Chakula cha mchana kwa wanafunzi; Sababu isiyotajwa kwenye taaluma mbovu ya mtoto

sepema

JF-Expert Member
Jun 13, 2019
591
1,000
Salaam waungwana, poleni na hongereni nyote mnaopambana kuutafuta mkate wenu wa kila siku.

Naomba niende kwenye mada.

Binadamu ama kiumbe yeyote iki awe katika ustawi unaotakiwa ni lazima apate mahitaji muhimu ya kumuwezesha kuishi. Miongoni mwa mahitaji muhimu kwa kiumbe hai ni chakula, mengine yatafuata baada ya shibe. Wanafunzi hasa wa ngazi ya shule za msingi na sekondari ni moja Kati ya viumbe hai hivyo nao suala la chakula sio lakupuuza kabisa.

Nimeshawishika kuandika haya baada ya kutembelea shule kadhaa huku wilayani kwangu nilipo. Picha niliyoipata nikwamba wanafunzi wengi hasa wa kutwa hawapati chakula cha mchana shuleni huku ratiba ya shule ikienda hadi saa 10 jioni. Nimebahatika kuongea na baadhi ya wanafunzi ambapo walieleza kuwa wengi wao wanaondoka nyumbani asubuhi bila kupata kitu chochote hali inayosababishwa na Hali ngumu ya maisha huko majumbani kwao.

Watoto hawa wanaambiwa na wazazi wao wavumilie hadi jioni wakirudi nyumbani watakuta chakula ambacho pia hakina uhakika. Wanaeleza kuwa utimamu wa akili huanza kupotea kuanzia saa 4 asubuhi ambapo wengi husinzia madarasani. Changamoto hii imeathiri maendeleo yao kitaaluma Jambo linalosababisha kufanya vibaya kwenye mitihani yao. Nani alaumiwe, serikali au mzazi.? Wazazi wanadai hawana uwezo wakuchangia chakula cha mchana shuleni na wakati huo wanaamini hilo nijukumu la Serikali kuhakikisha wanafunzi wanapata chakula wawapo shuleni.

Serikali nayo inahamasisha wazazi kuhakikisha watoto wao wanakula shuleni kwa kuwachangia. Serikali nayo inaamini hili nijukumu la mzazi sawa na lile la kununua kalamu, sare na madaftari. Wakati hizi pande mbili zinavutana kuhusu chakula tukumbuke kuwa huyu mwanafunzi anapoteza umakini wakusikiliza kuanzia saa 4 asubuhi.

Tutarudi na roho zetu?

NB: Sina picha za mtoto mwenye njaa.
 
Kuna shule za sekondari wanakunywa uji, msosi wa mchana na jioni lakini watoto ni Vibuyu tu. Kula shuleni watoto sio mbaya ila ubaya unaanzia kwenye kukipata hicho chakula.

Wazazi wabishi, hawachangi Kuna shule nyingi walianzisha mfumo huo Lakini ulikufa kisa ushiriki hafifu.

Labda Kama serikali ipo tayari kulisha watoto wote kuanzia msingi na sekondari ila wazazi mtawaua tu hawachangi.
 
Maisha ya kijijini hasa ile miaka yetu ilikua changamoto sana sana sana.

Yani ukitoka shuleni na wazazi ndio wanarudi kutoka shamba, hapo wote msaidiane ili ugali ushushwe.

Was hard life I never forgot.
 
Salaam waungwana, poleni na hongereni nyote mnaopambana kuutafuta mkate wenu wa kila siku.

Naomba niende kwenye mada.

Binadamu ama kiumbe yeyote iki awe katika ustawi unaotakiwa ni lazima apate mahitaji muhimu ya kumuwezesha kuishi. Miongoni mwa mahitaji muhimu kwa kiumbe hai ni chakula, mengine yatafuata baada ya shibe. Wanafunzi hasa wa ngazi ya shule za msingi na sekondari ni moja Kati ya viumbe hai hivyo nao suala la chakula sio lakupuuza kabisa.

Nimeshawishika kuandika haya baada ya kutembelea shule kadhaa huku wilayani kwangu nilipo. Picha niliyoipata nikwamba wanafunzi wengi hasa wa kutwa hawapati chakula cha mchana shuleni huku ratiba ya shule ikienda hadi saa 10 jioni. Nimebahatika kuongea na baadhi ya wanafunzi ambapo walieleza kuwa wengi wao wanaondoka nyumbani asubuhi bila kupata kitu chochote hali inayosababishwa na Hali ngumu ya maisha huko majumbani kwao.

Watoto hawa wanaambiwa na wazazi wao wavumilie hadi jioni wakirudi nyumbani watakuta chakula ambacho pia hakina uhakika. Wanaeleza kuwa utimamu wa akili huanza kupotea kuanzia saa 4 asubuhi ambapo wengi husinzia madarasani. Changamoto hii imeathiri maendeleo yao kitaaluma Jambo linalosababisha kufanya vibaya kwenye mitihani yao. Nani alaumiwe, serikali au mzazi.? Wazazi wanadai hawana uwezo wakuchangia chakula cha mchana shuleni na wakati huo wanaamini hilo nijukumu la Serikali kuhakikisha wanafunzi wanapata chakula wawapo shuleni.

