CHADEMA yapasuka vipande vipande kuna uwezekano wa kutoshiriki uchaguzi ujao kwa visingizio dhaifu

Lucas Mwashambwa

JF-Expert Member
Jul 28, 2022
15,270
9,716
Ndugu zangu watanzania,

Kwa sasa hali ni mbaya sana sana ndani ya CHADEMA ,chama kimepasuka na kugawanyika vipande vipande.hakuna maelewano,hakuna mipango wala mikakati ya pamoja,hakuna mshikamano wala umoja wa wanachama na viongozi ndani ya chama hicho,hakuna Dira wala muelekeo wa pamoja wala lugha ya pamoja ndani ya nyumba hiyo.

Hakuna sera za pamoja,hakuna ajenda za pamoja ndani ya chadema kwa sasa,hakuna maono wala misingi ya chama inayowaunganisha CHADEMA kwa sasa.kila mtu kivyake ,kila mtu na anavyoamini na njia za kufikia.kila mtu na njia yake ,kila mtu na muelekeo wake,kila mtu na misamiati yake,hakuna msimamo wa pamoja kama chama.

Kila mmoja anajiendea anakotaka mwenyewe,kila mmoja anazungumza lugha yake mwenyewe na kuielewa mwenyewe lugha hiyo,kila mmoja na mikakati na mipango yake,kila mmoja na Dira yake ,kila mmoja anajiona yupo sahihi na anajiona yeye ndiye anapaswa mawazo yake kuongoza chama.chama hakina msemaji wala mwenyekiti wa kuheshimika,kila mmoja anamwenyekiti wake na katibu wake na msemaji wake anayemuamini akizungumza. Chama kimebaki kama mkusanyiko wa kondoo waliotelekezwa na mchungaji wake na kubakia wakitanga tanga.

Kwa sasa ndio maana hakuna habari za mikutano wala operation, kwa kuwa hakuna maelewano mazuri kati ya mwenyekiti wa chama na makamu wake,hakuna maelewano kati ya wanachama na uongozi wa juu,hakuna imani na kuaminiana miongoni mwa viongozi wenyewe, kila mmoja yupo upande wake kwa malengo yake binafsi na siyo chama.

Tuhuma na kutuhumiana ndiko kumetawala ndani ya CHADEMA, hisia za usaliti na kusalitiana ndiko kumeteka hisia za chama chote kuanzia juu mpaka chini,kila mmoja akimuona mwenzake ni msaliti na anakisaliti chama.

Lissu kaona isiwe shida kaamua kususa chama na shughuli zote za chama,kaamua kuwa mbali na chama,kaamua kuangalia mambo mengine,kaamua kunyoosha mikono juu.kaona sasa CHADEMA ni kama ipo katika ujenzi wa mnara wa Babeli ambapo ni lugha gongana ndio iliyotawala ndani ya chama,hakuna kusikilizana wala wa kusikilizwa.hakuna cha mkubwa wala mdogo,wote ni makambale na wote ni mabeberu walioota ndevu na wote ni mafahari ndani ya Zizi ,kila mmoja anangurumaa kwa sauti nzito kuonyesha umwamba wake na kwamba yeye ndiye mkubwa na mbabe .

Sasa yasemekana kuna uwezekano chama hicho kisishiriki uchaguzi wowote kati ya mwakani na mwaka unaofuata.maana umoja na mshikamano umevunjika na kinaona hakiwezi kupata wala kuambulia chochote kile katika uchaguzi wowote ule ambao kitashiriki. Kwakuwa hakina nguvu kutokea ndani yake ambayo ndio msingi wa ushindi kwa chama chochote kile kuwa na umoja na mshikamano kutokea ndani yake kabla ya kwenda kupambana nje.

Tuendelee kutulia kuangalia mnyukano unaoendelea ndani ya chama hicho kinachorusha lawama kwa baadhi ya viongozi wake wa juu kuwa wanajichotea na kujipakulia sana minyama ya Minofu laini laini na kujinenepesha wao huku chama na wanachama wakiendelea kukondeana na kudhoofika kila uchwao.

Kazi iendelee, mama Ametufikia na kuwafikia watanzania kwa utumishi wake uliotukuka wa kugusa maisha ya watanzania wanyonge wasio na Sauti.

Lucas Hebel mwashambwa, Kijana mzalendo na mpenda nchi yangu.

0742-676627.
 
Kama ungekuwa huweki namba ya simu ningeyaheshimu mawazo yako, lakini kwa hiyo namba uliyoweka hapo, unaonesha dhahiri wewe ni mwepesi usiyejiweza kwa chochote hapo ulipo, simply unasubiri kupigiwa simu upozwe na chochote, hivyo sioni sababu kwangu ya kuyaheshimu hayo mawazo yako, unaonekana haupo huru kimawazo wala kiuchumi, hili ni jukwaa la walio huru wewe katafute jukwaa lako.
 
