Chama dola kinapokosa upinzani tutegemee nini?

Sky Eclat

JF-Expert Member
Oct 17, 2012
57,597
215,270
1575017199101.jpeg


Gen Paul Kagame alipotwaa madaraka alicheza kulinyoosha Bunge halafu akavimaliza vyama vya upinzani,watu wa chama chake RPF wakabaki wanamshangilia na kuona wamebaki wao tu kama chama tawala!

Baada ya kuona sasa bunge ni dhaifu, mahakama ni yake na vyama vya upinzani vimebaki majina tu na wapinzani akawatia ndani, akaanza kushughulikia na chama chake RPF mbacho ni maswahiba zake waliomwingiza madarakani kutoka chama cha RPF.

Akaanza na Mkuu wa inteligensia Kanal Patrick Karegea na Mkuu wa mMjeshi Gen Kayumba Nyamwasa,akawafuta kazi na wakakimbilia afrika ya kusini kuokoa maisha yako na wengine wengi wakakimbia Rwanda na kwenda kuishi uhamishoni ile top cream ya RPF iko uhamishoni kuhofia maisha yao,leo amebaki mwenyewe!

Sasa anatamba na ameunganisha chama chake rpf na jeshi sasa system inafanya uchaguzi na anashinda mwenyewe na ameshaongeza muda wa kukaa madarakani! Ni mwerevu sana na sasa anatamba mwenyewe kama tembo uwanjani! Chama cha RPF sasa ni system ya jeshi siyo chama tena! Anakula bata na ukimsema vibaya haupo labda uzungumze ukiwa chumbani na mkeo!

Naona mahali fulani chama tawala wanashangilia vyama vya upinzani kufa,bunge dhaifu na mahakama kutotenda haki,nawashangaa kwani wanaelekea huko!Wanakoelekea chama kitabaki jina tu na wataanza kushughulikiana wenyewe kwa wenyewe hamani, madudu ya awamu zilizopita yatawekwa hadharani.

Wengi watafungwa na wengine watakimbia nchi ili bwana mkubwa abakie kama tembo uwanjani baada ya hapo chama kitaungwa na vyombo, muda utaongezwa basi mchezo umekwisha na chama kitabaki jina mfumo utatawala! Uchaguzi hewa na mambo. Chama tawala ni sawa na kuni mbichi inayocheka kuni kavu ambayo ni vyama vya upinzani iko jikoni kwa sasa wakati kesho ni zamu yake!. Kuna mtabiri aliwahi kusema akimalizana na sisi atakuja kwenu!
 
hujaeleweka unataka nini wapinzani hawajafkuzwa wanaogopa vivuli vyao kila sehemu wanakimbia wanini sasa
 
Huko huko, lakini with current trends, hata mabeberu wanawzxa kusupport civil war ikianziswa na wasioweza kustahimili uonevu wa sasa. Nguvu ya umma haiwezekani kwa sasa, tu waogoa wa kufa sana tena sana!
Tunajiona tunakoelekea na siku hizi kila unapoongea na mtukufu ni lazima uanze na pongezi za ujenzi wa reli, barabara, ununuzi wa ndege na usifie uongozi wa awamu ya tano.
 
Tunajiona tunakoelekea na siku hizi kila unapoongea na mtukufu ni lazima uanze na pongezi za ujenzi wa reli, barabara, ununuzi wa ndege na usifie uongozi wa awamu ya tano.
By the way, obiter, Nimesoma mahali Lisu anasema atarejea marafiki watakaposema niko salama! Nimejiuliza marafiki gani> Ametaja mashirika ya haki za binadamu, serikali etc. Napata shida kidogo!
 
By the way, obiter, Nimesoma mahali Lisu anasema atarejea marafiki watakaposema niko salama! Nimejiuliza marafiki gani> Ametaja mashirika ya haki za binadamu, serikali etc. Napata shida kidogo!
lisu haeleweki anataka nini
 
By the way, obiter, Nimesoma mahali Lisu anasema atarejea marafiki watakaposema niko salama! Nimejiuliza marafiki gani> Ametaja mashirika ya haki za binadamu, serikali etc. Napata shida kidogo!
Lissu si mjinga, baada ya yaliyomtokea kurejea kwake ni lazima usalama wake awe na uhakika nao.
 
umeona hicho tu ? tatizo hamjui kuwa ndege zinapromote vitu vingi kama utalii siyo daladala hizo mkuu
Inabidi umfahamu mtanzania na hulka zake, siku zote anataka afanye kazi yenye thamani ya shiingi milioni moja halafu mwisho wa mwezi alipwe milioni kumi.
 
Inabidi umfahamu mtanzania na hulka zake, siku zote anataka afanye kazi yenye thamani ya shiingi milioni moja halafu mwisho wa mwezi alipwe milioni kumi.
Hapana watanzania ni wavumilivu sana, Mauro ya korosho ya msimu uliopita wengine hawajapata mpaka sasa hivi
 
Tundu Lisu alitabiri na sasa yameshaanza. Lakini nadhani kuna siku Rwanda itaingia tena kwenye civil war, hii hali haitadumu milele, hapana! Watakaokuwepo watasoma post hii!
Nami ninaungana nawe ,watakaokuwepo wataisoma hii ya kwangu pia,Sudan jana chama tawala chao kimefutwa kitu ambacho kilikuwa ndoto ya saa saba mchana na jua kali!!Zanu PF kipo kwenye ICU,SWAPO kinakabiliwa na mtihani mkubwa sana kipindi hiki(ke amejitokeza kupambana SIO me),Botswana hapo chama tawala wanayumba(pamoja na kushinda uchaguzi kwa mbinde).always muda ni ukuta.
 
Nami ninaungana nawe ,watakaokuwepo wataisoma hii ya kwangu pia,Sudan jana chama tawala chao kimefutwa kitu ambacho kilikuwa ndoto ya saa saba mchana na jua kali!!Zanu PF kipo kwenye ICU,SWAPO kinakabiliwa na mtihani mkubwa sana kipindi hiki(ke amejitokeza kupambana SIO me),Botswana hapo chama tawala wanayumba(pamoja na kushinda uchaguzi kwa mbinde).always muda ni ukuta.
Tena CCM kwa ukatili inaoufanya kwa wapinzani/wananchi, itakufa na maangamizi ya koo zao wanaotesa watu sasa. Watu wameweka mafundo makubwa. Unadhani say motto wa jiwe yuko slama? Siro? Bashiru? Polepole? Wakati utaongea.
 
Back
Top Bottom