Challenge ya kusave pesa UTT

Inaruhusiwa kufungua mifuko zaidi ya mmoja?
Ruksa shekhe ni wewe na pesa zako tu.

Ila kuna mifuko yenye low risk na mifuko yenye moderate risk.

Kwa sisi masikini kuelekea kipato cha kati na pesa zetu za kudunduliza huwa wanashauri ufungue mifuko yenye low risk kama LIQUID/UKWASI FUND na BOND FUND.
 
Elezea hiyo ukwasi ya utt...nikiweka million 230 napata kiasi gani kwa mwezi
 
Hongera mkuu
mzabzab pitia hichi kitabu kuna madini mengi ila kama upo Daslam nenda posta kwenye jengo la SUKARI HOUSE.Hapo ndipo makao makuu ya UTT.

Utapata elimu au kijisemina kifupi kama nusu saa ndani ya kumbi zao zilizo nadhifu full kiyoyozi na utaelewa kiundani.Elimu yao ni bure.

Pia kwa hapo makao makuu utapata huduma zote.

📌Beba pasport size na kitambulisho cha nida na account namba za benki unazotaka uwe unapokelea pesa.

wapo wazi siku za kazi na jumamosi mpaka saa nane mchana.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…