CHADEMA yawanasa Lowassa, Mwigulu

CHADEMA yawanasa Lowassa, Mwigulu

Hawa jamaa kete ya mabomu imewashinda sasa kete ya Mussa Tesha ya tindikali nayo chali sasa wanafukuzia wa machinga na boda boda lakini na hii itafail kweli kaburi linawanyemelea


Hiyo nayo mbona makapi tu ,walishaitumia huko Arusha na haikufua dafu ndiyo maana sasa hivi wanahasira sana na waendesha boda boda Arusha.

kwa Arusha sasa hivi wamehamia kwa madereva wa Noah.
 
Hii hoja haina mashiko kwani hawa jamaa kufanya harambee kuna shida gani kwa cdm mi naona mnalalamika kutafuta sympathy bila sababu,nyie kama mnakubalika kuna shida gani hapo.
 
Huyu mzee tu muda wake umeisha kwani sisi hatuta mchagua mgonjwa kuwa rais. Kuwa rais ni kutafuta kufa haraka kwani ataibua makubwa kuliko ya Richmund.
 
Nimejaribu kusoma mara tatu lakini bado sijaona cha ajabu. Siasa za CDM zinaonekana ni za kitoto sana kiasi kwamba wanaogopa hadi watu kurudisha kadi na kujiunga na vyama vingine. Jamani kuwa na kadi sio sababu kuwa utakipigia kura chenye hiyo kadi. Dr. Slaa ana kadi ya CCM mbona yeye ni CDM? Mnasema chama kinakubalika kisha mnaogopa mamluki? Huwa nina shaka sana na Demokrasia yenu, yaani imekua kama ya kulamishana vile. Msiogope bali chukulieni kua ni changamoto.
 
Mtalalamika mpaka lini? Chama cha dhifa ya kitaifa chama malalamiko kama mke mwenza

"To know the enemy is half the victory"
 
Hizo fedha ni halali yao wachukuwe kwani zimetokana na kodi zao,ila kama kawaida akili mkichwa.
 
Watanzania chukueni pesa ongezeni mitaji.
 
Atawanunua vijana wenye tamaa kama kina mwampamba,shoza,chris lukos, ila vijana wengi wa tz wanamsimamo. Huyo fisadi amewamaliza wote ktk chama chake kwa kuwawekea sumu na vitisho. Hadi kina mwakyembe wamesalim amri. Leo anautaka urais pamoja na uizi wake wote aliotuibia. Anatuhonga fedha ileile
 
Mimi tena ndio nimeishiwa na nguvu,Juzi tu viongozi wetu walikuwa Ikulu na watuhumiwa wakifurahi katika Dhifa ya Taifa leo tumerudi pale pale katika malalamiko yetu ya kila siku.Wakati mwingine viongozi wetu hawaeleweki na wanatukatisha tamaa hata sisi huku foot-soldiers

Hupaswi kuishiwa nguvu kamanda.Mapambano huwa yana challenges zake,na ndio maana kunahitajika mshikamano katika kipindi kigumu, na hasa vikao vya mara kwa mara kwa ajili ya kupeana feedback na the way forward ili kuweza kuhakikisha kwamba muda wote watu wako focused and in line.

Hili la harambee kwa bodaboda sio geni,ameanza nalo Mulugo huko mbeya ili kuweza kumdhohofisha Sugu,limeenda Arusha limeshindwa, sema mwanza wameliboresha kwa kujaribu vifaa vya CHADEMA virudishwe ili kuteka watu wengi zaidi.

Nalo washauri CHADEMA ni kujipanga,kwani usitegemee adui yako atarelux wakati wewe unampiga.Ni lazima nayeye ajitetee, kumbukebni hii ni vita.Nikipata muda ntajitahidi niwepo kwenye hiyo Harambee ili niweze kujaribu kusoma mawili matatu,na ikibidi tubadilishane mawazo humu ndani.

Najua MM Mwanakijiji amekua down kwa ziara ya Obama,lakini najua wakati wa mapambano kuna muda mtu unachoka ,unapumzika kidogo then munkari ukuipanda unaendelea tena.So hatupaswi kukata tamaa, mpaka mwisho.Vikwazo huwa haviepukiki.
 
Hakika hamdanganyiki kwa vile wanamwanza sasa wameanza kuona uozo wa CDM, huku kulalamika kwenye jukwaa lenu hilin la JF ni dalili kuwa maji yamewafika shingoni, ila mmechelewa.
Acha fikra mgando we thatha kama Jamii Forum ni jukwaa la CHADEMA basi na wewe ni CHADEMA. Tatizo la maccm wengi akili zenu ni Za kuzimana tu.
 
