Chama gani mbadala kwa CCM?

Hangover ya kukulia katika mfumo wa chama kimoja. Unfortunately, it is too late for him to change. Kwamba hataki mabadiliko haimanishi kwamba hayatatokea. Poleni my colleague BB!

Nakubaliana nawe, uwezo wa kufikiri nje ya box hawana. inawezekana kiapo hiki kimewaathiri sana (Naapa naahidi mbele ya chama, mapinduzi nitakulinda mpaka kufa!!!!!) kidogo tunachoweza kujadili ni kuwa waliapa kukilinda chama mpaka kife au mpaka wao wafe!!!!!
 

Very true,though it hurts and we dont like it.. I think he is posing a challenge
 
Hangover ya kukulia katika mfumo wa chama kimoja. Unfortunately, it is too late for him to change. Kwamba hataki mabadiliko haimanishi kwamba hayatatokea. Poleni my colleague BB!

Huyu jamaa anawaaibisha academicians,usomi wake ni wa makaratasi,hawezi kufikiria nje ya box.
 

Siwezi kumshangaa huyo DR,watanzania wengi wana inferiority complex, they fear their nature,huyu DR naye yumo katika hilo kundi mazungumzo yake huwa nayasikiliza sana,ukimuangalia sana huwa comments zake anaangalia mambo yamekaaje kwa wakati huo(anafuata upepo).sote tunajua watu wa aina hii ndio washauri wa serikali yetu katika mambo mengi ya maendeleo Dr Bana kwa upande wangu huwa simtofautishi na mwanasheria mkuu wa serikali ,kwa ajili ya kuhangaikia mkate wa siku hiyo iliyopambazuka na kesho atajua kesho kukicha watachangaje karata wapate mkate mzuri wenye siagi ya brueband toka Kenya badala ya Tanbond ya Tanzania.
Ni aina ya watu wanajitahidi kuakikisha wanaitetea CCM na Serikali yake hata kwa makosa ilimuradi wafanikiwe kuchumia tumbo.
Sasa hivi dunia imebadilika sana kwenye secta ya siasa na uongozi,nchi yetu bado haijabadilika kwasababu kuna udicteta na ufalme wa chini chini ,tena ufalme huu ni mbaya sana kwa sababu ni ufalme wa viongozi kutaka famili zao kuwa viongozi pia hata kama hawawezi muda wao wa kupumzika ukifika.
Nchi hii wapo wenye uwezo wa kuwa viongozi wazuri kinachowashinda ni masharti ya kuingia katika hako kakundi ka sasa maana wanajitahidi kadiri iwezekanavyo kulinda na kuhalalisha maovu wao hiyo sio sera yao katika maisha wanayoamini wao.

Tanzania ya leo haikupaswa kuwa hivi, ni matatizo ya uongozi ndio yametufikisha hapa,hili DR Bana asibishe na wasababishaji ndio hao hao anao wapigia debe leo kwa nguvu zake zote,hivyo DR Bana ajue kuwa kwakuendelea kuwa na mtiririko wa hao viongozi tutazidi kutiririka kwenye maangamizi ya uchumi wetu na maisha ya watanzania kwa ujumla wake.
Kinachotakiwa sasa kwa hali yoyote ile mabadiliko ya uongozi(mfumo mzima)ni lazima ili turudi kwenye msitari.
Tuliweka matumaini sana kwa JK lakini mwishoe hakuna tulichopata zaidi ya kuendelea kuanguka kutokana na matokeo ya sasa wale wote wanaojitayarisha kumrithi siwaamini hata kidogo lazima watanzania tu wa suspect kama ni failure tayari kabla hata hawajaingia madarakani.

CCM ikitoka madarakani ndio utakuwa mwanzo wa kuwepo mfumo mpya wa uongozi amini usiamini uongozi mzima wa CCM utabadilika na ndio uwazi utakuwapo na ulinzi wa mali yetu utakuwapo pia mfumo wa siasa utabadilika kwa 100%. Kwa watanzania wenzangu ambao tunaweza kupamabanua mambo kwa ukweli na si kwa unafiki tuendelee kufanya hivyo kwa jia yoyote ile iwe kwa mahojiano na vyombo vya habari au kwa mitandao kama JF. JF ni chuo cha maendeleo ya kweli.
 
bado tanzania tuna watu wanaojua kusoma,wanasikia na kuona lakini vyote hivyo havina faida ni mtu asiyekuwa navyo vyote.
 
mwamba ngozi daima huvuta kwake,ulitegemea atasemaje?
 
