Chama cha ushirika MTAMA waiba pesa za wakulima

MJINI CHAI

JF-Expert Member
Dec 12, 2010
2,198
1,226
Pamoja na Jitihada kubwa zinazofanywa na Serikali ya Awamu ya Tano kuboresha zao la korosho kwa wakulima kupata bei nzuri ambayo haijawahi kutokea hapo nyuma kwa mfumo wa stakabadhi ghalani, mfumo huu umeingia dosari kwa baadhi ya maeneo kama Mtama kwa Nape baadhi ya wakulima mpaka sasa wanahangaika bila kupata msaada na majibu ya kutosha baada ya Majina yao kuwepo kwenye orodha ya malipo awamu ya pili, lakini wanapoenda banki hawakuti pesa.

Wakimuuliza Kiongozi/Mwenyekiti wa Chama cha Ushirika ambao wanaandaa hundi na kupeleka benki husika wamekuwa wakiazungusha wananchi na kuwalaghai ya kuwa hundi zilikosewa, wakati wengine huombwa stakabadhi ili wathibitishe na wakiziacha tu kwa uelewa mdogo wa kisheria basi viongozi hao huzipoteza na kukosekana ushahidi.

Zoezi la kulipa kwa awamu ya Pili lilifanyika mwezi wa November 2017 lakini mpaka leo hakuna kinachojulikana.Tafadhali Mamlaka ya Korosho wasaidieni hawa wakulima ambao wanateseka kudai pesa zao.

MTAMA ya Mh. Nape, Mh. Majaliwa, Mh. Magufuli, bado kuna watu wanarudisha nyuma jitihada zenu!!
 
hatari sana.
Mkuu kuna watu hawaogopi chochote Nchi hii hasa linapokuja swala la Pesa tena hata hawaoni aibu...................!!!! wenyeviti wa Vijiji, Diwani, Katibu Tarafa na wengine wapo lakini wamekaa kimywa wakati wananchi wakidhulumiwa Haki zao...............!!!! Bodi ya Korosho na Vyama vya Msingi ni Tatizo sana..................!!!
 
Taarifa nilizozipata pia Kutoka wilaya ya Masasi Mtwara kuna wakulima mpaka leo hii 2018 hawajalipwa pesa zao za kuuza korosho za mwaka Juzi (2016). Hii ni dhuluma kubwa ambayo haivumiliki, nashindwa kuelewa Viongozi wa Kata mpaka Vijiji hawalioni hili? au ni Mtandao? Jamani hivi Mhe MAJALIWA na Mh. Rais watayafanya mangapi? Chaguzi zinakuja hizi 2020 siyo mbali, tuwatumikie wananchi. Kila jambo lina uvumilivu wake!
 
Watu waliopo Mikoa ya Kusini yaani Lindi na Mtwara leteni mrejesho huko kwani nasikia wahusika wameshaanza vikao, kunani?
 
Imekuwaje watu wapo kimywa kwenye swala kubwa linalogusa Matarajio ya wengi. Je, kesho na kesho kutwa wakulima wakigoma kuuza Korosho zao kwenye vyama vya Msingi. Lawama atabeba nani?
 
Lakini wakulima walitakiwa wawe wamefungua account bank, walifanya hivyo???
Mkuu kwa mujibu ya baadhi ya wakulima ni kuwa lazima wafungue account kwa benki. Kilichofanyika/Kinachofanyika ni kuwa Majina ya walioingiziwa pesa Benki huwekwa kwenye mbao za matangazo lakini wakulima wanapokwenda benki hawakuti chochote na wakirudi kwa chama cha Ushirika huombwa Stakabadhi za Mauzo kuthibitisha.

Hapo kwa Uelewa Mdogo wa Baadhi ya Wakulima huambiwa waziache Stakabadhi zao na mwisho wa yote Hupotezwa na mkulima hukosa haki yake, wengine Wanaojitambua huondoka nazo na wakikomaa huambiwa wakati wa kuandika hundi walikosea kuandika account namba hivyo wafanye subra, hapo napo ndiyo imetoka ni kesho kesho kutwa wakienda kwa Diwani au Polisi wanaambiwa hilo ni swala la madai wawaone wahusika wawalipe! Kwa kweli vyama vya USHIRIKA ni tatizo hebu fikiri kuna wakulima ambao tangu mwaka 2016 mpaka leo hii hawajalipwa.