Serikali nayo inahamasisha wazazi kuhakikisha watoto wao wanakula shuleni kwa kuwachangia. Serikali nayo inaamini hili nijukumu la mzazi sawa na lile la kununua kalamu, sare na madaftari. Wakati hizi pande mbili zinavutana kuhusu chakula tukumbuke kuwa huyu mwanafunzi anapoteza umakini wakusikiliza kuanzia saa 4 asubuhi.

Tutarudi na roho zetu?

NB: Sina picha za mtoto mwenye njaa.
Ushauri wako ni ?
 
Tukimaliza Suala la chakula cha watoto,
Tuje suala la posh ya nauli kwa walimu.
Hawana posh kabisa wanafundisha kwa stress sana,kiwango cha ufundishaji kinakuwa chini mno,maana madeni ya kwa mangi,mikopo,wanasomesha na wao kodi ya nyumba tcheee full stressed.
 

Attachments

  • 255744740850_status_355898da088d4575b9b29e17a9fe2b27.mp4
    1.8 MB
Nashukurui wazaz wangu nilikuwa napata. Chakula mchana ugali na maharage na j tano wali maharage
Bas Kuna vijaana walikuwa wanajiona mabishoo mbaya hawali chakul Cha shule walikuja kufeli Sana vibaya kwani mm nikishakula hyo saa nane saa Tisa narudi kukamua had saaa kumi na moja ndipo Sasa nirudi Kijiji kwetu
 
Salaam waungwana, poleni na hongereni nyote mnaopambana kuutafuta mkate wenu wa kila siku.

Naomba niende kwenye mada.

Binadamu ama kiumbe yeyote iki awe katika ustawi unaotakiwa ni lazima apate mahitaji muhimu ya kumuwezesha kuishi. Miongoni mwa mahitaji muhimu kwa kiumbe hai ni chakula, mengine yatafuata baada ya shibe. Wanafunzi hasa wa ngazi ya shule za msingi na sekondari ni moja Kati ya viumbe hai hivyo nao suala la chakula sio lakupuuza kabisa.

Nimeshawishika kuandika haya baada ya kutembelea shule kadhaa huku wilayani kwangu nilipo. Picha niliyoipata nikwamba wanafunzi wengi hasa wa kutwa hawapati chakula cha mchana shuleni huku ratiba ya shule ikienda hadi saa 10 jioni. Nimebahatika kuongea na baadhi ya wanafunzi ambapo walieleza kuwa wengi wao wanaondoka nyumbani asubuhi bila kupata kitu chochote hali inayosababishwa na Hali ngumu ya maisha huko majumbani kwao.

Watoto hawa wanaambiwa na wazazi wao wavumilie hadi jioni wakirudi nyumbani watakuta chakula ambacho pia hakina uhakika. Wanaeleza kuwa utimamu wa akili huanza kupotea kuanzia saa 4 asubuhi ambapo wengi husinzia madarasani. Changamoto hii imeathiri maendeleo yao kitaaluma Jambo linalosababisha kufanya vibaya kwenye mitihani yao. Nani alaumiwe, serikali au mzazi.? Wazazi wanadai hawana uwezo wakuchangia chakula cha mchana shuleni na wakati huo wanaamini hilo nijukumu la Serikali kuhakikisha wanafunzi wanapata chakula wawapo shuleni.

Serikali nayo inahamasisha wazazi kuhakikisha watoto wao wanakula shuleni kwa kuwachangia. Serikali nayo inaamini hili nijukumu la mzazi sawa na lile la kununua kalamu, sare na madaftari. Wakati hizi pande mbili zinavutana kuhusu chakula tukumbuke kuwa huyu mwanafunzi anapoteza umakini wakusikiliza kuanzia saa 4 asubuhi.

Tutarudi na roho zetu?

NB: Sina picha za mtoto mwenye njaa.
Shida ipo kwa wazazi huku kwetu Lindi mzazi kuchangia elfu tatu mwanae ale kwa wiki anaona ni nyingi sasa nani alaiumiwe hapo
 
Wazazi ni wabishi kuchangia.

Wakiambiwa wachangie pesa za shule wanasema elimu bure na tumeambiwa tusitoe kitu kila kitu serikali inalipa.

Ni mbinde kumchangisha mzazi kipindi hizi siasa ni kwenye kila kitu.
 
Shida ipo kwa wazazi huku kwetu Lindi mzazi kuchangia elfu tatu mwanae ale kwa wiki anaona ni nyingi sasa nani alaiumiwe hapo
Umeongea ukweli, Ila nazan jamii inapaswa kuelimishwa kuhusu umuhimu wa elimu. Wazaz wengi WA kusini elimu sio kipaumbele, Sana Sana elimu ya dini, wao huamin maisha sio lazima uwe na elimu mbona waoh hawana elimu na wanaishi.
Kwahyo uku kunahitajika elimu itolewe Kwa jamii kuhusu umuhimu wa elimu Kwa mtoto, jamii na Taifa kiujumla
 
Nyanda za Juu Kusini wazazi wanajitahidi sana kuchangia, tena wengine anapeleka hadi mahindi na sukari
 
Back
Top Bottom