Gazeti la Nipashe la leo ukurasa wa 8 lina habari njema kwamba Mbunge wa Mbeya mjini Mr Two akishirikiana na Bw John Mwambingija wanaongoza operesheni maalum ya kuingiza wanachama wapya wa Chadema vijijini.Operesheni hiyo inajulikana kama TWANGA KOTEKOTE.Kikosi kazi hicho kimelitikisa jimbo la Rungwe linaloshikiliwa na Prof Mark Mwandosya na Chadema imezoa mamia ya wanachama,wengine wamejitoa CCM na kujiunga na Chadema.Jimbo la Rungwe lilikuwa linaonekana kama ngome kuu ya CCM lakini Chadema wamelitikisa vilivyo na baada ya ziara ya wapiganaji hao Vijana takriban wote wamekimbilia chadema.........