Kweli akili ndogo!!!! Huo si uoga ila ni tahadhari, umakini na ukomavu katika mapambano. Na kwa nini kila wakati ccm ni unafiki wizi ugaidi udora nu uchafu tuuu!!! mmekwisha
kama ni hujuma tu mnaogopa nini? na kama siyo kweli kuwa hamkubaliki mnaogopa nini?
 
waache wahangaike, hizo ni hela zetu walizoiba kupitia Richmonduli na symbion, pokeeni wanazirejesha kwa mtindo tofauti. Mwanza si Monduli kwamba wananchi watabadilika waende Magamba na wala si Bagamoyo, Mwanza ni kwa wajanja na si makanjanja! Ila tu wawe makini na wake zao kama Nchemba naye atakuwepo!
 
Nimewaona wapambe wao jana pale coffee shop mwanza hotel, wamejazana wananunuliwa chakula cha usiku!
Huku wakimsifia eti 'rais ajaye!?'

Roho ikaniuma sana, ukiwaangalia hali zao, unasikitika! Lakin ndo wakipewa sahani ya chips na rost kuku na wengine bia, wanajitia wamesahau shida zao!

When they wake up, they will realize that it was just a dream!! A day dream!
 
MBINU zinazosukwa na vigogo wa Chama Cha Mapinduzi (CCM), Edward Lowassa na Naibu Katibu Mkuu (Bara), Mwigulu Nchemba ili kukidhohofisha Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA) jijini Mwanza zimefichuka.

Lowassa ambaye ni Mjumbe wa Halmashauri Kuu (NEC) na Mwigulu wanatajwa kutaka kutumia harambee ya kuchangia wafanyabiashara wadogo (Machinga) eneo la Makoroboi jijini hapa leo ili kufanikisha hujuma zao hizo za kisiasa.

Kwa mujibu wa Mwenyekiti wa CHADEMA Kanda ya Magharibi, Peter Makere, kupitia idara yao ya usalama wamefanikiwa kunasa mikakati hiyo ya kutaka kuwadhoofisha.

Alisema kuna baadhi ya makada wa CCM wamejipanga kuhujumu kadi na baadhi ya vifaa vya uenezi vya CHADEMA kwa ajili ya kuvirudisha kwenye harambee hiyo ili kuhadaa umma kuwa chama hicho hakikubaliki.

Makere alisema kuwa mgeni rasmi wa harambee hiyo, ametajwa kuwa ni Waziri Mkuu aliyejiuzulu, Lowassa ambaye ataongozana na makada wengine wa CCM, akiwemo Mwigulu.

“CHADEMA Kanda ya Ziwa Magharibi, imebaini mbinu chafu na ovu zinazopangwa na makada wa CCM kuhujumu kadi na vifaa vyetu. Hujuma hizi zinaandaliwa ili kuuhadaa umma eti CHADEMA haikubaliki. Vifaa hivi vimepangwa kurudishwa kwenye harambee ya kuchangia machinga itakayoongozwa na Lowassa,” alisema.

Alisema kuwa CHADEMA kama chama makini na chenye dira thabiti ya kuwakomboa Watanzania kutoka kwenye makucha ya CCM yaliyojaa umasikini, wanaomba umma upuuze hujuma hizo na kuendeleza mapambano ya kuiondoa madarakani 2015.

Aidha, Makere aliwaomba wamachinga na wananchi wa Jiji la Mwanza bila kujali itikadi zao wapokee fedha za CCM na waongeze ujasiri na mbinu za kuiondoa madarakani katika uchaguzi mkuu ujao.

Alisema muda huu ni wa msimu, kwani baadhi ya viongozi wa CCM wanaotafuta urais kwa gharama kubwa kupitia makanisa na misikitini, wameanza kujipendekeza ili waungwe mkono, hivyo ni vema Watanzania wakawaogopa watu hao kama ukoma.

“CCM lazima ibadilike, iachane na siasa uchwara, hadaa, ghiliba na mazingaombwe. CHADEMA tunataka chama hicho kupitia viongozi wake kiwaambie Watanzania kimewafanyia nini katika sekta za elimu, afya, maji, ajira kwa zaidi ya miaka 50 ya uhuru,” alisema Makere.

Source:Tanzania Daima Ijumaa

Kuna msomi nilisha wahi kumsikia akisema Mwana CCM yeyote akisha jua anaweza kupitishwa na chama chake kuwa mgombea Urais kinachofuata sasa ni kupambana na Chadema kwani hata CCM hata kama wakimpitisha bado hawezi kushinda iwapo Chadema itakuwa kama hivi ilivyo
 
Kuishabikia ccm ni sawa na ku....kuu... shi..kii..shwa. ukuta...!!
 
Lowasa anataka kutumia umasikini wa chinga mwanza kujiimarisha, lakini kwa mwanza atakwama, aulize Muzinza Masha alivyo fanywa. Pesa yake wakaila na ubunge wakampa Wenje.
 
Jamani Lowasa ni wazuri Mkuu aliyeondolewa na kashfa ya ufisadi. Huyu Jamaa asiwe Mjinga Anadi sera na is maigizo. I hate Lowassa
 
Back
Top Bottom