Wakulima wa korosho bado hawaridhishi na utaratibu wa STAKABADHI Ghalani hasa kwa hawa watu/Wezi wanaojifanya wamekosea account namba na pesa kuzihamishia kwenye account wanazozijua wao!

WAMELALA USINGIZI AU WANASHIRIKI UONEVU/WIZI HUU RC Makonda uko vizuri.

 
Mkuu kwa Mujibu ya Baadhi ya Wakulima ni kuwa Lazima Wafungue Account kwa Benki.....Kilichofanyika/Kinachofanyika ni kuwa Majina ya walioingiziwa pesa Benki huwekwa kwenye mbao za Matangazo.......Lakini Wakulima wanapokwenda Benki hawakuti chochote na wakirudi kwa chama cha Ushirika huombwa Stakabadhi za Mauzo kuthibitisha.....Hapo kwa Uelewa Mdogo wa Baadhi ya Wakulima huambiwa waziache Stakabadhi zao na mwisho wa yote Hupotezwa na mkulima hukosa haki yake, wengine Wanaojitambua huondoka nazo na wakikomaa Huambiwa wakati wa kuandika Hundi walikosea Kuandika Account namba hivyo wafanye Subra....Hapo napo ndiyo imetoka ni kesho kesho Kutwa............Wakienda kwa Diwani au Polisi wanaambiwa hilo ni swala la madai wawaone wahusika wawalipe....................!!!!!! Kwa kweli Vyama vya USHIRIKA ni tatizo hebu fikiri kuna wakulima ambao tangu mwaka 2016 mpaka leo hii hawajalipwa...............

Wakulima wa Korosho bado Hawaridhishi na Utaratibu wa STAKABADHI Ghalani..................hasa kwa hawa watu/Wezi wanaojifanya wamekosea Account Namba na pesa kuzihamishia kwenye Account wanazozijua wao........................!!!!

WAMELALA USINGIZI AU WANASHIRIKI UONEVU/WIZI HUU RC Makonda uko vizuri......

Hii AMCOS iko chini ya MAMCU au TANECU?
 
hii AMCOS iko chini ya MAMCU au TANECU...?
Mkuu hayo tuyaache........Lakini elewa na REGISTRAR OF COOPERATIVE SOCIETIES wanachotakiwa kujua ni kwamba Account wakulima wamefungua na Viongozi wanazijua ila Unajua Tena MWIZI amejua njia nyingine ya kujifanya WALIKOSEA account namba.............na hapo ndipo shida Hutokea Ukiuliza wamepeleka kwa Account gani hawataki kusema.....................!!!!
 
Mkuu hayo tuyaache........Lakini elewa na REGISTRAR OF COOPERATIVE SOCIETIES wanachotakiwa kujua ni kwamba Account wakulima wamefungua na Viongozi wanazijua ila Unajua Tena MWIZI amejua njia nyingine ya kujifanya WALIKOSEA account namba.............na hapo ndipo shida Hutokea Ukiuliza wamepeleka kwa Account gani hawataki kusema.....................!!!!

kwa sasa wamepotea hao wakidakwa kwa kweli....
 
leo watu wa CRDB na NMB Walikuwepo hapa MTAMA Afisa mtendaji amewaka kweli kwa swala hili na amewapa wahusika walipe wananchi ndani ya siku tatu........ngoja tuone.........!! mambo ni Motoooooo................
 
