CHADEMA Yasambaratisha CCM Iramba Mashariki

CHADEMA Yasambaratisha CCM Iramba Mashariki

Hongereni chadema kwa kufanikiwa kazi ya kumuua mama yake zitto.

Khaaa, ninahakika kama wewe ni mwajiriwa popote, basi unaofanya kazi hua wanakuogopa balaa kwa majungu na Uongo!!!! CDM inahusikaje na kifo cha bimkubwa!?
 
ulea leane kaka! Jana nilikuwepo nkungi hivi unaweza kufananisha na ule mkutano wa kinana? Tuwe wakweli na tuache ushabiki pembeni!

Kwa hakika jana palikuwa patupu na wewe uwe mkweli kabisa ndugu yangu! Nilikuja nikitokea shelui nilipitia msingi, gumanga, nduguti hadi nkungi lakini cdm jana mumeaibika sana!

Nitaweka picha ili umati ujionee wenyewe! Kati ya kinana na mbwembwe zenu za jana!

pia mkuu tuwe wakweli mikutano yote ya kinana watu wanasombwa na malori na kujazwa sehemu moja ili kuwahadaa watz kwamba maccm bado watu wanawapenda, sasa kama ww ni mkweli hebu kuwa mkweli na kwa hili.
 
mnajifariji wenzenu wana dola; wapinzani wakichukua nchi jeshi itachukua hatamu ya uongozi wa nchi
kuwa na jeshi pamoja na dora vilikuwa na mwanzo wake kama vitakavyokuwa na mwisho. Kwa bahati mbaya (kwako) cdm wanaiangalia kesho kuanzia hapa walipo wakati wewe ukiingalia leo tu!
 
Umati mkubwa wa wananchi uliofurika katika mkutano wa hadhara wa CHADEMA Kata ya Nkungi Jimbo la Iramba Mashariki leo umesababisha shughuli zote kusimama kwa zaidi ya saa tatu.

Mkutano huo ulihutubiwa na viongozi kadhaa wa kitaifa na mkoa wakiongozwa na Mkurugenzi wa Sera na Utafiti Mwita Mwikabe Waitara na Kamanda maarufu wa Chadema katika Jimbo hilo George Gunda.

Akizungumza katika mkutano huo Kamanda George alishambulia CCM kwa umaskini wa wananchi na sera mbovu za huduma ya Afya.

Kamanda George pia alilaani CCM kutukana matusi viongozi wa Chadema wakati walipohutubia jimboni humo.

Kamanda George ambaye ni mwiba kwa CCM na amekuwa akiwatia sana ujasiri vijana wa jimbo hilo aliwataka wananchi wajiandae kuing'oa CCM katika chaguzi zote zijazo wakianzia na Serikali za Mitaa.

Naye Mwita Waitara aliyekuwa mgeni Rasmi ameendelea kuzungumzia umuhimu wa wananchi kujitambua na kuikataa CCM huku akifurahishwa na umati mkubwa wa watu waliojitokeza.

Waitara pia alizungumzia umuhimu wa wananchi kuunganisha nguvu katika suala la Katiba mpya na kuunga mkono Rasimu ya Tume ya Warioba ambapo umati mkubwa ulipiga kelele kwamba unataka Serikali Tatu.

Baadaye mamia ya wananchi wamechukua kadi mpya za Chadema huku wengine wengi wakirudisha kadi za CCM.

Kati ya waliorudisha kadi ni vijana zaidi ya 20 waliopewa kadi za CCM wiki mbili tu zilizopita na Katibu Mkuu wa CCM alipotembelea Kata hiyo.

"The best fruits will be found only onto slow growing trees"
 
msaada; hivi hili jimbo ndilo la mchumi numberi one tz?
 
Ulea leane kaka! Jana nilikuwepo Nkungi hivi unaweza kufananisha na Ule mkutano wa Kinana? Tuwe wakweli na tuache ushabiki pembeni!

Kwa hakika Jana palikuwa patupu na wewe uwe mkweli kabisa ndugu yangu! Nilikuja nikitokea Shelui nilipitia Msingi, Gumanga, Nduguti hadi Nkungi lakini CDM Jana mumeaibika sana!

Nitaweka Picha ili umati ujionee wenyewe! Kati ya Kinana na mbwembwe zenu za Jana!

Na yale malori mliyolipiwa na Halmashauri kusomba watu wilaya za jirani ndiyo yalileta umati wa Kinana?
 
Tumeshuhudia mikutano ming ya chadema ikihudhuriwa na watu wengine pia mkisingizia wengine wamerudisha kadi za ccm,lakin mwisho wa siku mnajua tunavyo wabwaga. Sera alizo ongelea bwana george ni zile zile tunazo zijua za chadema kwani hazina updates siku zote. Sisi ni wakazi wa Iramba mashariki na tunatoka hicho hicho kijiji KWA HIYO TUNA JUA CCM IMEFANYA NN NA IMETULETEA NINI, TUWE WA WAZI NDUGU ZANGU NA CHADEMA ONDOENI WAZO KUWA SIKU MOJA MTALICHUKUWA JIMBO LA IRAMBA MASHARIKI. KIDUMU CHAMA CHA MAPINDUZI
 
Hivi angekufa mama yake ni kiongozi yoyote wq Chadema kutoka kaskazini mikutano ya chama ingeendelea.

Mbona Mbunge wenu wa CCM kafiwa na Baba yake lakini Kinana na Nape, Pia Mwigulu wameendelea na Ziara zao na kujifanya kutoa Pole katika mikutano ya hadhara je pole hizo zina maana yeyote kulingana na hiki ulichokiandika?
 
Tumeshuhudia mikutano ming ya chadema ikihudhuriwa na watu wengine pia mkisingizia wengine wamerudisha kadi za ccm,lakin mwisho wa siku mnajua tunavyo wabwaga. Sera alizo ongelea bwana george ni zile zile tunazo zijua za chadema kwani hazina updates siku zote. Sisi ni wakazi wa Iramba mashariki na tunatoka hicho hicho kijiji KWA HIYO TUNA JUA CCM IMEFANYA NN NA IMETULETEA NINI, TUWE WA WAZI NDUGU ZANGU NA CHADEMA ONDOENI WAZO KUWA SIKU MOJA MTALICHUKUWA JIMBO LA IRAMBA MASHARIKI. KIDUMU CHAMA CHA MAPINDUZI
 
Hivi angekufa mama yake ni kiongozi yoyote wq Chadema kutoka kaskazini mikutano ya chama ingeendelea.
mbona kuna kiongozi wa CCM kafiwa na baba yake mzazi na Kinana anaendelea tu na Mikutano na JK yupo NYC anakula kuku na warembo....unacheka ----- la mwenzio wakati lako liko wazi
 
Majaji wangapi wamehudhuri msiba wa mama xito?
 
Back
Top Bottom