Kwa kipindi kirefu tangu kuanzishwa kwa mfumo wa vyama vingi tumeshuhudia uanzishwaji wa vyama lukuki lakini vyama hivi vingi vimekuwa kama Mali ya mtu binafsi,tunaweza tusikubaliane lakini sisi sote ni mashahidi mfano Chama cha UDP cha mzee Cheyo, TLP cha mzee Lyatonga, na vingine vingi.ukiviangalia huoni vikisimama kama taasisi bali vipo kama Mali ya mtu.chama cha CUF kimeendelea kuwepo lakini uhai wake unategemea eneo moja la nchi Pemba, bila pemba hakuna CUF huku bara ipo tu mradi na sote tunajua.Chadema kimejitahidi kuenea kwenye sehemu sehemu za bara lakini kule zanzibar hakipo kabisa.katika Hali kama hiyo na kwa kuangalia katiba yetu Chama pekee kinachobaki kuwa na sifa pande zote mbili za muungano ni ccm.Katika Hali kama hiyo wote ni mashahidi kuwa vyama hivi havijajengwa katika misingi imara ya kushika nchi hasa kwa katiba hii ya sasa.Tunaweza kuilalamikia ccm lakini ni ukweli usiopingika kuwa bado hatujawa na Chama kilichosheheni barabara pande zote na nchi nzima kwa maana ya uwepo wake zaidi ya ccm.kwa sababu hiyo bado hatuna Chama mbadala kwa mfumo,Sera na uwepo wake.vyama vya upinzani vinapaswa kuungana na kuunda Chama imara kinachoweza kushika dola.kwa mtizamo wangu naona bado hakuna Chama mbadala wa kushika dola na kuongoza nchi.