Challenge: Ulipata GPA ya ngapi Chuo Kikuu?

Hicho alichokwambia maana yake ni nini
 
Hilo ndo tatizo kubwa la ukabila, wahaya mnapeana majibu humo chuoni?
Umepindisha ukweli tuu huyo lecturer alikupa hint kwenye open book exam lazima.
 
Big Up Mkuu
 
Kupata gpa ya 4 chuo huo ni wendawazimu...watu mlikua mnapenda ligi za kushindana mpaka chuoni?

Mimi nilikula zangu3.6 tena kwa mbinde sana
 
GPA ni takataka kama haikusaidii

wapo waliopata Gpa za 2.5 wanakula maisha kwenye vitengo wakati wale wenye 4.0+ wapo kitaa hawana ramani au wapo kampuni za mishahara kiduchu kazi mlima.
GPA kweli sio issue sana unaweza kuwa na GPA ya 3 na ukala kitengo kizuri tu serikalini bado wenye na GPA za 4 au 5 wakabaki kitaa wanasota maana mfumo wa sekretarieti ya ajira katika utumishi wa umma wanachoangalia ni ufaulu interview tu hawajali GPA ya ngapi we faulu interview tu wanakupa kitengo,japo nashauri vijana wapate GPA nzuri maana kuna taasisi nyingine hauwezi pata kazi kwa utaratibu maalumu bila kuwa na GPA kubwa kwa mfano BOT ,na kazi za lecturerers
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…