blackice2100
JF-Expert Member
- May 11, 2020
- 2,038
- 2,718
Habari zao ni za kutabirika na za mezani zaidi kuliko za kuzitafuta na kwa sasa ni za kumpamba mtawala aliyeko madarakani japo naamini ni za kinafki kama kawaida yao.
Ngoja Samia aondoke madarakani ndo utaiona rangi ya hawa wanafki walioamua kukimbia taaluma yao na kuwa wapiga debe wa kusoma upepo.
Ngoja niingie kwenye hoja ya msingi; Hebu naomba kujuzwa mmiliki wa hili gazeti haswa ni nani la Jamvi la Habari?
Hili gazeti kama si kwa makusudi basi kuna mtu ana ajenda zake za kugombanisha viongozi wa WALIMU na SERIKALI tena anatumia nguvu kubwa sana sijajua ana maslahi gani.
Nakumbuka tangu wale viongozi walipoomba kutohudumu nafasi walizoteuliwa na Rais mama Samia yaani hili gazeti limekomaa na hawa watu haswa.
Hebu wapana wa maarifa mtufungue macho kuna nini nyuma ya pazia?