katibu mkuu wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) ndg Abdulrahman Kinana amewaumbua wanachama na viongozi wa Chama Cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA) baada ya kusema kuwa Viongozi wa Chama hicho wanatoa ahadi feki na matumaini hewa kwa wananchi wakati hawana uwezo wa kufanya maamuzi yeyote kwani Serikali iliyopo ipo Chini ya Chama Cha Mapinduzi (CCM) na ndicho chenye uwezo wa kufanya maamuzi ya kusaidia wananchi.
Kinana ameyasema hayo leo katika mkutano wa hadhara uliofanyika katika uwanja wa Nyangumbu - Geita mjini, ambapo amesema kuwa Viongozi wa CHADEMA wamewalaghai wananchi wa Kijiji cha Mgusu kwa kuwakataza kupokea fedha ya ruzuku kutoka Serikalini kiasi cha Bilioni 3.4 kwa wachimaji wadogo, wakiwadanganya kuwa wakipokea eneo lao litachukuliwa.
Katibu Mkuu huyo wa CCM amesema kuwa CHADEMA wamekuwa na tabia ya kudanganya wananchi, ambapo M/kiti wao Mhe Mbowe alidanganya kuwa anarudisha gari ya KUB lakini ukweli ni kuwa gari hiyo anaitumia mpaka hivi sasa na anaitumia kufanyia magendo ambapo iliwahi kukamatwa nchini Kenya, pia ametaja kuwa Halmashauri ya Karatu inayoongozwa na CHADEMA inaongoza kwa rushwa na ufisadi wa zaidi ya Bilioni 2.
Katibu Mkuu akihutubia maelfu ya wananchi wa Geita mjini katika uwanja wa Nyangumbu
Katibu wa NEC Itikadi na Uenezi Nape Nnauye akihutubia wakazi wa Kalangalala, Nyankumbu Geita ambapo aliwata wananchi hao kutokubali kuyumbishwa na vyama vilivyopoteza muelekeo.
Mbunge wa Viti Maalum mkoa wa Geita Mhe.Vicky Kamata akihutubia wananchi wa Geita.
Kinana ameyasema hayo leo katika mkutano wa hadhara uliofanyika katika uwanja wa Nyangumbu - Geita mjini, ambapo amesema kuwa Viongozi wa CHADEMA wamewalaghai wananchi wa Kijiji cha Mgusu kwa kuwakataza kupokea fedha ya ruzuku kutoka Serikalini kiasi cha Bilioni 3.4 kwa wachimaji wadogo, wakiwadanganya kuwa wakipokea eneo lao litachukuliwa.
Katibu Mkuu huyo wa CCM amesema kuwa CHADEMA wamekuwa na tabia ya kudanganya wananchi, ambapo M/kiti wao Mhe Mbowe alidanganya kuwa anarudisha gari ya KUB lakini ukweli ni kuwa gari hiyo anaitumia mpaka hivi sasa na anaitumia kufanyia magendo ambapo iliwahi kukamatwa nchini Kenya, pia ametaja kuwa Halmashauri ya Karatu inayoongozwa na CHADEMA inaongoza kwa rushwa na ufisadi wa zaidi ya Bilioni 2.
Katibu Mkuu akihutubia maelfu ya wananchi wa Geita mjini katika uwanja wa Nyangumbu
Katibu wa NEC Itikadi na Uenezi Nape Nnauye akihutubia wakazi wa Kalangalala, Nyankumbu Geita ambapo aliwata wananchi hao kutokubali kuyumbishwa na vyama vilivyopoteza muelekeo.
Mbunge wa Viti Maalum mkoa wa Geita Mhe.Vicky Kamata akihutubia wananchi wa Geita.