Mwanahabari Huru
JF-Expert Member
- Mar 9, 2015
- 14,242
- 34,917
Viongozi waandamizi wa CCM ( katibu mkuu, Abdulrahman Kinana na katibu mwenezi ndugu Nape Moses Nauye), wamemtukana mwenyekiti wao wa CCM Mh. Jakaya Mrisho Kikwete.
Wakihutubia kwa mbwembwe wilaya ya Kyerwa, vijiji vya Biharamulo na Kahama, walisimama jukwaani ambapo pamoja na uongo mwingi wa kuwadanganya wananchi kuwa wanawapenda, waliamua kusema wanataka sheria ya manunuzi ifutwe kwani inasababisha:
1. Urasimu mkubwa,
2. Badala ya kuondoa/ kuziba mianya ya rushwa imeongeza,
3. Inawazuia watu kufanya maamuzi bila kuingiliwa!
Wakati akipendekeza na kuagiza hayo mshauri huyo, mwenyekiti wake leo tarehe 18/6/2015, amesema kabla hajatoka madarakani anajivunia kupunguza rushwa kupitia sheria ya manunuzi (public procurement Act PPA).
Sasa watuambie : nani yuko sahihi? Pili, wakati akijinasibu kupunguza rushwa, mbona wakurugenzi wake wamepitiwa na CAG, bwana Assad na kusema halmashauri karibu zote zinazoongozwa na CCM zinaongoza kwa hati chafu?
Wakihutubia kwa mbwembwe wilaya ya Kyerwa, vijiji vya Biharamulo na Kahama, walisimama jukwaani ambapo pamoja na uongo mwingi wa kuwadanganya wananchi kuwa wanawapenda, waliamua kusema wanataka sheria ya manunuzi ifutwe kwani inasababisha:
1. Urasimu mkubwa,
2. Badala ya kuondoa/ kuziba mianya ya rushwa imeongeza,
3. Inawazuia watu kufanya maamuzi bila kuingiliwa!
Wakati akipendekeza na kuagiza hayo mshauri huyo, mwenyekiti wake leo tarehe 18/6/2015, amesema kabla hajatoka madarakani anajivunia kupunguza rushwa kupitia sheria ya manunuzi (public procurement Act PPA).
Sasa watuambie : nani yuko sahihi? Pili, wakati akijinasibu kupunguza rushwa, mbona wakurugenzi wake wamepitiwa na CAG, bwana Assad na kusema halmashauri karibu zote zinazoongozwa na CCM zinaongoza kwa hati chafu?