Facts1
JF-Expert Member
- Dec 23, 2009
- 307
- 28
Chadema yawasilisha malalamiko
Mashirika ya kimataifa pia yaelezwa
Kauli iliyotolewa na vyombo vya usalama Ijumaa iliyopita na kusomwa hadharani na Mnadhimu Mkuu wa Jeshi la Ulinzi la Wananchi wa Tanzania (JWTZ), Luteni Jenerali Abdulrahman Shimbo, juu ya Uchaguzi Mkuu imezua mambo mapya na sasa Chama cha Demokrsia na Maendeleo kimelalamika rasmi kwa jumuiya ya kimataifa kuwa kuna njama za kuvuruga uchaguzi huo utakaofanyika Oktoba 31, mwaka huu.
Waraka wa Chadema wenye kumbukumbu namba C/HQ/ADM/SG/02/79 uliochapishwa Oktoba 4, mwaka huu na umesainiwa na Mwenyekiti wa Kampeni za urais za Chadema, Profesa Mwesiga Baregu na kupelekwa kwa kiongozi wa mabalozi walioko nchini.
Pia umenakiliwa kwa ofisi zote za kibalozi zilizopo nchini, mashirika ya kimataifa yaliyo nchini, wagombea urais wote na vyombo vya habari.
Waraka huo unasema kuwa Chadema wameguswa na kauli ya Luteni Jenerali Shimbo alipowatahadharisha Watanzania kwamba majeshi na vyombo vya usalama wamejiandaa kuzikabili vurugu zozote zitakazotokea wakati wa uchaguzi huo.
"Pasipo kutoa uthibitisho, Luteni Jenerali Shimbo alieleza hisia kwamba vyombo vya usalama vimepokea taarifa za kiintelijensia zikionyesha kuwepo vyama vya siasa vinavyojiandaa kwa ajili ya vurugu zinazoweza kusababisha umwagaji wa damu nchini," alisema.
Profesa Baregu ameelezea katika waraka huo kuwa ni kitendawili kwa Luteni Jenerali Shimbo kuvitaka vyama vya siasa na wagombea wao kuyakubali matokeo ya Uchaguzi Mkuu wa Oktoba 31, mwaka huu.
"Pamoja na kutambua haja ya majeshi ya ulinzi kuhakikisha utawala wa sheria na taratibu vinafuatwa, hasa wakati huu wa uchaguzi, tunaamini kwamba tamko hilo kwa kipindi hiki cha kampeni za kisiasa, limetolewa kwa pupa na bila vielelezo vyovyote thabiti," alisema.
Alisema Chadema inaliona tamko hilo ni kuingilia dhahiri mchakato wa uchaguzi na kupanga matokeo yake.
Alisema inapaswa kueleweka kwamba tamko la JWTZ ni kinyume cha Katiba na kwa makusudi limevuka mamlaka ya kikatiba kwa kuingilia shughuli za Jeshi la Polisi.
Pia, Profesa Baregu anasema hakuna msingi wa kutoa tamko hilo zito katikati ya kampeni, wakati hakuna uthibitisho wa tukio kubwa linalohatarisha amani na utulivu nchini.
"Nchi hii inatawaliwa kisheria kwa mujibu wa Katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na sheria nyingine zilizopitishwa na Bunge. "Kama kuna watu wanaobainika kujihusisha na vurugu na kuhatarisha amani, jambo ambalo ni kosa la jinai hapa nchini, ni lazima washitakiwe," alisema.
Alisema Chadema haioni mantiki ya vyombo vya usalama kulalamika hadharani badala ya kuchukua hatua za kisheria kudhibiti uvunjifu wa amani na utulivu.
"Kama vyombo vya usalama vina taarifa sahihi ama za kiintelijensia, kwamba zimebaini kuwepo shughuli za jinai, vinapaswa kuchukua hatua mapema kuliko kutoa tamko la kisiasa," alisema.
Profesa Baregu alisema Chadema hakiamini kwamba tamko hilo lilitokana na taarifa zilizokusanywa kutoka katika vyanzo vya kiintelijensia. Badala yake alisema lina shinikizo la kisiasa linalokusudia kuwatisha wapiga kura na kutoa ubashiri kwamba matokeo ya Uchaguzi Mkuu ujao hayatatokana na kura za wananchi bali kwa hila za vyombo vya dola yakiwemo majeshi.
"Tunaamini kwamba mchakato wa kisiasa lazima uachwe bila kuingiliwa na majeshi kama hakuna sababu za msingi kufanya hivyo," alisema. Profesa Baregu alisema ijulikane kwamba tamko la JWTZ lilitolewa wakati kukiwa na mfululizo wa vitendo vya uvunjaji wa Sheria ya Uchaguzi ya mwaka 2010, uliofanywa na mgombea urais kupitia Chama Cha Mapinduzi (CCM), Rais Jakaya Kikwete.
