Miss Halima
Member
- Aug 4, 2026
- 45
- 73
Makada watano wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA), wamekishtaki tena chama hicho katika mahakama kuu ya Dodoma.
Walalamikaji katika shauri hilo Miscellaneous Cause No. 205810F of 2026, Barnabas Okola, Joseph Mwakidasi, Mathias Cosmas, Abubakari Mashambo na Lembruce Mchome.
Washtakiwa katika shauri hilo ni Bodi ya Wadhamini ya CHADEMA, Katibu Mkuu wa CHADEMA, Msajili wa Vyama vya Siasa na Mwanasheria Mkuu wa Serikali.
Kupitia akaunti yake katika mtandao wa X, Mkurugenzi wa Sheria na Haki za Binadamu wa CHADEMA, Gaston Garubindi, amesema amepokea wito kutoka Mahakama Kuu ya Tanzania, Masjala Kuu Dodoma, unaomtaka yeye pamoja na wahusika wengine kufika mahakamani kwa ajili ya kusikiliza shauri hilo.
Garubindi, amesema shauri hilo limepangwa kusikilizwa mbele ya Jaji A. Mruma kesho Jumatano Agosti 12, 2026, kuanzia saa 3:00 asubuhi.
“Tumepokea wito kutoka mahakama kuu, Masijala kuu Dodoma kwamba tumeshitakiwa na Katibu wa CHADEMA mkoa wa Morogoro na wenzake, shauri litakuwa mbele ya Jaji Mruma. Tumeitwa kufika mahakamani hapo tarehe 12 August 2026.
“Huu ni mwendelezo wa mbinu chafu, wanapambana na sisi lakini mwisho wa siku hawatashinda
Soma Pia: Heche: Ndani ya siku 2, Viongozi 51 wa CHADEMA wamekamatwa na kubambikiziwa Kesi za Ugaidi
“Hati hiyo imeelekeza wahusika kufika mahakamani kwa njia ya mtandao bila kukosa, pamoja na kuwasilisha nyaraka zote wanazokusudia kuzitumia katika kuunga mkono hoja zao mbele ya mahakama,” amesema Garubindi.
Walalamikaji katika shauri hilo Miscellaneous Cause No. 205810F of 2026, Barnabas Okola, Joseph Mwakidasi, Mathias Cosmas, Abubakari Mashambo na Lembruce Mchome.
Washtakiwa katika shauri hilo ni Bodi ya Wadhamini ya CHADEMA, Katibu Mkuu wa CHADEMA, Msajili wa Vyama vya Siasa na Mwanasheria Mkuu wa Serikali.
Kupitia akaunti yake katika mtandao wa X, Mkurugenzi wa Sheria na Haki za Binadamu wa CHADEMA, Gaston Garubindi, amesema amepokea wito kutoka Mahakama Kuu ya Tanzania, Masjala Kuu Dodoma, unaomtaka yeye pamoja na wahusika wengine kufika mahakamani kwa ajili ya kusikiliza shauri hilo.
Garubindi, amesema shauri hilo limepangwa kusikilizwa mbele ya Jaji A. Mruma kesho Jumatano Agosti 12, 2026, kuanzia saa 3:00 asubuhi.
“Tumepokea wito kutoka mahakama kuu, Masijala kuu Dodoma kwamba tumeshitakiwa na Katibu wa CHADEMA mkoa wa Morogoro na wenzake, shauri litakuwa mbele ya Jaji Mruma. Tumeitwa kufika mahakamani hapo tarehe 12 August 2026.
“Huu ni mwendelezo wa mbinu chafu, wanapambana na sisi lakini mwisho wa siku hawatashinda
Soma Pia: Heche: Ndani ya siku 2, Viongozi 51 wa CHADEMA wamekamatwa na kubambikiziwa Kesi za Ugaidi
“Hati hiyo imeelekeza wahusika kufika mahakamani kwa njia ya mtandao bila kukosa, pamoja na kuwasilisha nyaraka zote wanazokusudia kuzitumia katika kuunga mkono hoja zao mbele ya mahakama,” amesema Garubindi.