Hatimae baadhi ya Wakulima wamelipwa Haki yao. Shukrani ziwaendee Afisa Mtendaji wa Kata ya Mtama na Afisa Mtendaji wa kijiji cha Makonde, Watu wa Benki ya CRDB na NMB matawi ya Lindi, Mkuu wa Wilaya ya Lindi na Team yake kwa Jitihada zao za Kuhakikisha Haki ya Mkulima Haipotei na Kutoa Elimu ya Wizi wa Mtandaoni hasa kwa njia ya Kibenki. SHUKRANI SANA

ANGALIZO:

Pamoja na kazi Mzuri iliyofanyika na Mkuu wa Wilaya, lakini kuna watu bado wanasota hawajui wafuate taratibu zipi kupata haki yao kwani hata Jopo la Mkuu wa Wiaya walipokuja Mtama wananchi wachache waljitokeza eidha kwa kuwa wakati huu ni wa Kilimo hivyo wengi kuwa Mashambani. Lakini bado kuna ukakasi kwani wale ambao walijitokeza walielekezwa kwenye Ofisi za chama cha msingi cha Ushirika wakati wageni walikuwa kwenye Ofisi ya Mtendaji Kata hivyo kukosa nafasi ya kutoa Malalamiko yao juu ya Chama cha Msingi cha Ushirika Cha Mtama kutowalipa pesa zao za Mazao ya Korosho. Chama cha Ushirika hili wanahusika kuficha Maovu yao!

Msajili wa Vyama vya Msingi vya Ushirika, Malengo na Dira yenu iko vizuri na nakiri kabisa ya kuwa mmekuwa mukiondoa Vyama pamoja na Viongozi wao wasio waaminifu kwa Wakulima jambo ambalo kwa baadhi ya Wakulima wanaona Mpango mzima wa Stakabadhi Ghalani ni WIZI.

Hivyo basi ni vizuri kuvifuatilia kwa karibu vyama hivi ili kubaini mapungufu ya makusudi kwa nia ya kutenda uhalifu Unawezaje kuandika HUNDI na kuipeleka kwenye Account ya Mtu asiyejulikana na Mkulima kukosa pesa...........Mkulima akifuatilia Huzungushwa bila mafanikio. NI WIZI AMBAO HAUTAKIWI KUFUMBIWA MACHO.

Pia nichukue nafasi hii tena kuwashukuru Afisa Mtendaji wa Kata ya Mtama, CRDB lindi na NMB lindi, Mkuu kabanga, RC Makonda wa Dar Mpya, na Mkurugenzi wa REGISTRAR OF COOPERATIVE SOCIETIES. kwa dondoo na maelekezo yenu kwa kweli yamezaa Matunda ingawa bado kungali wengine wanalia. Mungu awaongezee Hekima na Busara.
 
Hatimae baadhi ya Wakulima wamelipwa Haki yao..............Shukrani ziwaendee Afisa Mtendaji wa Kata ya Mtama na Afisa Mtendaji wa kijiji cha Makonde, Watu wa Benki ya CRDB na NMB matawi ya Lindi, Mkuu wa Wilaya ya Lindi na Team yake kwa Jitihada zao za Kuhakikisha Haki ya Mkulima Haipotei na Kutoa Elimu ya Wizi wa Mtandaoni hasa kwa njia ya Kibenki...............!!! SHUKRANI SANA

ANGALIZO;
Pamoja na kazi Mzuri iliyofanyika na Mkuu wa Wilaya, lakini kuna watu bado wanasota hawajui wafuate taratibu zipi kupata haki yao kwani hata Jopo la Mkuu wa Wiaya walipokuja Mtama wananchi wachache waljitokeza eidha kwa kuwa wakati huu ni wa Kilimo hivyo wengi kuwa Mashambani......Lakini bado kuna ukakasi kwani wale ambao walijitokeza walielekezwa kwenye Ofisi za chama cha msingi cha Ushirika wakati wageni walikuwa kwenye Ofisi ya Mtendaji Kata hivyo kukosa nafasi ya kutoa Malalamiko yao juu ya Chama cha Msingi cha Ushirika Cha Mtama kutowalipa pesa zao za Mazao ya Korosho...................Chama cha Ushirika hili wanahusika kuficha Maovu yao.......!!!