Alisema Rais Kikwete amekuwa akitumia rasilimali za umma katika kampeni zake na katika matukio tofauti alizidisha muda wa kampeni unaotambulika kisheria.
Kwa mujibu wa Profesa Baregu, polisi na vyombo vingine vya usalama vina taarifa kwamba CCM imekuwa ikitoa mafunzo kwa kikundi cha Green Guards ambacho kinahusika kufanya vurugu kwenye mikutano ya kampeni ya Chadema.
Profesa Baregu alitaja baadhi ya maeneo yanayosadikiwa kuwa Green Guards wa CCM walifanya vurugu dhidi ya Chadema kuwa ni katika majimbo ya Busanda, Moshi Mjini na Ubungo. "Hakuna hatua zilizochukuliwa na Tume ya Taifa ya Uchaguzi licha ya malalamiko yetu kadhaa," alisema.
Pia Profesa Baregu alisema hivi karibuni gazeti la serikali la Daily News, lilitangaza matokeo ya mshindi wa urais kabla ya kufanyika kwa Uchaguzi Mkuu.
Alisema kutokana na hali hiyo, Chadema imetuma waraka kwa jumuiya ya kimataifa ambapo nakala zake zimesambazwa kwa balozi za nje na mashirika ya wahisani, ili wataimbue hali hiyo. Profesa Baregu alisema Chadema inaamini kuwa Nec itatimiza wajibu wake kuhakikisha kuwa Uchaguzi Mkuu unafanyika kwa huru na haki na kwamba uamuzi wa wananchi unaheshimiwa.
Ijumaa iliyopita Shimbo akiwa amefuatana viongozi waandamizi wa Jeshi la Polisi aliwaambia waandishi wa habari Makao Makuu ya Jeshi hilo kuwa vyombo vya ulinzi na usalama vimejiandaa kukabiliana na vurugu wakati wa Uchaguzi Mkuu na kuvitaka vyama vya siasa na wagombea kuyakubali matokeo yatakayotangazwa na Tume ya Taifa ya Uchaguzi (Nec).
Katika tamko hilo lililoelezwa ni la pamoja kati ya JWTZ na Polisi, limezuia mjadala kwa kada tofauti nchini, huku watu wengi wakimkosoa kwa mitazamo tofauti.
Mashirika ya kimataifa pia yaelezwa
Kauli iliyotolewa na vyombo vya usalama Ijumaa iliyopita na kusomwa hadharani na Mnadhimu Mkuu wa Jeshi la Ulinzi la Wananchi wa Tanzania (JWTZ), Luteni Jenerali Abdulrahman Shimbo, juu ya Uchaguzi Mkuu imezua mambo mapya na sasa Chama cha Demokrsia na Maendeleo kimelalamika rasmi kwa jumuiya ya kimataifa kuwa kuna njama za kuvuruga uchaguzi huo utakaofanyika Oktoba 31, mwaka huu.
Waraka wa Chadema wenye kumbukumbu namba C/HQ/ADM/SG/02/79 uliochapishwa Oktoba 4, mwaka huu na umesainiwa na Mwenyekiti wa Kampeni za urais za Chadema, Profesa Mwesiga Baregu na kupelekwa kwa kiongozi wa mabalozi walioko nchini.
Pia umenakiliwa kwa ofisi zote za kibalozi zilizopo nchini, mashirika ya kimataifa yaliyo nchini, wagombea urais wote na vyombo vya habari.
Waraka huo unasema kuwa Chadema wameguswa na kauli ya Luteni Jenerali Shimbo alipowatahadharisha Watanzania kwamba majeshi na vyombo vya usalama wamejiandaa kuzikabili vurugu zozote zitakazotokea wakati wa uchaguzi huo.
"Pasipo kutoa uthibitisho, Luteni Jenerali Shimbo alieleza hisia kwamba vyombo vya usalama vimepokea taarifa za kiintelijensia zikionyesha kuwepo vyama vya siasa vinavyojiandaa kwa ajili ya vurugu zinazoweza kusababisha umwagaji wa damu nchini," alisema.
Profesa Baregu ameelezea katika waraka huo kuwa ni kitendawili kwa Luteni Jenerali Shimbo kuvitaka vyama vya siasa na wagombea wao kuyakubali matokeo ya Uchaguzi Mkuu wa Oktoba 31, mwaka huu.
"Pamoja na kutambua haja ya majeshi ya ulinzi kuhakikisha utawala wa sheria na taratibu vinafuatwa, hasa wakati huu wa uchaguzi, tunaamini kwamba tamko hilo kwa kipindi hiki cha kampeni za kisiasa, limetolewa kwa pupa na bila vielelezo vyovyote thabiti," alisema.
