini bado ni watumwa ndani ya nchi yetu wenyewe! Mtumwa hupoteza kwanza fikra zake na kujiona yuko kawaida hataanapoonewa huwa hana uwezo wa kubishana na bwana wake! Watawala ndiyo mabwana wa watanzania.

Mkuu katika hali hii njia ni moja tu ni kuuangusha utawala unaodumisha utumwa huu na kuweka utawala mwingine wowotw ili watawala watambue umuhi wa kura za wananchi.

Mkuu mimi sisemi kuwa chadema italeta maziwa na asali, iLa ninachokiangalia hapa ni kubadilisha watawala ili kurejesha nguvu ya utawala kwa umma wa watanzania. Watawala wajue kuwa wananchi ndo wenye nchi wanauwezo wa kumweka yeyote wanayemtaka wao, na wanaweza kumwondoa wakati wowote wakitaka wao.

Tukifikia hapo ndipo heshima itarudi na kila mtawala atafanya yaliyomatakwa ya watanzania si matakwa yake na kIkundi cha watawala wenzake.

Tunataka ccm na mafisadi wake wakae pembeni ili kurejesha nguvu ya utawala kwa umma. Tunahitaji chama kingine kitakachotawala kikijua kuwa kimewekwa na nguvu ya umma hivyo kufanya yale tu umma unataka.

Tukifika hapa watawala hawatatupa shida hata ndani ya miaka miwili tunaweza kumpiga chini na kuweka wengine.

Bila kufanya hivyo tutaendelea kujenga taifa lenye watumwa ndani ya nchi yao na kikundi kidogo cha mabwana.

Mwenye kupinga mtazamo huu atakuwa ni chizi na pengine labda yuko katika hiki kikundi kidogo cha mafisadi na mabwana wanaotaka hali hii iendelee maana kwao ni faida na wataendelea kurisishana mpaka vitukuu.

Wake up Tanzanians achana na propaganda za watawala na mafisadi eti kuipiga chini ccm na kuweka chama kingine tunaweza kuruka mkojo na kukanya mavi! Kama wanamapinduzi tuliangalie swaala la kubadilisha utawala ni kuwanyang'anya ccm na mafisadi wake nguvu ya utawala na kuirejesha
kwa umma.
 
Mie uwa sioni tofauti yoyote kati ya wasomi wa Tanzania na wavuta bange wa Tandale kwa Bibi Nyau.
 
Mie uwa sioni tofauti yoyote kati ya wasomi wa Tanzania na wavuta bange wa Tandale kwa Bibi Nyau.

Unamaana wasomi wote wa Tanzania wako kama wavuta bange wa Tandale Kwa Bibi yako Nyau?
 
ila ni lazima ajue kwamba serikali ni wananchi sio chama,kama yeye hakuona chama mbadala sio ukomo wa kuwa na serikali mbadala wa hii tulionayo na labda anataka kutuaminisha kwamba hatuhitaji kuwa na serikali mbadala kisa hatuna hicho chama mbadala na sidhani kama ccm ndo wana hati miliki ya hii nchi au mkataba wa kuitawala tz maisha sio kweli..mda utakapofika na wananchi wakatafuta huo mbadala ndo atajua kwamba alikuwa anatuhadaa..
 
Hangover ya kukulia katika mfumo wa chama kimoja. Unfortunately, it is too late for him to change. Kwamba hataki mabadiliko haimanishi kwamba hayatatokea.

Nakionea huruma Chuo Kikuu cha Dar es Salaam. Siasa imejikita hadi kwa wasomi na wao wamepoteza umahiri wa uchambuzi badala yake wanachambuana.Enzi za akina Seth Chachage (RIP), Haroub Othmani (RIP), Wamba dia Wamba na Chris Peter Maina usingekuta haya. UDASA ilikuwa ikipika wanazuoni na mwanazuoni akitoa hoja inakuwa ni hoja wakilishi siyo siku hizi kunakuwa na hoja maslahi tuuu. Maskini UDSM
 

Tukiamua kutafuta data, sidhani kama tunaweza pata 10% ya hawa the so called Doctors and professors ambao kwa hakika wanafanya kazi zao fairly kwenye jamii yetu hii inayojaribu kujikwamua kifikra.
Inawezekana mtu ukifikia ngazi hii, akili haiwi sawa sawa.
 
Dr Bana ni kati ya wasomi wanaccm wanaojua kuwa mwisho wa ccm umefika, ila kwa kuwa anaroho mbaya kwa wanaccm wenzie anaamua kusema vile, kwa kuwa wanaccm karibia wote hamnazo, wanafurahia hii kauli ile mbaya, lakini mwisho wa siku watalia na kusaga meno
 
bana kasema kweli chadema bado sana kupewa nchi
 
 
yani bado mnalisikiliza hili zee,.of course hakuna mbadala kwenye mavazi,minguo ya njano na kijani wanavaa wao tu..nyambaf
 
Hangover ya kukulia katika mfumo wa chama kimoja. Unfortunately, it is too late for him to change. Kwamba hataki mabadiliko haimanishi kwamba hayatatokea.

Nilitaka kujua mawazo yako Dr Kitila dhidi ya Dr Bana, Big up Dr Kitila, hata Marehemu Col Gaddafi aliambiwa Waasi wame-advance 80% kushinda mapambano, halikataha katakata kuachaia madaraka, akaendelea kusisitiza waasi ni panya, mende, samaki wa bahari ya mediteranian
 

Mkuu naona CCM wana strategy nzuri. Uzuri wake ni kuwa wanajikita kwa wanyonge na wajinga. Nadhani hii ni genuine political strategy kwa kuwa wasomi tanzania hawafiki asilimia 5.
 
Hangover ya kukulia katika mfumo wa chama kimoja. Unfortunately, it is too late for him to change. Kwamba hataki mabadiliko haimanishi kwamba hayatatokea.
Kuhukumu moja kwa moja si sahihi, lazima kwanza tutazame shina la hoja na lazima tuwe wakweli...maneno ya Dr.Bana lazima yawe changamoto kwa vyama vya upinzani hasa CDM, ukweli ni kwamba chama chochote cha siasa huzaliwa,hukua na kuzeeka (kama ilivyo kwa CCM), na kwa kuwa CDM ni chama kinachokua lazima kijenge ukomavu wa kimkakati na kifikra katika jukumu kubwa la uongozi wa taifa letu
 
sijaelewa kwanini huyu bana anapewa sana airtime na vyombo vya habari wakati hana mawazo endelevu ya kuwasaidia watanzania.hata anapoongea unajua kabisa huyu ana kadi ya ccm.hivyo hawezi kuwa na mawazo nje ya ccm.hana mkusanyiko wa mawazo amekwisha kabisa na usomi wake feki huo.bana si mtu wa kumhoji kwa ajili aya kupata mawazo yenye kujenga.huyu nu mshauri wa jakaya.hana jipya aende zake.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…