Msajili wa Vyama vya Msingi vya Ushirika, Malengo na Dira yenu iko vizuri na nakiri kabisa ya kuwa mmekuwa mukiondoa Vyama pamoja na Viongozi wao wasio waaminifu kwa Wakulima jambo ambalo kwa baadhi ya Wakulima wanaona Mpango mzima wa Stakabadhi Ghalani ni WIZI........
Hivyo basi ni vizuri kuvifuatilia kwa karibu vyama hivi ili kubaini mapungufu ya makusudi kwa nia ya kutenda uhalifu...............Unawezaje kuandika HUNDI na kuipeleka kwenye Account ya Mtu asiyejulikana na Mkulima kukosa pesa...........Mkulima akifuatilia Huzungushwa bila mafanikio...............!!!! NI WIZI AMBAO HAUTAKIWI KUFUMBIWA MACHO...............

Pia nichukue nafasi hii tena kuwashukuru Afisa Mtendaji wa Kata ya Mtama, CRDB lindi na NMB lindi, Mkuu kabanga, RC Makonda wa Dar Mpya, na Mkurugenzi wa REGISTRAR OF COOPERATIVE SOCIETIES. kwa dondoo na maelekezo yenu kwa kweli yamezaa Matunda ingawa bado kungali wengine wanalia..................Mungu awaongezee Hekima na Busara...............
Haya haya haya haya kunekucha Lindi na Mntwara kuchele. Bila utapeli nchi nlingekuwa mbali sana. Watu kwenye vyama vya usharika kuna wizi Sana
 
Haya haya haya haya kunekucha Lindi na Mntwara kuchele. Bila utapeli nchi nlingekuwa mbali sana. Watu kwenye vyama vya usharika kuna wizi Sana
Ni kweli mkuu, lakini wapo viongozi waadilifu ambao nao huzungukwa, mwizi ana mbinu nyingi!
 
ni kweli mkuu......... lakini wapo viongozi waadilifu ambao nao huzungukwa........ mwizi ana mbinu nyingi............!!!
PM mhe Majaliwa awawashia Moto Viongozi wa Masasi Mtwara juu ya Vyama vya msini vya Ushirika..............Hongera sana PM.................!!!
 
Pamoja na Jitihada kubwa zinazofanywa na Serikali ya Awamu ya Tano kuboresha zao la Korosho kwa Wakulima kupata Bei Mzuri ambayo haijawahi kutokea hapo nyuma kwa Mfumo wa Stakabadhi Galani, Mfumo huu umeingia Dosari kwa baadhi ya Maeneo kama MTAMA kwa NAPE baadhi ya wakulima Mpaka sasa wanahangaika bila kupata Msaada na Majibu ya kutosha baada ya Majina yao kuwepo kwenye orodha ya malipo awamu ya Pili lakini wanapoenda Banki hawakuti pesa.........Wakimuuliza Kiongozi/Mwenyekiti wa Chama cha Ushirika ambao wanaandaa Hundi na kupeleka Benki husika wamekuwa wakiazungusha wananchi na kuwalaghai ya kuwa Hundi zilikosewa, wakati wengine huombwa stakabadhi ili wathibitishe na wakiziacha tu kwa Uelewa Mdogo wa kisheria basi Viongozi hao huzipoteza na kukosekana ushahidi....................Zoezi la kulipa kwa awamu ya Pili lilifanyika mwezi wa November 2017 lakini mpaka leo hakuna kinachojulikana.........

Tafadhali Mamlaka ya Korosho wasaidieni hawa Wakulima ambao wanateseka kudai Pesa zao............
MTAMA ya Mhe NAPE, Mhe MAJALIWA, Mhe MAGUFULI.....................Bado kuna watu wanarudisha nyuma Jitihada zenu.....................!!!!
Mbona mwaka huu hujaripot kuhusu suala la Serikali kutolipa na kuchelewa kuwalipa wakulima wa Korosho.
 
Una lako jambo Mkuu...........!!!!Kulikoni kwa sasa Nipo Kiwangwa Bwagamoyo..... Nayalia timing Mananasi..... Zao la Korosho pasua Kichwa.......Mara Watu wakuibie shambani mara stakabadhi Ghalani Mara usubiri Mnada mara kaangalie benki Pesa yako...... Hapo usisahau maswala ya Pembejeo ni shida tu.......
 
Back
Top Bottom