Kama ungekuwa huweki namba ya simu ningeyaheshimu mawazo yako, lakini kwa hiyo namba uliyoweka hapo, unaonesha dhahiri wewe ni mwepesi usiyejiweza kwa chochote hapo ulipo, simply unasubiri kupigiwa simu upozwe na chochote, hivyo sioni sababu kwangu ya kuyaheshimu hayo mawazo yako, unaonekana haupo huru kimawazo wala kiuchumi, hili ni jukwaa la walio huru.
Jikite kwenye hoja ambayo ipo mezani.
 
Eti ndugu zangu Watanzania kwa sasa CDM imepasuka, Hali ni mbaya Sana + Blah blah nyingiiii.......hili tangazo au habari umetuletea? Hembu katengueni hukumu ya mama aliyekutwa na nyama ya swala, Watanzania wamechoka na ubovu wenu.
 
Eti ndugu zangu Watanzania kwa sasa CDM imepasuka, Hali ni mbaya Sana + Blah blah nyingiiii.......hili tangazo au habari umetuletea? Hembu katengueni hukumu ya mama aliyekutwa na nyama ya swala, Watanzania wamechoka na ubovu wenu.
Kwani hukumu ya yule mama inaondoa vipi ukweli wa Chadema kupasuka na kukosa mshikamano ndani yake
 
Tanzania hakuna uchaguzi, bali Kuna maonyesho ya ujinga wa mtu Mweusi kwenye box la kura. Mtu mjinga tu ndio ataendelea kushiriki chaguzi hizi za kishenzi.
Kwani Mbowe na Lissu walikuwaga wanaingia kupitia uchaguzi upi au kwa njia ipi? Au walikuwa wanajipeleka wenyewe Bungeni?
 
Ndugu zangu watanzania,

Kwa sasa hali ni mbaya sana sana ndani ya CHADEMA ,chama kimepasuka na kugawanyika vipande vipande.hakuna maelewano,hakuna mipango wala mikakati ya pamoja,hakuna mshikamano wala umoja wa wanachama na viongozi
Wameshakutumia na yakutolea.
 
Kwani mbowe na Lissu walikuwaga wanaingia kupitia uchaguzi upi au kwa njia ipi? Au walikuwa wanajipeleka wenyewe Bungeni?
Narudia tena, mtu mpuuzi tu ndio ataendelea kushiriki hizi chaguzi za kihayawani. Ni aidha machafuko, ama mapinduzi ya kijeshi ili heshima ya box la kura irejee. Lakini hakuna mwanaume anayesimamisha vizuri atapoteza muda wake kwenye mstari wa kura eti anachagua viongozi, huku majizi ya ccm yameshaingia na matokeo mfukoni. Mtasimama watu wachache mno msiojitambua kwenye mistari ya kura kushiriki huo ushenzi.
 
Kama ungekuwa huweki namba ya simu ningeyaheshimu mawazo yako, lakini kwa hiyo namba uliyoweka hapo, unaonesha dhahiri wewe ni mwepesi usiyejiweza kwa chochote hapo ulipo, simply unasubiri kupigiwa simu upozwe na chochote, hivyo sioni sababu kwangu ya kuyaheshimu hayo mawazo yako, unaonekana haupo huru kimawazo wala kiuchumi, hili ni jukwaa la walio huru wewe katafute jukwaa lako.
Huyu njaa imeondolewa ufahamu, akili na utu. Amebakia na kichwa kopo. Kila siku anajitahidi kuandika ujinga wa aina fulani akitarajia ataonwa. Hajiamini wala hajielewa. Anatarajia maisha yake yatatengenezwa na watu wengine. Haelewi afanye nini ili maisha yake yasiyo na uelekeo yapate njia.
 
HATA KWENYE KUANDAA MAANDAMANO HAYA KUNA MPASUKO MKUBWA KWA SABABAU LISSU ANAWACHONGANISHA WANANCHI NA DOLA HUKU AKIJUA FAMILIA YAKE AMEIPELEKA NJE YA NCHI KWA HIYO WTAKAO UWAWA NA KUUMIA NI WANANCHI AMBAO HAWNA UWEZO WA KUWAPELEKA WATOTO WAO MAREKANI. TAZAMA VIDEO CHINI
 
Ndugu zangu watanzania,

Kwa sasa hali ni mbaya sana sana ndani ya CHADEMA ,chama kimepasuka na kugawanyika vipande vipande.hakuna maelewano,hakuna mipango wala mikakati ya pamoja,hakuna mshikamano wala umoja wa wanachama na viongozi ndani ya chama hicho,hakuna Dira wala muelekeo wa pamoja wala lugha ya pamoja ndani ya nyumba hiyo.

Kil

0742-676627.
CDM kilichoifanya SSM kuweka katiba mpya kwapani kinagawanyika? Hata chawa hawajafika ulipo
 
Nadhani ingekuwa vema kwako ungeshughulikia tatizo la akili yako kugawanyika vipande vipande kiasi kwamba huna faida kwa jamii yako wala Taifa.
Bams ungeacha wenye akili Timamu wajadili hoja hii huku wewe ukiendelea na hoja za kulingana na upeo wako na akili yako.maana hoja hii ni kubwa sana kwako na imekuzidi kimo cha akili yako.
 
Back
Top Bottom