Hao ndiyo chadema bwana hataki hata ukiwaambia ukweli kupinga ni jadi yao. ila kwa hapa nakupongeza kwa kuwaomba waelewe manaa ya neno Mbadala maana tutaruka Maji na kukanyaga matopeee

Utajuaje kama umekanyaga matope bila
kukanyaga?
 

Redet ni taasisi ya ilio jaa watu wenye kujikomba sana kwa ccm,na nashindwa kuelewa kua ni njaa au vyeo ndio wanacholilia,msomi mzima kama Dr Bana siku hizi ameamua kujivua nguo na kuipaka mafuta ccm kwa mgongo wa chupa....hii nis shame kwa taaluma yake,na hapo kwenye red mkuu ungesema baadhi ya wasomi wetu,maana si wasomi wote ambao wanaangukia watawala,wapo wenye misimamo yao na wenye kuheshimu na uelewa maana ya taalamu zao,ila hao uchwara ndio wamekua wapiga magoti kwa watawala na kusahau maana ya taaluma zao,majibu ya kua kama kuna chama mbadala cha kuongoza nchi au lah atayapata miaka si mingi huyo Dr Bana,tuombe uhaia tu
 
 
Hangover ya kukulia katika mfumo wa chama kimoja. Unfortunately, it is too late for him to change. Kwamba hataki mabadiliko haimanishi kwamba hayatatokea. Poleni my colleague BB!

mkuu hapa umeua kabisa hapa. Nimependa hiyo sentensi ta mwisho!!
Kwamba tu yeye hataki mabadiliko, haimaanishi kwamba hayatatokea.
 
Kila ninaposikia kwamba Dr Bana anakaribia kutoa taarifa ya upepo wa kisiasa hapa nchini huwa tayari napata mwelekeo/mtazamo wa taarifa zenyewe hata kabla ya kutolewa. Maana halisi ya utafiti ni kutafuta yale hasa yasiyofahamika lakini mtazamo wa huyu Bana Mkubwa waonekana wazi kuwa kuna kitu anatafuta toka 'Chama Chake'
 

Kwa maneno aliyo tamka nina kuwa na mashaka nae kuwa ni kibaraka wa ccm kwa asilimia 100.
 
Bensoni Bana hajaweza kujitofautisha na lay man mtaani huko.

Kutegemea takwimu za matokeo ya uchaguzi wa mwaka 2010 kama kigezo cha kusema hakuna chama mbadala ni kupotoka kuliko pitiliza.

Aende mbali kama msomi kuchambua makando kando ya kimifumo yalizalisha hayo matokeo.

Ajiulize kama sheria zinazotawala chaguzi za serikali za vijiji mitaa na vitongoji kama ni rafiki kwa watanzania kufanya maamuzi yao wanayoyaamini na yakaheshimika hivyo.

Vinginevyo mawazo ya huyu anayejiita msomi yako kwenye ulimwengu wa vionjo ama wa vinavyoonekana tuu (The world of apearance and not that of essence).
 
Mimi sitoshangaa kama kesho atasema kwamba "mpaka sasa haoniRais mbadala wa Kikwete
Tanzania" Hivyo JK aongezewe term nyingine kutokana na utafiti wa REDET!

Ama kweli Tanzania ina watu na viatu, pia kuna wasomi na wachumia tumbo!
 


Dr. Bana, baada ya kupewa kauongozi ka redet, amerudi kundini. simshangai
 

Ulikunywa nini kabla ya kuandika ulichokiandika hapa? It is your loss if you choose not to listen to what CHADEMA keep saying. Ufinyu wako wa uelewa hausababishi kutokuwepo kwa hicho usichokielewa!
 
Za mbayuwayu changanya na za kwako,sijui hata uanzie wapi kueleimishwa,maana umejichanganya kupita maelezo,hata kukueleimisha ni kazi,baki hivyo hivyo tu,maana katika society lazima watu kama nyie muwepo
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…