Chakula ni ibada kamili

Chakula ni ibada kamili

Mshana Jr

Platinum Member
Joined
Aug 19, 2012
Posts
360,032
Reaction score
828,826
Chakula ni ibada kamili, kisichezewe, kisitupwe, kisiharibiwe.

Chakula ni mojawapo ya mambo ambayo huileta familia pamoja na kujumuika wote, ni sehemu ambapo hufanyika sala na dua ya shukrani huku wakikumbukwa wale wote ambao hawakujaaliwa kupata mlo aidha kwa ugonjwa au kwa kukosa pesa nk. Chakula ni ibada kamili kwakuwa kilipitia hatua nyingi toka kupandwa kwake mpaka kukufikia wewe hapo mezani na ukajaaliwa kukila.

Chakula hakitupwi kwa namna yoyote ile labda kiwe kibovu na hakifai kuliwa, chakula ni kwa ajili ya faida ya mwili ili uweze kupata nguvu na afya za kumtumikia mungu wako na taifa na wote wenye uhitaji, chakula si ladha, ladha ni mdomoni tu. Mbwembwe zote za mapishi ni kwa ajili ya mdomo na ulimi wake basi!!! Kuna watu wana tabia ya kuagiza chakula kingi na kushindwa kukimaliza huu ni uharibifu na laana, wakati wewe unachezea chakula kuna mtu anahitaji japo robo tu ya hicho ili aweze kuishi tena!

Tukitunze na kukithamini chakula, tupo hivi tulivyo kwakuwa tunakula, chakula ni uhai na ibada kamil
 
Chakula ni ibada kamili, kisichezewe, kisitupwe, kisiharibiwe.

Chakula ni mojawapo ya mambo ambayo huileta familia pamoja na kujumuika wote, ni sehemu ambapo hufanyika sala na dua ya shukrani huku wakikumbukwa wale wote ambao hawakujaaliwa kupata mlo aidha kwa ugonjwa au kwa kukosa pesa nk. Chakula ni ibada kamili kwakuwa kilipitia hatua nyingi toka kupandwa kwake mpaka kukufikia wewe hapo mezani na ukajaaliwa kukila.

Chakula hakitupwi kwa namna yoyote ile labda kiwe kibovu na hakifai kuliwa, chakula ni kwa ajili ya faida ya mwili ili uweze kupata nguvu na afya za kumtumikia mungu wako na taifa na wote wenye uhitaji, chakula si ladha, ladha ni mdomoni tu. Mbwembwe zote za mapishi ni kwa ajili ya mdomo na ulimi wake basi!!! Kuna watu wana tabia ya kuagiza chakula kingi na kushindwa kukimaliza huu ni uharibifu na laana, wakati wewe unachezea chakula kuna mtu anahitaji japo robo tu ya hicho ili aweze kuishi tena!

Tukitunze na kukithamini chakula, tupo hivi tulivyo kwakuwa tunakula, chakula ni uhai na ibada kamil

Ujume mzuri sana. nitaufikisha kwa wengine pia!
 
Cant digest dume linaposema...... Mwaaaah mamito!!
 
kuna watu hata kupata mlo mmoja ni inshu jamani,pia tuwe na moyo mwepesi wa kuwasaidia wahitaji kwa chakula na mengineyo
Nasi tujifunze kukiheshimu na kukitumia ipasayo bila kukichezea kwa namna yoyote ile
Unapakua sahani nzima halafu unakula nusu, huu ni uharibifu mkubwa na kufisidi chakula
 
1466926948981.jpg
1466926954642.jpg
 
Somo zuri mkuu,ukitaka kuona uzito wa somo hili uwe na mgonjwa pale muhimbili,unakuta nyie mmejaa kwa mgonjwa wenu na mafurushi ya vyakula,lakini pembeni kalala mgonjwa hana hata ndugu mmoja na hana hata uwezo wa kununua kikombe cha chai,hali hii huwa inaniumiza sana, Mwenyezi MUNGU na azidi kutukumbusha kuwa duniani tu wapitaji tu,tuwasaidie wahitaji.
 
Somo zuri mkuu,ukitaka kuona uzito wa somo hili uwe na mgonjwa pale muhimbili,unakuta nyie mmejaa kwa mgonjwa wenu na mafurushi ya vyakula,lakini pembeni kalala mgonjwa hana hata ndugu mmoja na hana hata uwezo wa kununua kikombe cha chai,hali hii huwa inaniumiza sana, Mwenyezi MUNGU na azidi kutukumbusha kuwa duniani tu wapitaji tu,tuwasaidie wahitaji.
Au mgonjwa wenu ashindwe kabisa kula hayo mapochopocho kutokana na hali yake ya ugonjwa. ..kuna vitu ukivitafakari kwa undani wake vinatisha sana
 
Mfano kwenye shughuli,muda wa chakula unakuta mtu anapakua kila aina ya chakula,mwanzo wa meza hadi mwisho,halafu anakula kiduchu anaacha sahani imejaa,sasa kama unajua huwezi kula sana ulipakua chote cha nini?na unakuta kuna wengine wamekosa.
 
Mfano kwenye shughuli,muda wa chakula unakuta mtu anapakua kila aina ya chakula,mwanzo wa meza hadi mwisho,halafu anakula kiduchu anaacha sahani imejaa,sasa kama unajua huwezi kula sana ulipakua chote cha nini?na unakuta kuna wengine wamekosa.
Ubinafsi choyo ulafi na kujipenda kulikopitiliza ni ibada za kishetani. ...
Hao hawana tofauti na kuua mwingine ili mambo yake yamwendee vema
 
Back
Top Bottom