Mkuu Ritz, heshima kwako!!!
CHADEMA hakina ulazima wa kujibu hoja za Cameron. Wenye ulazima huo ni chama tawala (CCM) ambao wameendekeza kuifanya budget ya TZ kuwa tegemezi kwa miaka 50 sasa. Cha kushangaza ni kwamba nchi ina rasilimali za kutosha kabisa kutosheleza mahitaji yake yote ila kwa umbumbumbu wa MAGAMBA, wameamua kuwapa wawekezaji uchwara maliasili za nchi bure kabisa....and then hao hao tuliwapa mali zetu bure kupitia mikataba hovyo kabisa leo hii wametudharau kiasi kwamba eti wanatupa sharti la kukubali ushoga ndio watupe misaada yao.
Serikali ya MAGAMBA imetufikisha pabaya sana.
CHADEMA hakina ulazima wa kujibu hoja za Cameron. Wenye ulazima huo ni chama tawala (CCM) ambao wameendekeza kuifanya budget ya TZ kuwa tegemezi kwa miaka 50 sasa. Cha kushangaza ni kwamba nchi ina rasilimali za kutosha kabisa kutosheleza mahitaji yake yote ila kwa umbumbumbu wa MAGAMBA, wameamua kuwapa wawekezaji uchwara maliasili za nchi bure kabisa....and then hao hao tuliwapa mali zetu bure kupitia mikataba hovyo kabisa leo hii wametudharau kiasi kwamba eti wanatupa sharti la kukubali ushoga ndio watupe misaada yao.
Serikali ya MAGAMBA imetufikisha pabaya sana.
Wanabodi.
Chama cha demokrasia na maendeleo (Chadema) kinatakiwa kiweke wazi msamamo kwa watanzania mahusiano yao na chama cha Conservative cha Uingereza..
Conservative ni wadhili wakubwa wa Chadema wanawapa misaada mingi sana Chadema.
Tunakumbuka 2005 na 2010 Chadema walipokea misaada mingi kutoka Conservative, Pikipiki, Magari, Baiskeli, pamoja na pesa..
Waziri mkuu wa Uingereza Davidi Cameron, kutoka chama cha Conservative, alitoa kauli kwenye mkutano wa nchi wanachama wa Jumuia ya Madola (CHOGM) uliofanyika Perth, Australia..
Nchi zinazoomba misaada kwao zitambue haki za mashoga kama moja ya masharti ya kupewa misaada hiyo..
Tunaomba viongozi wa Chadema walitolee maelezo jambo hili sababu kati ya wanaopokea misaada Chadema nao inapokea