Alisema Chadema inaliona tamko hilo ni kuingilia dhahiri mchakato wa uchaguzi na kupanga matokeo yake.
Alisema inapaswa kueleweka kwamba tamko la JWTZ ni kinyume cha Katiba na kwa makusudi limevuka mamlaka ya kikatiba kwa kuingilia shughuli za Jeshi la Polisi.
Pia, Profesa Baregu anasema hakuna msingi wa kutoa tamko hilo zito katikati ya kampeni, wakati hakuna uthibitisho wa tukio kubwa linalohatarisha amani na utulivu nchini.
"Nchi hii inatawaliwa kisheria kwa mujibu wa Katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na sheria nyingine zilizopitishwa na Bunge. "Kama kuna watu wanaobainika kujihusisha na vurugu na kuhatarisha amani, jambo ambalo ni kosa la jinai hapa nchini, ni lazima washitakiwe," alisema.
Alisema Chadema haioni mantiki ya vyombo vya usalama kulalamika hadharani badala ya kuchukua hatua za kisheria kudhibiti uvunjifu wa amani na utulivu.
"Kama vyombo vya usalama vina taarifa sahihi ama za kiintelijensia, kwamba zimebaini kuwepo shughuli za jinai, vinapaswa kuchukua hatua mapema kuliko kutoa tamko la kisiasa," alisema.
Profesa Baregu alisema Chadema hakiamini kwamba tamko hilo lilitokana na taarifa zilizokusanywa kutoka katika vyanzo vya kiintelijensia. Badala yake alisema lina shinikizo la kisiasa linalokusudia kuwatisha wapiga kura na kutoa ubashiri kwamba matokeo ya Uchaguzi Mkuu ujao hayatatokana na kura za wananchi bali kwa hila za vyombo vya dola yakiwemo majeshi.
"Tunaamini kwamba mchakato wa kisiasa lazima uachwe bila kuingiliwa na majeshi kama hakuna sababu za msingi kufanya hivyo," alisema. Profesa Baregu alisema ijulikane kwamba tamko la JWTZ lilitolewa wakati kukiwa na mfululizo wa vitendo vya uvunjaji wa Sheria ya Uchaguzi ya mwaka 2010, uliofanywa na mgombea urais kupitia Chama Cha Mapinduzi (CCM), Rais Jakaya Kikwete.
Alisema Rais Kikwete amekuwa akitumia rasilimali za umma katika kampeni zake na katika matukio tofauti alizidisha muda wa kampeni unaotambulika kisheria.
Kwa mujibu wa Profesa Baregu, polisi na vyombo vingine vya usalama vina taarifa kwamba CCM imekuwa ikitoa mafunzo kwa kikundi cha Green Guards ambacho kinahusika kufanya vurugu kwenye mikutano ya kampeni ya Chadema.
Profesa Baregu alitaja baadhi ya maeneo yanayosadikiwa kuwa Green Guards wa CCM walifanya vurugu dhidi ya Chadema kuwa ni katika majimbo ya Busanda, Moshi Mjini na Ubungo. "Hakuna hatua zilizochukuliwa na Tume ya Taifa ya Uchaguzi licha ya malalamiko yetu kadhaa," alisema.
Pia Profesa Baregu alisema hivi karibuni gazeti la serikali la Daily News, lilitangaza matokeo ya mshindi wa urais kabla ya kufanyika kwa Uchaguzi Mkuu.
Alisema kutokana na hali hiyo, Chadema imetuma waraka kwa jumuiya ya kimataifa ambapo nakala zake zimesambazwa kwa balozi za nje na mashirika ya wahisani, ili wataimbue hali hiyo. Profesa Baregu alisema Chadema inaamini kuwa Nec itatimiza wajibu wake kuhakikisha kuwa Uchaguzi Mkuu unafanyika kwa huru na haki na kwamba uamuzi wa wananchi unaheshimiwa.
Ijumaa iliyopita Shimbo akiwa amefuatana viongozi waandamizi wa Jeshi la Polisi aliwaambia waandishi wa habari Makao Makuu ya Jeshi hilo kuwa vyombo vya ulinzi na usalama vimejiandaa kukabiliana na vurugu wakati wa Uchaguzi Mkuu na kuvitaka vyama vya siasa na wagombea kuyakubali matokeo yatakayotangazwa na Tume ya Taifa ya Uchaguzi (Nec).
Katika tamko hilo lililoelezwa ni la pamoja kati ya JWTZ na Polisi, limezuia mjadala kwa kada tofauti nchini, huku watu wengi wakimkosoa kwa mitazamo tofauti.