Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA), Kanda ya Kaskazini kimemsimamisha Katibu wa Kamati ya Sheria na Haki za Binadamu wa chama hicho, Odero Charles Odero kupisha uchunguzi dhidi ya tuhuma zinazomkabili.
Odero ambaye alikuwa miongoni mwa wagombea wa nafasi ya uenyekiti ndani ya Chadema, majukumu yake kama mjumbe sekretarieti ya kanda pia yatasimama
Katika uchaguzi wa ndani wa Chadema uliofanyika Januari 21, 2025 alikuwa akichuana na Freeman Mbowe aliyekuwa akitetea nafasi ya uenyekiti na Tundu Lissu ambaye mwisho wa uchaguzi aliibuka mshindi
Odero alishika nafasi ya tatu kwa kupata kura moja. Lissu alipata kura 513 na Mbowe akipata kura 482. Jumla ya kura zilizopigwa zilikuwa 999 na halali zikiwa 996 huku tatu zikiharibika
Taarifa ya kusimamishwa kwa Odero ndani ya Chadema Kanda ya Kaskazini imetolewa jana Jumatano, Julai 30, 2025 na Katibu Kanda ya Kaskazini, Ndonde Totinan baada ya kupokea tuhuma dhidi ya kada huyo kuwa mwenendo usioridhisha
Asubuhi ya leo Alhamisi, Julai 30, 2025, Mwananchi limemtafuta Odero ambaye amesema barua ya kusimamishwa kwake aliipokea usiku wa jana Jumatano. Hata hivyo, hakueleza kwa kina tuhuma hizo zinazoelezwa iwapo anazifahamu
Chanzo: Mwananchi
Katika uchaguzi wa ndani wa Chadema uliofanyika Januari 21, 2025 alikuwa akichuana na Freeman Mbowe aliyekuwa akitetea nafasi ya uenyekiti na Tundu Lissu ambaye mwisho wa uchaguzi aliibuka mshindi
Odero alishika nafasi ya tatu kwa kupata kura moja. Lissu alipata kura 513 na Mbowe akipata kura 482. Jumla ya kura zilizopigwa zilikuwa 999 na halali zikiwa 996 huku tatu zikiharibika
Taarifa ya kusimamishwa kwa Odero ndani ya Chadema Kanda ya Kaskazini imetolewa jana Jumatano, Julai 30, 2025 na Katibu Kanda ya Kaskazini, Ndonde Totinan baada ya kupokea tuhuma dhidi ya kada huyo kuwa mwenendo usioridhisha
Asubuhi ya leo Alhamisi, Julai 30, 2025, Mwananchi limemtafuta Odero ambaye amesema barua ya kusimamishwa kwake aliipokea usiku wa jana Jumatano. Hata hivyo, hakueleza kwa kina tuhuma hizo zinazoelezwa iwapo anazifahamu
Chanzo: Mwananchi