Inside10
JF-Expert Member
- May 20, 2011
- 33,615
- 40,161
Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA) kimetangaza kutoitambua serikali ya Tanzania iliyozaliwa na uchaguzi wa Oktoba 29, 2025, ikidai kuwa uchaguzi huo uligubikwa na ukiukwaji wa haki, sheria na misingi ya demokrasia.
Katika taarifa yao kwa umma iliyotolewa na Makamu Mwenyekiti wa CHADEMA Bara, John Heche, Desemba 11, 2025, CHADEMA imetaka kuvunjwa kwa Tume Huru ya Taifa ya Uchaguzi (INEC) iliyosimamia uchaguzi huo ikisema tume hiyo “haina uhuru, haina uaminifu na haiwezi kusimamia uchaguzi wa haki.”
Katika maelezo yao, chama kimeorodhesha matukio kadhaa ya kile walichokiita ukandamizaji ikiwamo kuzuiwa kwa shughuli za kisiasa, kufungiwa akaunti za chama, kukamatwa kwa viongozi, kuzimwa kwa mitandao, kutekwa na kupotezwa kwa raia, pamoja na kupigwa risasi kwa wananchi wakati wa uchaguzi, huku ikitaka miili ya watu waliouawa kukabidhiwa kwa familia zao ili “izikwe kwa heshima za Kitanzania.”
Kutokana na matukio hayo CHADEMA imetaka kuundwa kwa Serikali ya Mpito itakayowekwa chini ya uangalizi wa taasisi za kimataifa, kurejesha utulivu na kufungua anga la kisiasa.
Chama hicho kimetoa wito kwa Jumuiya ya Kimataifa kuwawekea vikwazo wote waliotajwa kuhusika katika uhalifu wa kibinadamu, huku kikipendekeza fedha za misaada zisipelekwe serikalini bali kwa asasi huru.
Chanzo Jambo TV
Katika taarifa yao kwa umma iliyotolewa na Makamu Mwenyekiti wa CHADEMA Bara, John Heche, Desemba 11, 2025, CHADEMA imetaka kuvunjwa kwa Tume Huru ya Taifa ya Uchaguzi (INEC) iliyosimamia uchaguzi huo ikisema tume hiyo “haina uhuru, haina uaminifu na haiwezi kusimamia uchaguzi wa haki.”
Katika maelezo yao, chama kimeorodhesha matukio kadhaa ya kile walichokiita ukandamizaji ikiwamo kuzuiwa kwa shughuli za kisiasa, kufungiwa akaunti za chama, kukamatwa kwa viongozi, kuzimwa kwa mitandao, kutekwa na kupotezwa kwa raia, pamoja na kupigwa risasi kwa wananchi wakati wa uchaguzi, huku ikitaka miili ya watu waliouawa kukabidhiwa kwa familia zao ili “izikwe kwa heshima za Kitanzania.”
Kutokana na matukio hayo CHADEMA imetaka kuundwa kwa Serikali ya Mpito itakayowekwa chini ya uangalizi wa taasisi za kimataifa, kurejesha utulivu na kufungua anga la kisiasa.
Chama hicho kimetoa wito kwa Jumuiya ya Kimataifa kuwawekea vikwazo wote waliotajwa kuhusika katika uhalifu wa kibinadamu, huku kikipendekeza fedha za misaada zisipelekwe serikalini bali kwa asasi huru.
Chanzo Jambo TV