CHADEMA yawasilisha pingamizi dhidi ya Zitto

CHADEMA yawasilisha pingamizi dhidi ya Zitto

gongo tu huko hakuna la maana

dah! unajitajidi kweli kupambana hadi umeamua kutumia id nyingine! kaza buti pengine utafanikiwa. nikuambie kitu, ukianguka ukachafuka jaribu kuvua ile nguo yenye matope kisha uoge, hakuna atakayejua kuwa ulichafuka. ukitembea hivyo hivyo na tope kila mtu atajua kuwa ulianguka na uko mchafu.
sasa ndugu zanguni ccm kujisafisha hamtaki, mnang'ang'ana tu kwa maneno kuwa nyie ni wasafi wakati matope bado mnayo dah! sijui tuwasaidieje? ufisadi hamtaki kuacha, uzembe kwenye uongozi hamtaki kurekebisha tutawadekeza mpaka lini wajemeni?! this time you must go bwana
 
Mzito Kabwela aende akakamilishe usajili wa ACT ili ajifunze kama kujenga chama ni kazi lelemama!
 
Wewe gamba tu. Zitto ana akili kuliko wewe mfuasi wake usiejua unafiki anaoufanya. Chadema washajua janja ya nyani yake yote hana jipya amebakia kufulia tu tumsahau
 
Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema), kimewasilisha majibu na pingamizi la awali dhidi ya Mbunge wa Kigoma Kaskazini, Zitto Kabwe kuhusu Kamati Kuu ya Chama hicho akiitaka mahakama kuzuia uanachama wake usijadiliwe hadi kesi ya msingi itakaposikilizwa.Kadhalika, chama hicho kimejibu barua ya Zitto pamoja na kuwasilisha mwenendo wa shauri lililopelekea kuvuliwa nyadhifa za uongozi katika chama hicho kama mlalamikaji alivyoomba.Majibu hayo yaliwasilishwa jana Mahakama Kuu Tanzania, Kanda ya Dar es Salaam.Mawakili wa chama hicho, Tundu Lissu na Peter Kibatala, katika pingamizi hilo kuna hoja sita na wakiitaka Mahakama kutupilia mbali kesi hiyo kwamba haina mashiko ya kisheria.Hoja hizo ni shauri hilo halina msingi kwa sababu halikuwasilishwa katika Mahakama ya chini kusikilizwa na kutolewa maamuzi kwa mujibu wa kifungu cha 13 cha Mwenendo wa Mashauri ya Madai.Limewasilishwa masijala Kuu ya Mahakama Kuu badala ya masijala ya Wilaya kinyume cha sheria na taratibu za masijala za Mahakama.Mlalamikaji hajaomba maoni ya Mahakama Kuu kuhusiana na suala linalohusiana na uanchama wake Chadema.Nyingine ni shauri halina msingi kwa sababu Zitto anaendesha mashauri mawili, Mahakama Kuu na rufaa ya kwenye Baraza Kuu la chama.Pia Mahakama Kuu siyo mahali pake kwa sababu Zitto hajatumia nafasi zilizopo ndani ya Chadema.Mahakama Kuu haina mamlaka ya kutoa maamuzi ya maombi ya kuzuia Zitto asijadiliwe uanachama wake kwa sababu ni mambo ya yanayohusu Chadema.Chadema wakijibu maombi ya msingi ya Zitto kupitia hati iliyosainiwa na Sylvester Masinde na Katibu Mkuu wa chama hicho, Dk. Wilbrod Slaa, wamedai kwamba hawana ubishi kwamba mlalamikaji alivuliwa uongozi Novemba 22, mwaka 2013.Pia, inaeleza kwamba Zitto alishiriki katika Mkutano wa Kamati Kuu na alijua kinachoendelea kuhusu tuhuma zake.Chadema inaomba Mahakama kutupilia mbali maombi ya mlalamikaji kwa kuwa hayana mashiko ya kisheria.Mapema Januari 2, mwaka huu Zitto kupitia Wakili Albert Msando, alifungua kesi mahakamani hapo dhidi ya Baraza la Wadhamini la Chama hicho na Katibu Mkuu, Dk. Slaa, akiiomba Mahakama itoe zuio la muda la Kamati Kuu kutojadili suala la uanachama wake hadi kesi ya msingi itakaposikilizwa na kutolewa maamuzi.Mahakama iliyokaa chini ya Jaji John Utamwa ilikubali na kutoa zuio la muda hadi kesi ya msingi itakapoisha.Hisani ya Nipashe
safi sana,kweli chadema ni noma,hakika ukombozi uko karibu
 
DU- Hawa CHADEMA hawa, sijawahi kuona chama cha siasa kina activities nyingi namna hii na zote zinatekelezwa kwa ufanisi namna hii.
 
Kuna Mwandishi
mmoja kutoka China anaeandikia gazeti la Raia Mwema aliwahi kuandika kuwa
Zito kwasasa hana lakufanya isipokua kuondoka Chadema, katika makala
hiyo huku akidhani kuwa nikweli Zito anaipenda sana CDM kutokana na Zito
mwenye kulalamika sana kwenye vyombo vya habali. Alimtaka ajiodoe kwani
kung'ang'ania sana madaraka kwa nguvu kunge endelea kukuza mgogoro
ndani ya chama hali ambayo ingekipotezea mvuto chama nakusababisha
kupoteza mvuto ndani ya jamii, sasa tofauti na alivyozani Mwandishi huyo
nikua Zito anachofanya sasa ni wivu, Kwakua kaona mwelekeo wa CDM
kushika Madalaka 2015
anaona Nikukivuruga ili wakose wote.
we jitekenye tu!
 
umevimbiwa ubwabwa wa msibami wewe


Yaani una manisha hawa wapo katika msiba wa CCM!!!!!!!



Kwani CCM imeshakufa kabla ya mwaka 2015!!!!! Siamini lakini !!!! inawezekana!!!

profilepic 2015.JPG


MIZAMBWA
INANIUMA SANA!!!
 
Chadema malizeni hili swala la Zitto dogo keshang‘olewa meno ya nini kumchinja, mwacheni arudi kwenye chama kaa nccr walivyofanya kwa kafulila nna uhakika ameshanyooka
 
Shida ya vijana wengi wa kitanzania ni ubishi na ushabiki wa matusi bila hoja za msingi,ukimuuliza mtu sababu ya kushabikia hana hoja ya maana
 
Back
Top Bottom